Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,896
Mnamo tarehe 30/5/2018 Viongozi wa Vyama 2 vya upinzani nchini ndg. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto na Bwana Freeman Aikael Mbowe walitamka dhamira ya kushirikiana kwa kuanzia kuweka mgombea mmoja wa ubunge Jimbo la Buyungu Mkoa wa Kigoma na hatimaye nchi nzima. Makubaliano haya ambayo yanarejewa kama MAKUBALIANO YA KAKONKO) hatimaye yatafikishwa kwenye vikao vya Vyama vya ACT Wazalendo na CHADEMA ili kupata baraka za wanachama.
Kuna watu kadhaa wamekuwa wakihoji kwa uzuri au Kwa ubaya makubaliano haya. Ndugu Ado Shaibu ameweka Maelezo ya Viongozi hao ‘ verbatim ‘ ili wanachama na Wananchi Kwa ujumla wajue kiini chake Nini haswa.
Chama cha ACT Wazalendo Katika Kikao chake cha January Mwaka 2018 kiliazimia Katika mwelekeo wa Chama Mwaka 2018 kuwa ni Muhimu kujenga mashirikiano na Vyama vingine na makundi mengine ya kijamii. Mwelekeo huo umewekwa hapa pia. Tunataka kujenga a DEMOCRATIC FRONT kwa kuhusisha wana Demokrasia nchini kwa madhumuni ya 1) kutetea, kuimarisha na kulinda Demokrasia yetu ya Vyama vingi 2) kujenga Uchumi shirikishi wa Wananchi ( inclusive economy).
MAKUBALIANO YA KAKONKO ( YAMINI YA FREEMAN MBOWE NA ZITTO KABWE JIMBONI BUYUNGU ).
Na Ado Shaibu
Msiba wa Mwalimu Bilago, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, Naibu Waziri Kivuli Wa Wizara ya Elimu, Mwenyekiti wa Kanda ya Magharibi na Mjumbe Wa Kamati Kuu ya CHADEMA ulikuwa wa aina yake. Kubwa ni mnyukano wa dhahiri baina ya Spika na Mwenyekiti wa CHADEMA kuhusu tarehe ya mazishi ya marehemu. Spika akisisitiza marehemu azikwe Jumatano, CHADEMA walisisitiza na kusimamia Marehemu azikwe Alhamis ili kuwapa nafasi wananchi wa Buyungu Kumuaga mwakilishi wao. Baada ya mvutano wa muda mrefu, mwishowe Spika alisalimu amri na kuwaacha CHADEMA waendelee na utaratibu waliojipangia na familia. Akitoa hotuba yake wakati Wa kumuaga marehemu, Mbowe alimwita Zitto jukwaani na walichokifanya kinaelekea kubadili mwelekeo wa mambo Katika siasa za Tanzania. Lakini, hadi sasa, watu wengi bado wana maswali;
Nini hasa kilitokea?
Nini kilisemwa kwa mapana yake?
Yaliyosemwa yana matokeo gani Katika mwenendo Wa siasa za nchi yetu?
Nini kinafuata?
Baadhi ya maswali haya yanatokana na ukweli kwamba kutokana na kutokuwepo na vyombo vya habari vya kitaifa vilivyoripoti tukio zima msibani Kakonko, baadhi ya watu wameshindwa kupata picha kamili ya kilichotokea. Ili kuziba sehemu ya pengo hilo nimelazimika kuandika (transcribe) yaliyosemwa ili kuwawezesha wachambuzi, wadadisi na wapenzi wa demokrasia nchini kuelewa kilichotokea ili kushiriki vyema Kwenye mjadala huu. Kwa wapenzi wa video wanaweza kuirejea hotuba yote kwenye ukurasa wa CHADEMA Wa Kanda ya Magharibi ()
.......
