Malalamiko: TIGO Tanzania

Malalamiko: TIGO Tanzania

huku Tanga,muda jioni,intanet yao inakuwa slow zaidi ya mwendo wa konokono.Tigo jirekebisheni.
 
Hawa tigo ni wazi sana nimeamua kuivunja laini yao. Nimeweka vocha nikajiunga kifurushi, nimepiga simu mpaka muda umeisha ghafla inaingia meseji wamenikopesha 1300 nitalipa 1500. Sikuhitaji kukopa wala kukopeshwa. ....

Ulikuwa Hujui Hilo mkuu?
Jamaaa wezi balaaa hawa siwezi ndo vile tenaaaa huwezi kuwakwepa aiseee
 
Yawezekana ni maagizo toka kwa maccm kutafuta pesa za uchaguzi kwa hali yoyote ile.si unajua wahisan wamekata kamba na uchaguzi mkuu mwakani.
 
Utafiti unaonesha kwamba jumla ya muda wa hewani ambao watanzania wanautumia kwa masaa 24 tu, ni sawa na jumla ya muda wa hewani unaotumiwa na watu wa Denmark kwa miezi mitano...!!!
 
Nimeweka vocha ya elfu moja wamechukua nimeongeza na elfu nyingine wamechukua pesa yao. Sasa nashangaa nani amewaambia wanikopeshe?
 
jana wamenikera sana hawa tg ,najiunga nikitegemea kupata dakika 25 na mb 75 matokeo yake napata dakika 20 na 50 mb kwa sh499 huu ni wiz wanafanya hawajali wateja wao ,inabid kugomea hii mitandao yao
 
mmh! Hizi comedy sasa. Mbona badiliko kubwa sana! Au ilikuwa promo! Ngoja nisubiri airtel sasa, maana voda kimeshanuka, laini nimeweka kwenye kikombe.

Ilibidi niwaulize kwenye page yao FB kama wamekosea ama
la. Wakasema ndio package ilivyo kwa sasa! nikachoka kbs.
 
Team Kulia lia... Mi Nahama mtandao kwani Umelazimishwa kila Siku Upande Basi Moja
 
Mimi nadhani hapa ni kuwa na discipline itasaidia, wazo langu kama unajijua unatumia sana internet basi tafuta mtandao unaona unafaa kwa wakati huo, weka bajeti ya mwezi kulingana na gharama kwa wakati huo, tafuta wireless modem ili iwe rahisi kutumia kwenye device yoyote nikimaanisha ukiwa na shida na internet kwenye simu basi unaunga wireless hivyo hivyo kwenye laptop, kama ofisini kwako kuna internet basi hakikisha mahitaji yako ya internet unayamalizia ofisini haswa haswa muda wa lunch au jioni kabisa after office hours hiyo itakuondolea gharama za internet, kwenye kuongea mimi nashauri tujijengee tabia ya kupiga simu pale palipo na ulazima kama kuulizia mambo fulani au kwa simu za kibiashara ambazo zitaingia faida, wengi wetu tunapiga simu halafu tunaanza story au umbea au tunaitafuta point kwa mazungumzo marefu jambo ambalo sio sahihi, mfano mimi nikipiga simu basi kuna huo ulazima na nikipigiwa simu huwa nauliza vp mbona umenipigia na kama huna point nitakuambia samahani nitumie message. Hii imenisaidia kupunguza gharama, na mtandao ninaotumia kama hujajipanga basi huwezi nipigia simu ovyo.
 
Hawa tigo ni wazi sana nimeamua kuivunja laini yao. Nimeweka vocha nikajiunga kifurushi, nimepiga simu mpaka muda umeisha ghafla inaingia meseji wamenikopesha 1300 nitalipa 1500. Sikuhitaji kukopa wala kukopeshwa. ....

Mkuu,cha kufanya wee jiunge moja kwa moja bila ya kuweka vocha yani jiunge moja kwa moja na kifurushi mi wakinifanyiaga uhuni huwa nafanya hivyo baada ya muda wanaanza kutuma msg zao za kutia tia huruma oooh tunaomba uongeze salio ili kulipia deni ulilokopa tarehe kadha huwa naziangalia tu baada ya hapo najiunga na kifurushi moja kwa moja,kwa kweli hawatutendei haki aisee.
 
Back
Top Bottom