Mama anavutia sana; aliolewa na mwamame mmoja sasa wanaume waliokataliwa wanapiga misele tena

MKEHA

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
714
1,137
Kwa urembo na uzuri wa mama, wanaume wengi walipenda kuwa nae ili awe mke wao. Lakini kati ya wanaume hao wengi ni baba tu aliyebahatika kumuoa mama. Baba alijitahidi sana kuchakarika ili familia yake iwe njema kwa kufanya kazi zake kwa juhudi kubwa sana na maarifa.

Na ni kweli toka nizaliwe sijawahi lala njaa kwani baba anajitahidi sana kuleta sembe, mchele, maharage,mafuta, sukari na vyakula vingine kede wa kede.

Pamoja na kuwa mama aliolewa na baba lakini kumbe bado wale wanaume wengine walikuwa na nia nae waliendelea kumfuatilia mama wakitamani baba atoweke siku moja ili wapate nafasi ya kumchumbia tena mama.

Kuna siku baba aliacha kwenda kwenye kijiwe cha kahawa ambapo alikuwa akikutana na wenzake kupiga stori baada ya muda wa kazi, zilipita kama siku tano hizi bila kufika kijiweni wala kuoneka kwenye mishe mishe zake. Lakini pamoja na hayo yote sisi tuliendelea kula kama kawaida na huduma zingine ziliendelea kama kawaida.

Sisi kama familia tulijua kila kitu kuwa baba yupo ila ameamua kuishi tofauti na watu walivyo zoea kwamba muda baada ya kazi lazima aende kijiweni kwa mzee Ntiruhungwa anywe kahawa huku mazungumzo mengine ya siasa na michezo yakiendelea. Baada ya kubadili mfumo wa maisha yake acha vurugu zianze sana nyumbani kwetu.

Wale wanaume waliowahi kumchumbia mama wakaanza visa, mara warushe mawe juu ya paa la nyumba yetu, mara mawe kwenye madirisha yetu. Ilikuwa ni kama vita.

Wengine wakitoka vilabuni wanaputa karibu na nyumbani kwetu wakiimba nyimbo za kashfa juu ya baba yetu. Lakini familia yetu kimyaaaaaaa.

Wanaume wengine walifikia hatua ya kwenda kwa viongozi wa dini wakitaka eti ndoa ya baba na mama ivunjike kwani baba hatimizi tena wajibu wake kwa mama kana kwamba wanalala chumbani kwa wazazi wetu. Walishinikiza watoto tuseme baba alipo, tulipewa pipi, biskuti na zawadi nyingine ili tusema wapi baba alipo.

Kuna wengine walikuja na barua za posa wakutaka mama aolewe tena kwani mmewe ambaye ni baba yetu hawamwoni tena kijiweni na ile tabia ya kutupigia hadithi usiku wapita njia hawaisikii tena.

Tulifuatwa kila sehemu tuseme wapi baba alipo. Baada ya siku kupita mara huyo, Stori itaendelea wiki ijayo. USIKOSE KUFUATILIA KISA HIKI SIKU NYINGINE
 
Acha longolongo wewe! Mwambie BABA yako arudi kijiweni akachangamane na wazee wenzake. Kwa nini abadili tu ghafla utaratibu wake wa maisha na kuanza kujificha ndani? Kama anaumwa, nyinyi kama watoto pamoja na huyo mama yenu, mna wajibu wa kuwajulisha marafiki zake.
 
Mnajifanya anacheza mind games mkidhani hizi ni zama za kale, kwa taarifa yako watu wameshaamka, sasa hivi wanawachora tu nyie majizi ya kura na wamwaga damu.
 
Mambo wa wazazi wako yamekujaje huku jamani, watoto wa siiu hizi wanafikir kila kitu ni uzi.
Soma taratibu mkuu utamuelewa, lazima atuambie baba yake alipo!! Maana Yule baga wa ufipa mkimbizi wa kujitakia kwa beberu anaulizia kila siku na uzushi kibao.
 
Mnajifanya anacheza mind games mkidhani hizi ni zama za kale, kwa taarifa yako watu wameshaamka, sasa hivi wanawachora tu nyie majizi ya kura na wamwaga damu.
hatimaye umeshtuka kwamba mmepewa tangopoli.

muwe na akiba ya maneno,shwaini.
 
hatimaye umeshtuka kwamba mmepewa tangopoli.

muwe na akiba ya maneno,shwaini.

Pitia post zangu toka mwanzo, mimi nilisema siamini chochote kinachosemwa sasa, bali niko Kwenye hatua ya juu zaidi nikifanya maombi jizi la kura litangulie mbele ya haki. Maombi yangu haya yako kabla ya hiyo tetesi, na yataendelea kuwepo. Yaani nia yangu ni so advanced ya hilo unaloita tango pori.
 
Huko ni wapi huko kumekaa ki-rock sana?. Miaka hii kuna mambo ya kishamba kama hayo?. Shuleni unaenda kwelii wewe au kazi yako kuangalia uzuri wa mamaako na kucheck msambwanda wa mamaako?
 
Pitia post zangu toka mwanzo, mimi nilisema siamini chochote kinachosemwa sasa, bali niko Kwenye hatua ya juu zaidi nikifanya maombi jizi la kura litangulie mbele ya haki. Maombi yangu haya yako kabla ya hiyo tetesi, na yataendelea kuwepo. Yaani nia yangu ni so advanced ya hilo unaloita tango pori.
Kuna mwenzako nilimwambia tushindane kusali.

Mimi nakaa upande wa mema,yeye akae huo wake akakimbia. Hana uhakika hata na mungu anayemwomba,anafahamu anachokifanya ni kuwanga wala si sala.

kwahiyo nawewe mkuu, nikutakie sala njema.ila kumbuka,Mungu wetu hafanyii kazi majungu.
 
Back
Top Bottom