Freeman Mbowe, Mwenyekiti, CHADEMA
"Mikoa iliyotangulia kwenye mageuzi ilikuwa mikoa ya Kilimanjaro, Kigoma na Mara. Hii ndiyo iliyokuwa mikoa kinara ya mageuzi nchini"
"Mkoa Wa Kigoma umezalisha wanasiasa wengi. Kama kuna Mkoa.. ninarudia na Zitto ananisikia..Kama kuna mkoa majimbo yake yote yalistahili kuwa ya upinzani ni Mkoa Wa Kigoma"
"Lakini, tofauti za kimitizamo, tofauti ambazo tunaweza kusema zimekithiri labda, zimeugharimu mkoa Wa kigoma, zimeigharimu Tanzania"
"Tukaacha kupambana na Chama cha Mapinduzi tukaanza kupambana wenyewe kwa wenyewe. Hili ni kosa lililougharimu Mkoa wa Kigoma na kuigharimu nchi yetu"
"Lakini misiba ni fursa ya upatanisho, ni fursa ya watu kutafakari; Tofauti zetu zinaweza kuwa kubwa kuliko za adui yetu?"
"Leo Zitto na ACT, tumelia nao Dar es salaam, tumelia nao Dodoma, tumelia nao Kakonko na tutalia nao kijijini kesho"
"Zitto na ACT hawawezi kuwa wagomvi na wabaya Wa CHADEMA kuliko Chama cha Mapinduzi"
"Kwa misingi hiyo, ninachotaka Kukieleza kwa viongozi wangu Wa Chama na ninataka Mheshimiwa Zitto usimame na kutuhakikishia...Njoo hapa. Unajua huyu ni Mwanangu nimemlea mwenyewe na ninamjua" (Anamwita Ndugu Zitto jukwaani. Zitto anasimama na kupanda jukwaani)
"Huyu ni kijana wangu, ninamjua sana"
"Ninachokisema ni hiki; kwa mambo waliyotufanyia CCM leo Kakonko; kwa mambo waliyoifanyia familia ya Bilago na waombelezaji wote hawa na Watanzania kwa ujumla, hatuna sababu ya kutofautiana katika harakati zetu"
"Tunastahili kulia pamoja, kucheka pamoja na kuumia pamoja"
"Hili jimbo litarudia uchaguzi. ACT, CHADEMA na Chama kingine chochote cha upinzani kinachotaka kushirikiana, tutashirikiana kuhakikisha tunaweka mgombea mmoja. Kama Zitto anakataa, akatae hapa mbele ya watu"
"Sisemi mgombea lazima atoke CHADEMA. Hapana. Ninachosema tunaweka mgombea mmoja katika umoja wetu. Na muungano huu utakwenda nchi nzima"
"Toa kauli Kamanda.." (Kisha anamkabidhi Kipaza sauti Zitto)
.......
Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo.
"Mwenyekiti wa Mkoa Wa Kigoma na Katibu wako njooni hapa" (Ndugu Sendwe Mbaruku, Mwenyekiti wa Mkoa na Juma Ramadhani, Kaimu Katibu Wa Mkoa Wa Kigoma wanapanda jukwaani)
"Maelekezo yangu (Anawageukia Katibu na Mwenyekiti wa Mkoa wa Kigoma) hapa Buyungu, kwa heshima ya Mwalimu Bilago, liwalo na liwe, tutaweka Mgombea mmoja"
"Hata ikitokea wengine wakakengeuka, sisi na CHADEMA tunalishana yamini tutaweka mgombea mmoja ilimradi awe ni mgombea anayekubalika na anayeweza kushinda ili tulinde heshima ya Mwalimu Bilago na heshima ya Mkoa Wa Kigoma"
"Haijalishi atoke Chama gani na sitaki hadithi za konakona. Tunachoangalia ni mgombea mwenye ubora. Wote tutafanya kampeni pamoja"
"Mwenyekiti toa ahadi yako hapa" (Anampa kipaza sauti Mwenyekiti wa Mkoa Wa Kigoma wa ACT Wazalendo)
......
Sendwe Mbaruku, Mwenyekiti wa Mkoa Wa Kigoma, ACT Wazalendo
"Habari ya jioni wananchi Wa Buyungu. Kauli ya Kiongozi wetu wa Chama tumeichukua na tutaifanyia kazi. Asanteni sana"
.....
Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama ACT Wazalendo.
"Mwenyekiti (Mbowe) mimi nimemaliza kwa upande wangu".
........
