Malengo yangu kwa mtaji wa milioni tano

Malengo yangu kwa mtaji wa milioni tano

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2013
Posts
1,056
Reaction score
1,869
Habar wanajamvi, mimi ni muajiriwa katika shirika lisilo la kiserikali na pia najishughulisha na kilimo cha machungwa na mahindi na pia ni mfugaji wa kuku wa kienyeji chotara aina ya kuroiler. Kutokana kwamba kazi niliyokuwa nayo ni ya mkataba na mkataba unaelekea mwishoni ila mpaka mwisho wa mwaka nitakuwa nimekusanya kiasi kisichopungua milioni tano ila malengo yangu ni haya yafuatayo kwani niko Muheza Tanga ambapo mazao mengi yanakubali

Kununua poli la ekari tano kwa Tsh milioni mbili

Kufyeka na kulima kwa trekta kwa Tsh laki tano

Kununua mbegu za mahindi hybrid kwa garama ya Tsh 250000

Gharama za kupandia mahindi ni TSh 200000

Gharama ya palizi mbili ni laki tano
Gharama za madawa ni TSh 20000
Pia baada ya hapo natarajia ekari Tatu nipande michungwa kwa Gharama ya Tsh 250000

Na ekari mbili kasoro Robo nipande mikorosho na pia nitaacha Robo ekari kwa ajili ya makazi na ufugaji wa kuku.

Jumla ya garama ni 3770000

*mimi mwenyewe ni mtaalam wa kilimo na mifugo hivyo shughuli nyingine kama kupuliza dawa na kuandaa miche nitakuwa nafanya mwenyewe.

Pesa iliyobaki ni ya dharura na pia nitakuwa bado nipo kazini kwa mwaka mmoja mbele hivyo pesa ya kutumia nitakuwa napata

Naombeni ushauri kwa hilo wazo langu kama lina mapungufu au halifai

Ahsanteni
 
Habar wanajamvi, mimi ni muajiriwa katika shirika lisilo la kiserikali na pia najishughulisha na kilimo cha machungwa na mahindi na pia ni mfugaji wa kuku wa kienyeji chotara aina ya kuroiler. Kutokana kwamba kazi niliyokuwa nayo ni ya mkataba na mkataba unaelekea mwishoni ila mpaka mwisho wa mwaka nitakuwa nimekusanya kiasi kisichopungua milioni tano ila malengo yangu ni haya yafuatayo kwani niko Muheza Tanga ambapo mazao mengi yanakubali

Kununua poli la ekari tano kwa Tsh milioni mbili

Kufyeka na kulima kwa trekta kwa Tsh laki tano

Kununua mbegu za mahindi hybrid kwa garama ya Tsh 250000

Gharama za kupandia mahindi ni TSh 200000

Gharama ya palizi mbili ni laki tano
Gharama za madawa ni TSh 20000
Pia baada ya hapo natarajia ekari Tatu nipande michungwa kwa Gharama ya Tsh 250000

Na ekari mbili kasoro Robo nipande mikorosho na pia nitaacha Robo ekari kwa ajili ya makazi na ufugaji wa kuku.

Jumla ya garama ni 3770000

*mimi mwenyewe ni mtaalam wa kilimo na mifugo hivyo shughuli nyingine kama kupuliza dawa na kuandaa miche nitakuwa nafanya mwenyewe.

Pesa iliyobaki ni ya dharura na pia nitakuwa bado nipo kazini kwa mwaka mmoja mbele hivyo pesa ya kutumia nitakuwa napata

Naombeni ushauri kwa hilo wazo langu kama lina mapungufu au halifai

Ahsanteni
Wazo zuri
Plani imetulia.
Nakuabalisha kitu ambacho ni muhimu sana :- mchanganuo wa hayo mahesabu yalitumia muda wa ziada wa akili yako, Yaani ulitulia na kuelekeza uwezo wako wa kufikiri.
Sasa
Ili hayo mahesabu yako yatimie kivitenda ongeza pesa laki 5 ya kibanda cha wewe kukaa shambani hadi uhakikishe ,na laki 5 nyingine ya matumizi.
Usipofanya hivyo, hiyo 5m itaishia kwenye kununua shamba na kungoa visiki.
 
Wazo zuri
Plani imetulia.
Nakuabalisha kitu ambacho ni muhimu sana :- mchanganuo wa hayo mahesabu yalitumia muda wa ziada wa akili yako, Yaani ulitulia na kuelekeza uwezo wako wa kufikiri.
Sasa
Ili hayo mahesabu yako yatimie kivitenda ongeza pesa laki 5 ya kibanda cha wewe kukaa shambani hadi uhakikishe ,na laki 5 nyingine ya matumizi.
Usipofanya hivyo, hiyo 5m itaishia kwenye kununua shamba na kungoa visiki.
Ahsante sana mkuu
 
Daaaah wazo zuri sana tena una uzoefu na hayo unayotarajia kuyafanya basi naamin mungu atakusaidia kwa yote sababu una nia na uthubutu.
Mungu akutangulie.
 
Hii iko vzr Namungu akipenda ntakuja kukutembelea kwa nia ya kujifunza kwako mkuu
 
Ule uzi wako wa kuacha kazi uliishia wapi mkuu Naona umebadilisha na user name
 
Hilo shamba la mahindi ni kwa ajiri ya chakula cha familia au biashara?
 
Back
Top Bottom