Malawi Kiboko kwa Intelijensia

Sasa wewe unataka kuwafundisha Tanzania ambao wamepigana vita vyao na vya wengine? usitake ncheke!

ukisoma zaidi btn lines, ktk vita ya uganda Tanzania ndiyo iliyoshindwa. Taarifa za uchunguzi wa kivita ilionesha kuwa Uganda ilikuwa na war intelgence kali zaidi, ushahidi unaonesha kuwa watanzania walipofika kampala na entebe walikuta mipango yote ya vita ya tanzania ikiwa mezani. Amini aliondoka nchini kwa kuwa wananchi wake na jeshi lake hawakumuunga mkono kwa kuwa walikuwa wamechoshwa na udikteta wake. Wamalawi wanalitaka ziwa Malawi kwa kuwa kisheria nila kwao na hawana eneo lingine lenye resources nyingi kama hili.

Watanzania tungejua kupigana vita tungekuwa tulisha appeal mapema kwani si mara ya kwanza kwa malawi kutangaza kuwa ziwa ni lao. Hata tukienda mezani tuapeleka silaha gani, mtanzania hupi atatetea hoja?!, nikupe mifano inayoonesha jinsi tanzania tusivyokuwa na wazalendo khasa kwenye international arena: tulipeleka wawakilishi kule japani kuzungumzia mpango wa uvunaji wa samaki aina ya Tuna, TZ kama moja yenye tuna wengi, iliandikwa kuwa wawakilishi wetu walihongwa vidosho na kukubali mpango wa uvunaji wa tuna uliokuwa umebuniwa na walafi.

Fikiria hata kisa cha ml. Kili kuingizwa ktk maajbu ya dunia, wahusika waliuchuna ili makampuni yetu ya simu yapate kipato kwa text, nchi nyingine kupiga kura ilikuwa bure na hatimaye table mountain ya S.A ikashinda. Unayaona haya?.
 
Si tu kwamba Tanzania
haina viongozi, bali pia hata wananchi wa kuongozwa hakuna. Akili matope
kabisa! Nashawishika kuamini kuwa waanzisha thread hizi na masapota
wake ni watu wenye interest na Malawi lakini si watanzania.

you are right! wengine hapa inaonyesha si watanzania halisi!mfano dharau kwa wanajeshi wetu, inawezekana pia wakawa ni wamalawi wakiwa kazini!lkn upande wang tz iko mahali pa salama!
 
binafsi yule Mwanajeshi
alitudanganya sana na inapaswa afanye hvy kwan silaha za nchi ni siri ya
jeshi, ile kambi ya Gongo la Mboto sio kubwa sana kati ya Kambi kubwa
Tz. Ninaweza nikasema hata Lugaro ni kubwa sana kwa hiyo kambi ya
M/mboto.

Tatizo ni kwamba watu wanataka waambiwe kila kitu.kwa taarifa yenu kuna habari ambazo hata ndani ya majeshi wanaifahamu wachache,kwa ajili tu ya usalama wa nchi,sasa nyie wamalawi mnaojaribu kuleta habari zenu hapa,jidanganyeni na malawi yenu!
 
hawa wa tz wanajaribu tu kuzuia mikutano ya chadema na kutunyang'anya mademu zetu
 

Ni kweli kabisa ndugu yangu. Jumanne hii pia kuna watu wa Interpol wameingia hapa kutoka Malawi, yaani wamalawi.
 
mote ni watz...wanajaribu kuisaidia tz kuondokana na huu utitiri wa uzembe wa wana usalama wetu...wamekalia kupleka watu mabwepande huku malawi wakijaza vijana wao wa kazi kuisoma nchi yetu...
Tatizo ni kwamba watu wanataka waambiwe kila kitu.kwa taarifa yenu kuna habari ambazo hata ndani ya majeshi wanaifahamu wachache,kwa ajili tu ya usalama wa nchi,sasa nyie wamalawi mnaojaribu kuleta habari zenu hapa,jidanganyeni na malawi yenu!
 
umeona eeh...na bado..wataingia wengi tu!naamini malawi hawatakubali tugawane hilo ziwa..
Ni kweli kabisa ndugu yangu. Jumanne hii pia kuna watu wa Interpol wameingia hapa kutoka Malawi, yaani wamalawi.
 
check na hii ramani kutoka google earth...inaonekana tz hatuna chetu pale...ila tukomae tu huenda tukaambulia kipande japo kidogo...View attachment 61983


Ukizidi ku-zoom in zaidi utaona huo mpaka wa nyasa una rangi nyekundu kuonyesha kuwa kuna eneo la mgogoro kama ilivyo Abyei kati ya Sudan na Sudan Kusini.
 
 


Mkuu hivi unafikiri wamalawi ni wazalendo kwasasa?Nikutaarifu basi hakuna taifa lililogawanyika kwa kisiasa kwasasa kama Malawi hasa baada ya kifo cha Bingu Wa Muthalika,mpaka kuna habari za chini ya kapeti kuwa wapinzani wanamtega Mama Banda ili kumdhoofisha kisiasa na ndiyo wanaokuza haya mambo ya vita. Sipendi vita lakini siamini kushindwa vita kama tutafikia huko.
 
Zomba we sema tumepigana tu na tuna uzoefu....kwa taarifa yako kwa sasa tumebaki na intelijensia ya kuwapeleka watu mabwepande, mpaka tunashtuka jamaa watakuwa wameshamchukua Vasco na kuondoka nae...

Wakimchukua Vasco itakuwa jambo la maana sana na hakuna kwenda kupigana kumdai arudishwe,wakae nae tu!!!kudadadeki
 
usitudanganye hapa! we unadhani data kuhusu vitu hivyo viko tu! ok wakijua tuna akiba na silaha za kutosha wao inawasaidia nini? wao tangu mwanzo walisema km Tz itaanzisha vita wao wataenda kushtaki kwa jumuia za kimataifa! Tz tumewazidi Malawi kwa ubora na ukubwa wa jeshi! katafute data
 

Usilolijua ni sawa na usiku wa giza,Ni vigumu kujua habari za kijeshi za nchi hasa Tanzania kama ilivyo vigumu kwa ngamia kupita katika tundu la sindano,kwa wale waliopitia Jeshi wanajua nini ninachokiongea,siyo mchezomchezo mnaozungumzia hapa,huo ujumbe utakuwa unafuatiliwa kwa hatua wanazotembea,gesture kwa wale wanaopishana nao hata kusalimiana nao, walichobeba, mazungumzo hata ya simu,hadi wanavyopepesa macho bila wao kujua,hata magari,wanapokula kulala na hata picha wanazochukua watu wanaoongea nao yaani kuna watu wamesomea kazi hiyo ya upelelezi kisaikologia na kuhitimu vilivyo,akikuangalia anakusoma hadi unachofikiria au unachotaka kuongea na lengo lako ni nini turudi nyuma wakati wapigania uhuru wa Afika kusini walivyokuwa hapa na base zao za mafunzo ya kupiga huko kusini,hiyo chuki iliyokuwepo lakini waliishindwa kabisa TZ

Bado Msumbiji,Zimbabwe,Angola hata huko Malawi kwenyewe, kuitangazia vita TZ ni sawa na kuzitangazia vita hizo nchi nilizozitaja hakuna pa kutokea hawa wanatuogopa kuliko nchi yoyote duniani kwani wanajua fika mafigo yetu na mikono yetu ilivyo mirefu,hadi leo hizo nchi tulizozikomboa hazijalipa fadhila kwa TZ,wanasubiri yeyote atuchokoze wapate nafasi ya kulipa hizo fadhila,kama ilivyokuwa Uganda.pomoja na hayo operation za kijeshi hazifanyiki mchana ni usiku tena ule mnene pakipambazuka wako pirini katikati hakuna hata mtu anayeweza kuona achilia mbali kuhisi,na kwa utaratibu wa kijeshi utambulisho wako ni neno la siri ambalo linabadilika kila muda hata ukiwa mmoja wao ukashindwa kujitambulisha kwa neno la siri wakati huo,adhabu yake ni mbaya inaweza kuwa hata kifo kwa kuhisi kuwa mpelelezi au msaliti fulani hivi unaetoa siri za jeshi kwa raia au nje.hakuna jasusi aliyeweza kujipenyeza katika intelijensia ya jeshi akapona huyo hayupo,hata uraiani kwa masuala ya kijeshi hayupo hata mmoja kwa nchi yetu hii takatifu ya Tanzania.
 
inawezekana kweli mpaka wa ziwe uwe mashariki kabisa ya ziwa bila tz kupata hata kipande?
 
Na hiyo ilikuwa mali yao wamalawi - Nyasaland enzi hizo. Je, wanaikana.

 
Tusidanganyane hapa jamani. Hii thread haina maana. Ni kama tunataka kulikuza tu suala hili. Hawo watu wanakuja kutembea tu. Sikatai, inawezekana wapo wachache kama ambavyo nasisi tunao kule kwao ila chamsingi, mpaka sasa mimi sioni dalili ya vita. Pamoja na mambo ya Mwabepande, bado naamini Tanzania tuna one of the best intelligence system katika bara la Afrika. Hatubabaishwi kabisa katika hilo
 
Wamalawi wako makini sana katika kuamua hatima yao. Nimesoma magazeti na blogs zao nyingi za kwao nimegundua wamalawi wengi wako against vita baina yao na sisi, na wengi wanatutambua kama majirani zao wa karibu na wa siku nyingi. Wapo walevi wachache kama i(ilivyo huku) pia wanaoshabikia vita. Nionavyo serikali yao imepima upepo na kuligundua hilo, kwamba vita kamwe haitakuwa kwa maslahi ya wamalawi wala watanzania; ndiyo maana wameamua kulipeleka suala hili mbele ya vyombo vya kisheria vya kimataifa ili kupata suluhu. Binafsi nazipongeza hatua za hivi karibuni za serikali ya Malawi kuongeza mahusiano yake na sisi na nashauri sisi pia tufanye hivyo ili kuepusha uhasama usio wa lazima uliozalishwa na historia yetu ya kutawaliwa. Wote, wamalawi na watanzania wana madai ya haki kabisa kudai kama wanavyodai; Mkoloni alikabidhi Nyasaland ramani inayoonyesha nchi hiyo kumiliki ziwa lote, kwetu alikabidhi ramani ambapo Tanzania ilionekana kumiliki nusu ya eneo la maji ya ziwa na UN baadae walithibitisha nadharia ya umilikaji wa nusu ya eneo la maji pale ambapo mipaka ya nchi inakutana na ziwa au maji. Ni kwa mantiki hayo inapaswa pande zote kuketi na kuzungumza nini kifanyike ili udugu na ushirikiano uliodumu karne nyingi uendelee. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.
 
hivi mnafkiri japanese naval force imekuja nchini by default at this time!!??

Jiulize, livefire exercise ya mwaka huu kwanini itafanyika brigade 401(kusini)?? Hizo delegation hazina lolote, mama banda anajaribu kujiweka karibu maana majasusi wake walimwambia zaidi ya malori 90 yenye silaha nzito zilizofunikwa na maturubai yalipelekwa mbeya na ruvuma

pia mjapani ametangaza kuna "uwezekano" wa jwtz naval command kufanya nao mazoezi.., kwnn saivi tunahitaji naval exercise now na nchi kisiwa wataalam wa amphibious operations??!

Unajua mjapan amekuja na meli ngapi?? Zina nini ndani? JWTZ ni zaidi ya mnavyoijua..., its a secret society, JWTZ inaheshimika africa, hawakurupuki,

Be a great thinker, read between lines..., moshe dayan staki kusema mengi.., just be a GREAT THINKER!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…