Freeman Mbowe, Mwenyekiti, CHADEMA
"Ngoja kwanza niwaulize (Anawageukia Mwenyekiti na Katibu Wa Mkoa Wa Kigoma Wa ACT). Wewe (Mwenyekiti wa Mkoa) ulikuwa CHADEMA? (Mwenyekiti anakubali). Wewe ulikuwa CHADEMA? (Katibu Wa Mkoa anajibu alikuwa CUF kabla ya kujiunga na ACT). Tumemaliza. Asante sana Mheshimiwa Zitto na tutaweka mgombea mmoja"
"Tusiishie Buyungu. Tusiishie hapo. Hatuwezi kuendelea kujenga siasa za mifarakano katika nchi hii. Lazima tutafute namna ya kumaliza tofauti zetu na tuendelee kuwa wamoja"
........
Transcription hii imefanywa na Ado Shaibu, Katibu Wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi, ACT Wazalendo
Simu: 0653619906
—————————
Mwelekeo wa Chama cha ACT Wazalendo Katika mwaka 2018
1. Kupigania Haki za Wafanyakazi kupitia Vyama vya Wafanyakazi na haki za raia kupitia vyama vya Wakulima, Wavuvi, Wafugaji na Wafanyabiashara wadogo kwa kujenga ushirikiano wa kipambano na Jumuiya hizo za Wananchi.
2. Kuongoza juhudi za Ushirikiano na Vyama vingine vya upinzani kwa shabaha ya kuimarisha Demokrasia ya vyama vingi nchini kwa kufanya vikao vya Mara kwa Mara na Viongozi wa Vyama vingine na kufanya shughuli za pamoja.
3. Kuendelea kusemea Haki za Kijamii kama Elimu na Afya na kuongeza juhudi za kupigania Haki ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi wote hasa Wakulima kwa kushawishi kuanzisha Fao la Bei katika mfumo wa Hifadhi ya Jamii nchini na Bima ya Afya kwa kila Mtanzania.
4. Kuendelea kushawishi Sera za Uchumi zinazomkomboa mwananchi wa kawaida kwa kukosoa Sera zinazodidimiza Maendeleo ya Uchumi na kupendekeza Sera mbadala.
5. Kujikita Katika Uimarishaji wa Chama kwenye ngazi zote na kufanya Mkutano Mkuu wa Chama Mwezi Agosti Jijini Mbeya sambamba na Mkutano Mkuu wa Kidemokrasia 2018.
Imetolewa na
Kamati Kuu ya Chama Cha ACT Wazalendo
Januari, 2018
———————————
Kuna watu kadhaa wamekuwa wakihoji kwa uzuri au Kwa ubaya makubaliano haya. Ndugu Ado Shaibu ameweka Maelezo ya Viongozi hao ‘ verbatim ‘ ili wanachama na Wananchi Kwa ujumla wajue kiini chake Nini haswa.
Chama cha ACT Wazalendo Katika Kikao chake cha January Mwaka 2018 kiliazimia Katika mwelekeo wa Chama Mwaka 2018 kuwa ni Muhimu kujenga mashirikiano na Vyama vingine na makundi mengine ya kijamii. Mwelekeo huo umewekwa hapa pia. Tunataka kujenga a DEMOCRATIC FRONT kwa kuhusisha wana Demokrasia nchini kwa madhumuni ya 1) kutetea, kuimarisha na kulinda Demokrasia yetu ya Vyama vingi 2) kujenga Uchumi shirikishi wa Wananchi ( inclusive economy).
MAKUBALIANO YA KAKONKO ( YAMINI YA FREEMAN MBOWE NA ZITTO KABWE JIMBONI BUYUNGU ).
Na Ado Shaibu
Msiba wa Mwalimu Bilago, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, Naibu Waziri Kivuli Wa Wizara ya Elimu, Mwenyekiti wa Kanda ya Magharibi na Mjumbe Wa Kamati Kuu ya CHADEMA ulikuwa wa aina yake. Kubwa ni mnyukano wa dhahiri baina ya Spika na Mwenyekiti wa CHADEMA kuhusu tarehe ya mazishi ya marehemu. Spika akisisitiza marehemu azikwe Jumatano, CHADEMA walisisitiza na kusimamia Marehemu azikwe Alhamis ili kuwapa nafasi wananchi wa Buyungu Kumuaga mwakilishi wao. Baada ya mvutano wa muda mrefu, mwishowe Spika alisalimu amri na kuwaacha CHADEMA waendelee na utaratibu waliojipangia na familia. Akitoa hotuba yake wakati Wa kumuaga marehemu, Mbowe alimwita Zitto jukwaani na walichokifanya kinaelekea kubadili mwelekeo wa mambo Katika siasa za Tanzania. Lakini, hadi sasa, watu wengi bado wana maswali;
Nini hasa kilitokea?
