Malalamiko kwa wandishi wa habari

Malalamiko kwa wandishi wa habari

Ketoka

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2015
Posts
1,121
Reaction score
1,981
Mimi sio mwandishi wa habari lakini sielewi kwa nini wandishi wanapotosha jamii kiasi hiki

Mtu hupata maarifa kutokana na vyanzo mbalimbali,miongoni mwa vyanzo vya maarifa ni magazeti

Mwanafunzi wa darasa la saba akikutana na gazeti kama hili limeandika TRA ya Kenya ,huyu mwanafunzi moja kwa moja ataelewa kuwa kumbe mamlaka ya mapato Kenya nayo inaitwa TRA

Wandishi wa Tanzania mnaendelea kuwafanya watanzania waendelee kuwa mbumbumbu ,wasiendelee kuelewa mambo,kwa uandishi huu Tanzania bado tupo nyuma sana
IMG_1532586093601.jpg
 
Uliyeleta Uzi huu una hoja ya maana sana. Waandishi wengi wa habari wamekuwa ni kioo kibovu sana katika jamii. Hata kiswahili wamechangia kwa kiasi kikubwa kukiaharibu. Jana nimemsikia mtangazaji akisema "hazara hiyo iliuzuriwa na watu wengi"
 
Lakini kaweka apostrophe sijui akimaanisha nini
 
Mimi sio mwandishi wa habari lakini sielewi kwa nini wandishi wanapotosha jamii kiasi hiki

Mtu hupata maarifa kutokana na vyanzo mbalimbali,miongoni mwa vyanzo vya maarifa ni magazeti

Mwanafunzi wa darasa la saba akikutana na gazeti kama hili limeandika TRA ya Kenya ,huyu mwanafunzi moja kwa moja ataelewa kuwa kumbe mamlaka ya mapato Kenya nayo inaitwa TRA

Wandishi wa Tanzania mnaendelea kuwafanya watanzania waendelee kuwa mbumbumbu ,wasiendelee kuelewa mambo,kwa uandishi huu Tanzania bado tupo nyuma sanaView attachment 819296
Hahahahahaha!! kwani wanatofauti na kiongozi wako jiwe aliye sema Saadam Hussein alikuwa Rais wa Kuwait?
 
Hahahahahaha!! kwani wanatofauti na aliye sema Saadam Hussein alikuwa Rais wa Kuwait?
Kweli bwana,hivi ukikutana na mtu anabisha kijiweni kuwa mamlaka ya mapato Kenya inaitwa TRA usishangae hata kidogo
 
Taaluma ya habari na utangazaji Tz ni ukanjanja mtupu..yaani wamejaa watu wasiojua mambo kabisa..sijui tcra wanafanya kazi gani..haiwezekani mwanahabari akosee na kusema mamlaka ya mapato na ushuru ya Kenya kuwa ni Tra ya Kenya!!
 
'TRA ya kenya' hakika tuna tatizo kubwa sana ktk hii sekta ya habari
 
Sijasoma Uandishi wa habari lakini kwa kuwa taaluma yangu inahusika na maana katika maandishi naweza kusema mwandishi hajapotoka sana. Kuna kitu kinaitwa 'eye catching words'. Maneno ambayo yatawavutia wasomaji. Kama mwandishi angeandika KRA badala ya TRA sijui kama kuna watu wangapi wanajua KRA ni nini. Ingewabidi wasomaji wengi wasome kwanza ndio wajue hata KRA ni kitu gani. Lakini kuitumia TRA tayari msomaji wa Kitanzania anakua amepata picha kichwani mwake maana ya hiyo hiyo habari. Matumizi ya single quotation mark '...' mojawapo ni pale unapoweka neno kutoka lugha nyingine au jipya. Hivyo mwandishi katumia sanaa katika uandishi. TRA sio neno la lugha tofauti wala jipya bali ni neno lililoingizwa kwenye muktadha mpya lakini unaoshabihiana. Hiyo imeondoa ukavu wa habari na kuipa mvuto wa kisanii (Literariness). Sidhani kama tunahitaji habari katika lugha kavu kavu tu.
 
