Makundi ya AFCON 2021

mshale21

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
2,049
4,904
Droo ya michuano ya kombe la mataifa ya Afrika AFCON 2021 imepangwa jana, huku vigogo na mabingwa watetezi Algeria wamepangwa kundi moja na bingwa wa zamani, Ivory Coast.

Katika sherehe za upangaji wa makundi hayo iliyofanyika jijini Yaounde, Cameroon timu hizo ziko kundi moja la E pamoja na mataifa ya Guinea ya Ikweta na Sierra Leone.

Magwiji wa soka la Afrika kama Didier Drogba, El Hadji Diouf na Samuel Eto'o, waikuwepo kushuhudia upangaji huo wa droo ulioongoza na Rais wa CAF,Patrice Motsepe.

Michuano hiyo inayozijumuisha timu 24 zilizopangwakatika makundi 6 itaanza Januari 9 mpaka Februari 6, 2022 nchini Cameroon.

Timu 6 zitakazoongoza makundi na 6 zitakazoshika nafasi ya pili zitaungana na zingine 4 zitakazokuwa na matokeo mazuri kwenye nafasi ya 3, kucheza hatua ya mtoano.

MAKUNDI YA AFCON 2021

Kundi A: Cameroon, Burkina Faso, Ethiopia, Cape Verde

Kundi B: Senegal, Zimbabwe, Guinea, Malawi

Kundi C: Morocco, Ghana, Comoros, Gabon

Kundi D: Nigeria, Egypt, Sudan, Guinea-Bissau

Kundi E: Algeria, Sierra Leone, Equatorial Guinea, Ivory Coast

Kundi F: Tunisia, Mali, Mauritania, Gambia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom