Makundi yenye dalili kujitokeza ndani ya CHADEMA

Mbelwa Germano

JF-Expert Member
May 7, 2011
789
289
Hali ya sasa ya kukubalika kwa kasi kwa CDM inatoa tafsiri nyingi kuhusu mustakabali wa baadaye. Wingi wa Wanachama ni ishara ya kujitokeza kwao kushiriki katika kugombea nafasi mbalimbali ndani ya chama. Lakini kikubwa zaidi cha kutazama ni kwa jinsi gani uteuzi wa wagombea nafasi za udiwani na ubunge zitafanyika. Ni ukweli usiopingika kama CDM wasipokuwa makini kutatokea makundi kama yaliyopo ndani ya CCM na kusababisha loopholes kwa CDM na kutoa mwanya kwa wapinzani(CCM) hivyo kuna kazi ya kujijenga kimuundo na kimkakati.

Kama nilivyotahadharisha awali kunahitajika umakini wa kuwaandaa viongozi wa chama wa wilaya na majimbo ambazo ndio wanasimamia upatikanaji wa wagombea kwa nafasi nilizoeleza awali. Bila kuweka mazingira mazuri makombora ya ufisadi yataelekezwa CDM na kurudisha imani kwa CCM.Ni ukweli usiopingika kama vita ya kuwania uteuzi kwa nafasi hizi itakuwa motomoto kwa CDM.

Kama mdau, unadhani nini kifanyike kuepusha makundi haya.

Nawakilisha
 
Ni kweli lakini kitakachoinusuru CDM ni uwazi na ukweli ambao hata hao wagombea wakijua wameshindwa kihalali basi watabariki matokeo na kuvunja makundi.

Makundi yanakuwa created na kubebana.
 
CDM sio CCM huku hakuna pilau wala vitenge vya bure,nadhani hilo wanalitambua kwa sana.
 
Makundi ni kitu gani. fafanua au wazungumuzia mitazamo tofauti juu ya namna ya kufikia malengo?
 
Ni majundi gani unayoyaongelea hapa??
Mimi naona unatoa angalizo la kuweka uongozi imara katika kula ngazi, then umerukia kwenye makundi. Sijakuelewa!!

Kama mdau, unadhani nini kifanyike kuepusha makundi haya.
 
Ngoja moto uwake hapo ndiyo tutajua kama CDM ina uongozi thabiti au la?vinginevyo yatatokea kama ya ................ Sisi yetu macho na masikio!
 
Nyie ndio mnaosema Chama kijitangaze vijijini lakini kimefanya hivyo na kimeanza kupata wanachama wengi sasa imekuwa tatizo tena kwenu du sijui mnataka wafanyeje
 
Ni hatari kupuuza angalizo alilotoa mtoa mada.
Kama ilivyo CCMN CDM imeundwa Tanzania na Watanzania
Na tukubali tusikubali, ufisadi umekuwa janga la kitaifa
Na kingine ni kuwa kuongoza nchi sio rais tu na Serikali kuu
CDM inapaswa kuwa na mifumo imara ya uongozi toka shina hadi taifa na watu hawa waandaliwe ili kama wapo wanaohamia na makando kando ya ubadhirifu, mfumo uwatambue mapema na kuwadhibiti
Kuhusu makundi: haya huletwa watu wanapotofautiana juu ya kiongozi wamtakae na hili halikwepeki. Kinachoweza kukwepeka ni kuruhusu makundi haya kukiyumbisha chama kama tunavyoona CCM
Udhibiti huu pia utafanikishwa na mfumo wazi na thabiti utakaowekwa wazi katika ngazi zote na yeyote atakayejaribu kukiuka kuadhibiwa bila kucheleweshwa
Kuchelewa kuchukua hatua ni kulea udhaifu
Kwa hiyo si busara kuipuuza hoja iliyotolewa kwa maneno kama CDM si kama CCM
Hata unapokuwa na kampuni yako ndogo na ghafla ikapanuka unapaswa kupitia upya na kuboresha mifumo yako
 
Chadema wana uongozi madhubuti wa kuwadhibiti wanachama wake.

Kama viongozi imara, mifumo imara ni muhimu sana kwa Chama cha Siasa
CCM ilipoanza ilionekana Chama imara
Walikuwa na viongozi imara waliofanya udhaifu wa mifumo yao isionekane
Walipokosa viongozi madhubuti, ghafla kila mtu anaona udhaifu na ubovu wa CCM
Chama kinatakiwa kuwa na mifumo madhubuti itakayomlazimisha kiongozi dhaifu awe imara au atoke na CCM hawana hilo
Imejengwa kwenye unafiki na kulindana
CDM kina bahati ya kuwa na viongozi makini ila kama CCM yawezekana baadae kukatokea kiongozi dhaifu
Ili kutofanya makosa ya CCM, huu ndio wakati wa kuweka mifumo itakayomkabili kiongozi dhaifu kabla hajatokea
 
Makundi ni kitu gani. fafanua au wazungumuzia mitazamo tofauti juu ya namna ya kufikia malengo?
Ndugu yangu Kidzude, ukweli una hulka moja hautaki kupuzwa, CHADEMA kama ilivyo CCM vyote ni vyama vya siasa vilivyoanzisha na watanzania wenye utamaduni unaondendana, tofauti yao ipo kwenye mitazamo. Kukubalika au kutokubalika kwa chama kunatokana na nyakati husika. CCM ya kipindi cha nyuma ilikuwa inakubalika kama CDM inavyoanza kukubalika sasa, kinachowaponza CCM sasa ni dhana nzima ya kimfumo na kimkakati. Yapo makundi ya kufikirika ndani ya CDM ambayo yanaweza kujitokeza na kuathiri chama kama ilivyo sasa kwa CCM.Ninapozungumzia makundi nina maana ya misuguano ya kimaslahi(yawe ya kiuongozi, fedha n.k.) ambayo yana nia ya kudhoofisha chama. Pamoja na CCM kuwa na viongozi imara kipindi cha nyuma kama ilivyo kwa CDM sasa, kimeshindwa kujipanga kimfumo na kimkakati kukabiliana na changamoto za nyakati, a usidhani CDM itakubalika tu kimujiza bila kufocus kimfumo na kimuundo. Viongozi wa CDM ni binadamu tu kama walivyo wa CCM, na ni wajibu wetu kukumbushana.
 
Hali ya sasa ya kukubalika kwa kasi kwa CDM inatoa tafsiri nyingi kuhusu mustakabali wa baadaye. Wingi wa Wanachama ni ishara ya kujitokeza kwao kushiriki katika kugombea nafasi mbalimbali ndani ya chama. Lakini kikubwa zaidi cha kutazama ni kwa jinsi gani uteuzi wa wagombea nafasi za udiwani na ubunge zitafanyika. Ni ukweli usiopingika kama CDM wasipokuwa makini kutatokea makundi kama yaliyopo ndani ya CCM na kusababisha loopholes kwa CDM na kutoa mwanya kwa wapinzani(CCM) hivyo kuna kazi ya kujijenga kimuundo na kimkakati.

Kama nilivyotahadharisha awali kunahitajika umakini wa kuwaandaa viongozi wa chama wa wilaya na majimbo ambazo ndio wanasimamia upatikanaji wa wagombea kwa nafasi nilizoeleza awali. Bila kuweka mazingira mazuri makombora ya ufisadi yataelekezwa CDM na kurudisha imani kwa CCM.Ni ukweli usiopingika kama vita ya kuwania uteuzi kwa nafasi hizi itakuwa motomoto kwa CDM.

Kama mdau, unadhani nini kifanyike kuepusha makundi haya.

Nawakilisha

ni kweli mkuu ulosema naunga mkono so plz naomba utupe mbinu mbadala
 
Ndugu yangu Kidzude, ukweli una hulka moja hautaki kupuzwa, CHADEMA kama ilivyo CCM vyote ni vyama vya siasa vilivyoanzisha na watanzania wenye utamaduni unaondendana, tofauti yao ipo kwenye mitazamo. Kukubalika au kutokubalika kwa chama kunatokana na nyakati husika. CCM ya kipindi cha nyuma ilikuwa inakubalika kama CDM inavyoanza kukubalika sasa, kinachowaponza CCM sasa ni dhana nzima ya kimfumo na kimkakati. Yapo makundi ya kufikirika ndani ya CDM ambayo yanaweza kujitokeza na kuathiri chama kama ilivyo sasa kwa CCM.Ninapozungumzia makundi nina maana ya misuguano ya kimaslahi(yawe ya kiuongozi, fedha n.k.) ambayo yana nia ya kudhoofisha chama. Pamoja na CCM kuwa na viongozi imara kipindi cha nyuma kama ilivyo kwa CDM sasa, kimeshindwa kujipanga kimfumo na kimkakati kukabiliana na changamoto za nyakati, a usidhani CDM itakubalika tu kimujiza bila kufocus kimfumo na kimuundo. Viongozi wa CDM ni binadamu tu kama walivyo wa CCM, na ni wajibu wetu kukumbushana.

mkuu ni kweli kabisa tusikatae ukweli kwani hata ccm walikataa na wanakataa hivihivi na kukifanya chama chao kidolore .haya mambo yapo ! tunataka tuwe na mbinu na mikakati ya kimfumo na kimuundo itakayojaribu kuziba mianya yote ya mipasuko ili kufanya cdm kudumu zaidi na kuleta tumani lililopotezwa na ccm kwa wananchi kwa muda mrefu!
 