Nini kilisemwa kwa mapana yake?
Yaliyosemwa yana matokeo gani Katika mwenendo Wa siasa za nchi yetu?
Nini kinafuata?
Baadhi ya maswali haya yanatokana na ukweli kwamba kutokana na kutokuwepo na vyombo vya habari vya kitaifa vilivyoripoti tukio zima msibani Kakonko, baadhi ya watu wameshindwa kupata picha kamili ya kilichotokea. Ili kuziba sehemu ya pengo hilo nimelazimika kuandika (transcribe) yaliyosemwa ili kuwawezesha wachambuzi, wadadisi na wapenzi wa demokrasia nchini kuelewa kilichotokea ili kushiriki vyema Kwenye mjadala huu. Kwa wapenzi wa video wanaweza kuirejea hotuba yote kwenye ukurasa wa CHADEMA Wa Kanda ya Magharibi ()
.......
Freeman Mbowe, Mwenyekiti, CHADEMA
"Mikoa iliyotangulia kwenye mageuzi ilikuwa mikoa ya Kilimanjaro, Kigoma na Mara. Hii ndiyo iliyokuwa mikoa kinara ya mageuzi nchini"
"Mkoa Wa Kigoma umezalisha wanasiasa wengi. Kama kuna Mkoa.. ninarudia na Zitto ananisikia..Kama kuna mkoa majimbo yake yote yalistahili kuwa ya upinzani ni Mkoa Wa Kigoma"
"Lakini, tofauti za kimitizamo, tofauti ambazo tunaweza kusema zimekithiri labda, zimeugharimu mkoa Wa kigoma, zimeigharimu Tanzania"
"Tukaacha kupambana na Chama cha Mapinduzi tukaanza kupambana wenyewe kwa wenyewe. Hili ni kosa lililougharimu Mkoa wa Kigoma na kuigharimu nchi yetu"
"Lakini misiba ni fursa ya upatanisho, ni fursa ya watu kutafakari; Tofauti zetu zinaweza kuwa kubwa kuliko za adui yetu?"
"Leo Zitto na ACT, tumelia nao Dar es salaam, tumelia nao Dodoma, tumelia nao Kakonko na tutalia nao kijijini kesho"
"Zitto na ACT hawawezi kuwa wagomvi na wabaya Wa CHADEMA kuliko Chama cha Mapinduzi"
"Kwa misingi hiyo, ninachotaka Kukieleza kwa viongozi wangu Wa Chama na ninataka Mheshimiwa Zitto usimame na kutuhakikishia...Njoo hapa. Unajua huyu ni Mwanangu nimemlea mwenyewe na ninamjua" (Anamwita Ndugu Zitto jukwaani. Zitto anasimama na kupanda jukwaani)
"Huyu ni kijana wangu, ninamjua sana"
"Ninachokisema ni hiki; kwa mambo waliyotufanyia CCM leo Kakonko; kwa mambo waliyoifanyia familia ya Bilago na waombelezaji wote hawa na Watanzania kwa ujumla, hatuna sababu ya kutofautiana katika harakati zetu"
"Tunastahili kulia pamoja, kucheka pamoja na kuumia pamoja"
"Hili jimbo litarudia uchaguzi. ACT, CHADEMA na Chama kingine chochote cha upinzani kinachotaka kushirikiana, tutashirikiana kuhakikisha tunaweka mgombea mmoja. Kama Zitto anakataa, akatae hapa mbele ya watu"
"Sisemi mgombea lazima atoke CHADEMA. Hapana. Ninachosema tunaweka mgombea mmoja katika umoja wetu. Na muungano huu utakwenda nchi nzima"
"Toa kauli Kamanda.." (Kisha anamkabidhi Kipaza sauti Zitto)
.......
Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo.
"Mwenyekiti wa Mkoa Wa Kigoma na Katibu wako njooni hapa" (Ndugu Sendwe Mbaruku, Mwenyekiti wa Mkoa na Juma Ramadhani, Kaimu Katibu Wa Mkoa Wa Kigoma wanapanda jukwaani)
"Maelekezo yangu (Anawageukia Katibu na Mwenyekiti wa Mkoa wa Kigoma) hapa Buyungu, kwa heshima ya Mwalimu Bilago, liwalo na liwe, tutaweka Mgombea mmoja"
"Hata ikitokea wengine wakakengeuka, sisi na CHADEMA tunalishana yamini tutaweka mgombea mmoja ilimradi awe ni mgombea anayekubalika na anayeweza kushinda ili tulinde heshima ya Mwalimu Bilago na heshima ya Mkoa Wa Kigoma"
"Haijalishi atoke Chama gani na sitaki hadithi za konakona. Tunachoangalia ni mgombea mwenye ubora. Wote tutafanya kampeni pamoja"
"Mwenyekiti toa ahadi yako hapa" (Anampa kipaza sauti Mwenyekiti wa Mkoa Wa Kigoma wa ACT Wazalendo)
......
Sendwe Mbaruku, Mwenyekiti wa Mkoa Wa Kigoma, ACT Wazalendo
"Habari ya jioni wananchi Wa Buyungu. Kauli ya Kiongozi wetu wa Chama tumeichukua na tutaifanyia kazi. Asanteni sana"
.....
Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama ACT Wazalendo.
"Mwenyekiti (Mbowe) mimi nimemaliza kwa upande wangu".
........
Freeman Mbowe, Mwenyekiti, CHADEMA
"Ngoja kwanza niwaulize (Anawageukia Mwenyekiti na Katibu Wa Mkoa Wa Kigoma Wa ACT). Wewe (Mwenyekiti wa Mkoa) ulikuwa CHADEMA? (Mwenyekiti anakubali). Wewe ulikuwa CHADEMA? (Katibu Wa Mkoa anajibu alikuwa CUF kabla ya kujiunga na ACT). Tumemaliza. Asante sana Mheshimiwa Zitto na tutaweka mgombea mmoja"
"Tusiishie Buyungu. Tusiishie hapo. Hatuwezi kuendelea kujenga siasa za mifarakano katika nchi hii. Lazima tutafute namna ya kumaliza tofauti zetu na tuendelee kuwa wamoja"
........
Transcription hii imefanywa na Ado Shaibu, Katibu Wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi, ACT Wazalendo
Simu: 0653619906
—————————
Mwelekeo wa Chama cha ACT Wazalendo Katika mwaka 2018
1. Kupigania Haki za Wafanyakazi kupitia Vyama vya Wafanyakazi na haki za raia kupitia vyama vya Wakulima, Wavuvi, Wafugaji na Wafanyabiashara wadogo kwa kujenga ushirikiano wa kipambano na Jumuiya hizo za Wananchi.
2. Kuongoza juhudi za Ushirikiano na Vyama vingine vya upinzani kwa shabaha ya kuimarisha Demokrasia ya vyama vingi nchini kwa kufanya vikao vya Mara kwa Mara na Viongozi wa Vyama vingine na kufanya shughuli za pamoja.
3. Kuendelea kusemea Haki za Kijamii kama Elimu na Afya na kuongeza juhudi za kupigania Haki ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi wote hasa Wakulima kwa kushawishi kuanzisha Fao la Bei katika mfumo wa Hifadhi ya Jamii nchini na Bima ya Afya kwa kila Mtanzania.
4. Kuendelea kushawishi Sera za Uchumi zinazomkomboa mwananchi wa kawaida kwa kukosoa Sera zinazodidimiza Maendeleo ya Uchumi na kupendekeza Sera mbadala.
5. Kujikita Katika Uimarishaji wa Chama kwenye ngazi zote na kufanya Mkutano Mkuu wa Chama Mwezi Agosti Jijini Mbeya sambamba na Mkutano Mkuu wa Kidemokrasia 2018.
Imetolewa na
Kamati Kuu ya Chama Cha ACT Wazalendo
Januari, 2018
———————————