Elections 2010 Malumbano ndani ya basi

Tuko

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
11,178
7,320
Hivi majuzi nilikuwa katika safari ya kuelekea katika vijjiji fulani, kukatokea malumbano ambayo yalinisisimua sana. Basi lilikuwa limejaa sana, konda 'anapanga' abiria. Abiria hawakufurahi lakini hakukuwa na option kwani hakukuwa na basi jingine linaloenda huko na barabara ni mbovu. Ndani ya basi alikuwepo bibi ambaye naye alikuwa analalamika kuwa anabanwa sana na anaumia. Kijana mmoja akamwambia yule bibi 'bibi usilalamike, shida yote hii inaletwa na nyie wazee mnaomchagua Kikwete' Kwa kweli yule bibi alikuwa mkali ajabu, analalamika 'kwa nini nilaumiwe mim... mbona nyie vijana hampigi kura mkamchagua huyo Lipumba (Inaonekana bibi alikuwa namfaham tu Kikwete na Lipumba). Bibi aliendelea kulalamika kwa muda mrefu kuwa kwanza kule kwenye gari walikuwepo wazee wawili tu, na vijana wengi... 'sasa kama nyie mnaona sisi wazee tunamchagua Kikwete, kwa nini nyie ambao ni wengi hampigi kura mkamchagua Lipumba au hiyo CHADEMA' aliendelea kulalama bibi huyo huku akishangiliwa na abiria wengi...

Msg niliyopata ni kuwa vijana hatupigi kura, na hata wazee wetu wanalijua hilo.

Vijana tubadilike mwaka huu (ingawa najua kwa bahati mbaya wengi hatujajiandikisha)..
 
Kweli kabisa Tuko vijana wengi hawajajiandikisha au hawataki kupiga kura lakini ndio wanaoongoza kulalamika.
 
Hivi majuzi nilikuwa katika safari ya kuelekea katika vijjiji fulani, kukatokea malumbano ambayo yalinisisimua sana. Basi lilikuwa limejaa sana, konda 'anapanga' abiria. Abiria hawakufurahi lakini hakukuwa na option kwani hakukuwa na basi jingine linaloenda huko na barabara ni mbovu. Ndani ya basi alikuwepo bibi ambaye naye alikuwa analalamika kuwa anabanwa sana na anaumia. Kijana mmoja akamwambia yule bibi 'bibi usilalamike, shida yote hii inaletwa na nyie wazee mnaomchagua Kikwete' Kwa kweli yule bibi alikuwa mkali ajabu, analalamika 'kwa nini nilaumiwe mim... mbona nyie vijana hampigi kura mkamchagua huyo Lipumba (Inaonekana bibi alikuwa namfaham tu Kikwete na Lipumba). Bibi aliendelea kulalamika kwa muda mrefu kuwa kwanza kule kwenye gari walikuwepo wazee wawili tu, na vijana wengi... 'sasa kama nyie mnaona sisi wazee tunamchagua Kikwete, kwa nini nyie ambao ni wengi hampigi kura mkamchagua Lipumba au hiyo CHADEMA' aliendelea kulalama bibi huyo huku akishangiliwa na abiria wengi...

Msg niliyopata ni kuwa vijana hatupigi kura, na hata wazee wetu wanalijua hilo.

Vijana tubadilike mwaka huu (ingawa najua kwa bahati mbaya wengi hatujajiandikisha)..

Unadhani ushindi wa KIKWETE wa 2005 ulitokana na kura za wazee? Hapa sikubaliani na wewe kwa sababu vijana walio wengi ambao walishiriki katika uchaguzi walimpa kura KIKWETE hususan vijana wasomi wa vyuo vikuu .Nakumbuka siku moja JK alitembelea chuo kikuu cha mlimani kabla hajatangaza nia ya kugombea 2005,ambapo vijana wengi walimfuata na kumtaka awanie nafasi ya urais. Napenda nikueleze kwamba vijana wengi bado wana imani na kikwete na watampa kura zao katika uchaguzi 2010. Hivyo, ushindi wa kikwete katika uchaguzi ujao hautatokana na kura za wazee tu bali pia kura za vijana
 
Unadhani ushindi wa KIKWETE wa 2005 ulitokana na kura za wazee? Hapa sikubaliani na wewe kwa sababu vijana walio wengi ambao walishiriki katika uchaguzi walimpa kura KIKWETE hususan vijana wasomi wa vyuo vikuu .Nakumbuka siku moja JK alitembelea chuo kikuu cha mlimani kabla hajatangaza nia ya kugombea 2005,ambapo vijana wengi walimfuata na kumtaka awanie nafasi ya urais. Napenda nikueleze kwamba vijana wengi bado wana imani na kikwete na watampa kura zao katika uchaguzi 2010. Hivyo, ushindi wa kikwete katika uchaguzi ujao hautatokana na kura za wazee tu bali pia kura za vijana
Natumai hata mwaka huu wanafunzi wa vyuo vikuu watapiga kura kumchagua Kikwete wakiwa majumbani mwao huku wakiwa walijiandikisha katika vituo vya sehemu wanaposoma na wakati huo vyuo vitakuwa havijafungiliwa wakati wa uchaguzi
 
Natumai hata mwaka huu wanafunzi wa vyuo vikuu watapiga kura kumchagua Kikwete wakiwa majumbani mwao huku wakiwa walijiandikisha katika vituo vya sehemu wanaposoma na wakati huo vyuo vitakuwa havijafungiliwa wakati wa uchaguzi

Pumba!
 
Walikuwa wanamwamini na sasa wameona pumba zake. Subili Oct 31, 2010. Hata mimi ni k=ijana nilimpa lakini nimeona ni careless kiasi gani". By the way, hata wazee nao wameanza kujua kuwa JK hafai. wajukuu zao wanakufa sababu ya kukosa dawa n.k!!!!!!!
 
Back
Top Bottom