Ni majundi gani unayoyaongelea hapa??
Mimi naona unatoa angalizo la kuweka uongozi imara katika kula ngazi, then umerukia kwenye makundi. Sijakuelewa!!

Kama mdau, unadhani nini kifanyike kuepusha makundi haya.

Dada yangu Eliza, mimi sikusema majundi nimesema makundi.Ukweli una hulka moja hautaki kupuzwa, CHADEMA kama ilivyo CCM vyote ni vyama vya siasa vilivyoanzishwa na watanzania wenye utamaduni unaoendana, tofauti yao ipo kwenye mitazamo. Kukubalika au kutokubalika kwa chama kunatokana na nyakati husika. CCM ya kipindi cha nyuma ilikuwa inakubalika kama CDM inavyoanza kukubalika sasa, kinachowaponza CCM sasa ni dhana nzima ya kimfumo na kimkakati (WAMEKATAA UKWELI KAMA WEWE UNAVYOUKATAA SASA). Yapo makundi ya kufikirika ndani ya CDM ambayo yanaweza kujitokeza na kuathiri chama kama ilivyo sasa kwa CCM.Ninapozungumzia makundi nina maana ya misuguano ya kimaslahi(yawe ya kiuongozi, fedha n.k.) ambayo yana nia ya kudhoofisha chama. Pamoja na CCM kuwa na viongozi imara kipindi cha nyuma kama ilivyo kwa CDM sasa, kimeshindwa kujipanga kimfumo na kimkakati kukabiliana na changamoto za nyakati, Na usidhani CDM itakubalika tu kimujiza bila kufocus kimfumo na kimuundo. Viongozi wa CDM ni binadamu tu kama walivyo wa CCM,ni wajibu wetu kukumbushana.

Tambua uongozi wa chama hauanzii makao makuu ya chama. Unaweza kujikumbusha tu kwa mfano ni kwa nini baadhi ya maeneo ya Tanzania CDM walishindwa kusimamisha wagombea? Kujipanga! Narudia kwa kuwa wagombea udiwani na ubunge wanatoka katika ngazi ya jimbo na kwa kuwa mwaka kesho kuna uchaguzi na kwa kuwa 2014 kuna uchaguzi wa kiserikali na 2015 uchaguzi mkuu ipo haja ya kujipanga kimfumo na kimkakati kuepusha misuguano ya kimaslahi na rushwa ndani ya chama.

Naomba ushambulie hoja
.
 
Chadema wana uongozi madhubuti wa kuwadhibiti wanachama wake.

Hata wewe ni kiongozi kwa nafasi yako ya kibinadamu ukiongozwa na fikra, imani na mitazamo yako, jukumu la kujenga chama imara si tu la Mbowe, Dr.Slaa,Zitto, Mnyika au tundu lissu, ni letu sote. Jambo la msingi unalopaswa kufahamu kila binadamu anafanya makosa lakini hatuwezi kujiridhisha tuu na makosa ambayo tunafikiria yanaweza kutokea bila kutumikia fikra zetu katika kutafuta majawabu.
 
sure angalizo lako ni zuri, inabidi tuwe na uwazi ktk mambo yote ya kupata wagombea na viongozi wazalendo na waadilifu

Ndio Mkuu!Bila umakini tutapoteza ujasiri...na tutakapoteza ujasiri tusidhani litakuwa jambo rahisi kwa CDM kurudisha imani ya kizalendo kwa wananchi wa Tanzania
.
 
Wanga wengi!



Viva Chama cha Demokrasia na Maendeleo!

Nadhani umekurupuka kujibu bila kusoma na kutafakari content ya mada yenyewe...unapokosa umakini kinachofuata ni kukosa ujasiri. Kwa mantiki hii umethihirisha wewe ni mwanga wa kwanza:

Wanga wengi!

Viva Chama cha Demokrasia na Maendeleo!

Ungekuwa una fikra tulivu kama za makamanda wa CDM ungeona umantiki wa mada yenyewe.
 
Back
Top Bottom