Makutano Show
Member
- Aug 3, 2012
- 21
- 65
Wana-JF
Kama nilivyowaambia Jumamosi nilikuwa na Mhe January Makamba ambapopamoja na kuelezea maisha yake ya kawaida ya kisiasa pia alijibumaswali yenu.
Moja ya vitu alivyosema ni kuwa hana mpango wa kugombea Urais. Alisema anaamini nafasi ya urais inahitaji mtu ambaye amejiandaa Kisaikolojia, Kisiasa na Kifikra na kumalizia kwa kusema kuwa Urais sio uamuzi wa mtu mmoja kwa sababu nchi haiendeshwi na mtu mmoja nainahitaji watu ambao wanashauriana, kuandaa dira ya pamoja na kupeleka ujumbe wa kuwaunganisha Watanzania.
Alipoulizwa Rais anayekuja anatakiwa aweje alisema anatakiwa awe ni mtu atakaewaunganisha Watanzania huku akisema mianya ya ukabila, udini na rushwa ambayo babawa taifa Mwalimu Nyerere aliitaja imeanza kuonekana.
Pia Makambaalisema rais ajaye anatakiwa asiwe mtu mwenye hulka ya visasi na anatakiwa awe na uwezo wa kuwaambia wananchi kuwa yeye sio masiha wa kuyafanya maisha yao yabadilike papo kwa hapo kwa kuwa nchi ni ya watu wote, hivyo kila mmoja ana wajibu wa kutumia nafasi yake kuleta mabadiliko.
Alipoulizwa katika wanasiasa wa upinzani ni yupi anamkubali, alimtaja Zitto Kabwe kwa sababu ana uwezo wa kusema na kusimamia kile anachokiamini, ujasiri wa kuomba ushauri kama kuna jambo ambalo halielewi na pia anapenda kusoma na kujifunza. Pia alitaja kuwa anamheshimu sana Profesa Ibrahim Lipumba na wanasiasa wengine wa upinzani.
Pia alizungumzia nguvu ya mitandao ya kijamii, alikubali kuwa imekuwana nguvu katika kuwaunganisha wananchi kudai haki zao na pia kuwakutanisha watu wenye msimamo mmoja na kujadili mambo mbalimbali na akakiri kuwa chama cha mapinduzi kiliachwa nyuma katika hili lakini kwa sasa wanawasisitiza viongozi wote wilayani kujiunga na kuitumia mitandao ya kijamii.
Mahojiano zaidi yanapatikana katika YouTube channel hapa chini
Kama nilivyowaambia Jumamosi nilikuwa na Mhe January Makamba ambapopamoja na kuelezea maisha yake ya kawaida ya kisiasa pia alijibumaswali yenu.
Moja ya vitu alivyosema ni kuwa hana mpango wa kugombea Urais. Alisema anaamini nafasi ya urais inahitaji mtu ambaye amejiandaa Kisaikolojia, Kisiasa na Kifikra na kumalizia kwa kusema kuwa Urais sio uamuzi wa mtu mmoja kwa sababu nchi haiendeshwi na mtu mmoja nainahitaji watu ambao wanashauriana, kuandaa dira ya pamoja na kupeleka ujumbe wa kuwaunganisha Watanzania.
Alipoulizwa Rais anayekuja anatakiwa aweje alisema anatakiwa awe ni mtu atakaewaunganisha Watanzania huku akisema mianya ya ukabila, udini na rushwa ambayo babawa taifa Mwalimu Nyerere aliitaja imeanza kuonekana.
Pia Makambaalisema rais ajaye anatakiwa asiwe mtu mwenye hulka ya visasi na anatakiwa awe na uwezo wa kuwaambia wananchi kuwa yeye sio masiha wa kuyafanya maisha yao yabadilike papo kwa hapo kwa kuwa nchi ni ya watu wote, hivyo kila mmoja ana wajibu wa kutumia nafasi yake kuleta mabadiliko.
Alipoulizwa katika wanasiasa wa upinzani ni yupi anamkubali, alimtaja Zitto Kabwe kwa sababu ana uwezo wa kusema na kusimamia kile anachokiamini, ujasiri wa kuomba ushauri kama kuna jambo ambalo halielewi na pia anapenda kusoma na kujifunza. Pia alitaja kuwa anamheshimu sana Profesa Ibrahim Lipumba na wanasiasa wengine wa upinzani.
Pia alizungumzia nguvu ya mitandao ya kijamii, alikubali kuwa imekuwana nguvu katika kuwaunganisha wananchi kudai haki zao na pia kuwakutanisha watu wenye msimamo mmoja na kujadili mambo mbalimbali na akakiri kuwa chama cha mapinduzi kiliachwa nyuma katika hili lakini kwa sasa wanawasisitiza viongozi wote wilayani kujiunga na kuitumia mitandao ya kijamii.
Mahojiano zaidi yanapatikana katika YouTube channel hapa chini
Last edited by a moderator: