Makosa ya Hayati Magufuli hayasahihishiki

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,260
33,860
Kuna fikra za baadhi ya watu wanaotamani itokee siku moja "makosa" ya kimtazamo na kiutendaji ya Hayati John Magufuli, aliyekuwa Rais wa Tano wa serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania YAREKEBISHWE.

Kiuhalisia makosa hayo hayawezi kurekebishwa kwa kuwa umbali aliotufikisha Magufuli inakuwa ngumu sana kurudi kwenye njia sahihi kiurahisi. Kitu pekee kinachoweza kufanyika ni kusuluhisha mitazamo yetu na uhalisia wa mambo.

Kwa mfano; chuki kati ya wafuasi wake na wale waliokuwa wanaipinga falsafa yake ya undeshaji nchi inarekebishwaje? Jee watu waliodhurika wakati wa utawala wake wanaponaje ama wale waliopotea wanapatikanaje? Leo hii hawa kina Ben Saanane, Simon Kanguye, Azor Gwanda nani anajua walipo na inawezekana wakarudishwa kwa familia zao. Lissu na wengine waliopata ulemavu zama hizo maisha yao yanaweza kurejerezwa?

Nani mwenye akili timamu anayeweza kusimamisha ujenzi wa bwawa la umeme la Nyerere kwa hatua ililofikia. Au SGR inawezaje kuwachwa wakati tayari mabilioni ya shilingi yameteketea kwenye mradi huo tayari. Nani ataruhusu mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa wakati CCM amri ya marufuku hiyo haiwahusu?​
 
Aisee!!

Kweli CCM itaendelea kutawala...

Ha! Ha! Ha! Ha!
Wewe ni zuzu!

Hao uliowataja ni kina nani mbona juzi tu hapa watu 7 wa familia moja wameuawa kwa mapanga wao siyo watu? Wameuawa kipindi cha magu?

Ulimboka nae alikuwa magu yule?
Mwangosi nae alikuwa magu?
Dr. Mvungi alikuwa magu?
Hivi umejaza mavi huko kichwani kiasi kwamba hukumbuki kama enzi za jk kuna bomu lilirushwa kwenye mkutano wa chadema pale soweto arusha likaua watu 5? Alikuwa magu yule?

Na hawa nao vipi umeshaambiwa wako wapi mpaka muda huu?
Screenshot_20220726-080825_Facebook.jpg
 
Inaonekana you come from a long line of psychopaths, ndiyo maana labda wewe unaoana ni sawa Wamasai kufukuzwa kwenye ardhi yao kupisha Mwarabu awinde, Magufuli asingeruhusu hili, low IQ unaona Bwawa la kuzalisha Umeme > 2000 MW na Reli madhubuti na ya kisasa inayoweza kufupisha safari kwa kwa zaidi ya masaa 10 ni kupoteza fedha?
 
Inaonekana you come from a long line of psychopaths kwenye familia na ukoo wako, ndiyo maana kwako wewe unaoana ni sawa Wamasahi kufukuzwa kwenye ardhi yao kupisha Mwarabu awinde, Magufuli asingeruhusu hili, low IQ unaona Bwawa la kuzalisha Umeme > 2000 MW na Reli madhubuti na ya kisasa inayoweza kufupisha safari kwa kwa zaidi ya masaa 10 ni kupoteza fedha?
Hiyo safari inafupishwa ni ya nini au ya nani? Hilo bwawa la umeme limegharimu shilingi ngapi na litaanza lini kuzalisha umeme na likianza litashusha bei ya umeme ama litapandisha?
 
Hiyo safari inafupishwa ni ya nini au ya nani? Hilo bwawa la umeme limegharimu shilingi ngapi na litaanza lini kuzalisha umeme na likianza litashusha bei ya umeme ama litapandisha?

Ungeuliza hayo maswali kwanza ueleweshwe kabla ya kuanza kukejeli mambo usioyaelewa.

Kama hata hauelewi kwamba sgr inafupisha safari na umuhimu wa kufupisha safari kwenye uchumi wa nchi au hauelewi hata hydroelectricity is the cheapest form of electricity Duniani na what it means kuwa na cheap electricity/ kWh kwenye uchumi wa nchi bado una safari ndefu sana na no wonder umeshindwa kumuelewa Magufuli!
 
Kabisa. kwa mfano wa umeme wa maji kule rufiji. Jee tulishamaliza kufanya uwekezaji kwenye mradi wa Gesi ili izalishe umeme?

SGR ipo kwa kuwa iliyopo ilielemewa ama ni kwa kuwa kuna watu wanaona "usasa" na fahari kuwa na SGR?
umeme wa gas ni ghali ukilinganisha na huu wa maji, hii ndio sababu iliyofanya Magufuri a opt kwenye rufiji dam, lakini vilevile mikataba ya gas aliyoifanya kikwete unaijua?

kuhusu SGR, ni option nzuri sana kwasababu itaongeza idadi ya mizigo mara dufu kuliko hii inayopita kwenye MGR.
 
Inaonekana you come from a long line of psychopaths kwenye familia na ukoo wako, ndiyo maana kwako wewe unaoana ni sawa Wamasahi kufukuzwa kwenye ardhi yao kupisha Mwarabu awinde, Magufuli asingeruhusu hili, low IQ unaona Bwawa la kuzalisha Umeme > 2000 MW na Reli madhubuti na ya kisasa inayoweza kufupisha safari kwa kwa zaidi ya masaa 10 ni kupoteza fedha?
Ni lini Ngorongoro imetangazwa kuwa Game reserve? Unaelewa tofauti ya National park na Game reserve?
 
Back
Top Bottom