Tatizo kubwa kwenye habari hii naliona kwa wasomaji. Maoni yanaonesha wazi uelewa wa matumizi ya lugha (Language use) kwenye jamii uko chini. Habri iko sahihi kabisa kwani inafikisha ujume uliokusudiwa kirahisi zaidi na kimvuto zaidi. Lakini, wasomaji wanauelewa wa sanaa ya matumizi ya lugha?
 
waandishi wa Tanzania ni janga la taifa kwani wanaongoza kwa upotoshaji na pia wanaongeza idadi ya wajinga kwani kuna watu wanaamini kila kinachoandikwa magazetini au kutangazwa kwenye vyombo vya habari bahati mbaya baraza la habari limefumbia macho tatizo hili na kusubiri hadi wapewe malalmiko lakini serikali ikichua hatua wanakuwa wa kwanza kulalamika ila wangepambana na tatizo hili ingekuwa vigumu serikali kuingilia kati sasa hivi nimeacha kusikiliza radio kwani nako kunaupotoshaji mkubwa kwa magzeti nasoma ya kiingereza haya ya kiswahili yanatia kichefuchefu
 
Sijasoma Uandishi wa habari lakini kwa kuwa taaluma yangu inahusika na maana katika maandishi naweza kusema mwandishi hajapotoka sana. Kuna kitu kinaitwa 'eye catching words'. Maneno ambayo yatawavutia wasomaji. Kama mwandishi angeandika KRA badala ya TRA sijui kama kuna watu wangapi wanajua KRA ni nini. Ingewabidi wasomaji wengi wasome kwanza ndio wajue hata KRA ni kitu gani. Lakini kuitumia TRA tayari msomaji wa Kitanzania anakua amepata picha kichwani mwake maana ya hiyo hiyo habari. Matumizi ya single quotation mark '...' mojawapo ni pale unapoweka neno kutoka lugha nyingine au jipya. Hivyo mwandishi katumia sanaa katika uandishi. TRA sio neno la lugha tofauti wala jipya bali ni neno lililoingizwa kwenye muktadha mpya lakini unaoshabihiana. Hiyo imeondoa ukavu wa habari na kuipa mvuto wa kisanii (Literariness). Sidhani kama tunahitaji habari katika lugha kavu kavu tu.
Sitaki kupingana na taaluma ya wandishi wa habari huenda ni language use ili kumjengea msomaji picha ya kitu chenyewe

Nakuja kwenye impact ya habari kwenye jamii

Ukiwa kama Mzee wa familia unachukua gazeti kama hilo unaenda nalo nyumbani,mwanao anachukua hilo gazeti anasoma TRA ya Kenya hebu fikiria mwanao kitakachomuijia kichwani kuwa kumbe na Mamlaka ya mapato Kenya nayo inaitwa TRA,Sasa kadri anavyokuwa anajua hivyo hivyo,siku akikutana na mtu mwingine atamwambia Kenya kuna TRA sio KRA,madhara yake sasa tunakuja na kizazi ambacho hakijui mambo ,mbumbumbu
 
Sitaki kupingana na taaluma ya wandishi wa habari huenda ni language use ili kumjengea msomaji picha ya kitu chenyewe

Nakuja kwenye impact ya habari kwenye jamii

Ukiwa kama Mzee wa familia unachukua gazeti kama hilo unaenda nalo nyumbani,mwanao anachukua hilo gazeti anasoma TRA ya Kenya hebu fikiria mwanao kitakachomuijia kichwani kuwa kumbe na Mamlaka ya mapato Kenya nayo inaitwa TRA,Sasa kadri anavyokuwa anajua hivyo hivyo,siku akikutana na mtu mwingine atamwambia Kenya kuna TRA sio KRA,madhara yake sasa tunakuja na kizazi ambacho hakijui mambo ,mbumbumbu
Cha kwanza mtoto ataelewa kuwa wahusika ni shirika lenye majukumu sawa na TRA Tanzania. Kama ingeandika KRA kwanza huyo mwanao asingeelewa KRA ni mnyama gani. Huko ndani ya habari lazima kuna ufanunuzi nini TRA YA KENYA inamaanisha. Lakini uzuri ni kuwa kichwa cha habari kimefikisha ujumbe bila ukakasi kabisaaa. Jaribu kuwapa watu wakawaida mtaani changamoto waambie wakufafanulie walivyoelewa 1. Waambie Mfanyabiashara wa kenya amekamatwa na KRA 2. Mfanyabiashara amekamatwa na 'TRA YA KENYA'. Uliza kila swali watu tofauti. Waambie wakuambie KRA inamaanisha nini kwenye swali la kwanza na TRA YA Kenya inamaanisha nini kwenye swali la pili. Majibu utayoyapata yatumie mwenyewe. Naamini utaafika uchaguzi wa mwandishi.
 
Back
Top Bottom