Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,320
Hivi majuzi nilikuwa katika safari ya kuelekea katika vijjiji fulani, kukatokea malumbano ambayo yalinisisimua sana. Basi lilikuwa limejaa sana, konda 'anapanga' abiria. Abiria hawakufurahi lakini hakukuwa na option kwani hakukuwa na basi jingine linaloenda huko na barabara ni mbovu. Ndani ya basi alikuwepo bibi ambaye naye alikuwa analalamika kuwa anabanwa sana na anaumia. Kijana mmoja akamwambia yule bibi 'bibi usilalamike, shida yote hii inaletwa na nyie wazee mnaomchagua Kikwete' Kwa kweli yule bibi alikuwa mkali ajabu, analalamika 'kwa nini nilaumiwe mim... mbona nyie vijana hampigi kura mkamchagua huyo Lipumba (Inaonekana bibi alikuwa namfaham tu Kikwete na Lipumba). Bibi aliendelea kulalamika kwa muda mrefu kuwa kwanza kule kwenye gari walikuwepo wazee wawili tu, na vijana wengi... 'sasa kama nyie mnaona sisi wazee tunamchagua Kikwete, kwa nini nyie ambao ni wengi hampigi kura mkamchagua Lipumba au hiyo CHADEMA' aliendelea kulalama bibi huyo huku akishangiliwa na abiria wengi...
Msg niliyopata ni kuwa vijana hatupigi kura, na hata wazee wetu wanalijua hilo.
Vijana tubadilike mwaka huu (ingawa najua kwa bahati mbaya wengi hatujajiandikisha)..
Msg niliyopata ni kuwa vijana hatupigi kura, na hata wazee wetu wanalijua hilo.
Vijana tubadilike mwaka huu (ingawa najua kwa bahati mbaya wengi hatujajiandikisha)..