Ng'wamapalala
JF-Expert Member
- Jun 9, 2011
- 6,811
- 6,506
Kwani huyu Edward Lowassa siyo yule Edward Lowassa wa mwaka 2010 ambaye Mwenyekiti wa CCM-Taifa, Rais Kikwete aliushika mkono wake na kuunyanyua juu kuwaomba wapiga kura wa Jimbo la Monduli ili wamchague kuwa Mbunge wao huku akisema, hakuna mwakilishi mzuri nchini kushinda Edward Ngoyai Lowassa.
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Jakaya Kikwete, akimnadi mgombea ubunge jimbo la Monduli mkoani Arusha, Edward Lowasa, kwa wapiga kura wa jimbo hilo wakati wa mkutano wa kampeni 2010.
Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa akiwa na Edward Lowassa wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Arusha.
Kwani siyo huyu Edward Lowassa ambaye Mwenyekiti wa CCM-Taifa, Rais Kikwete aliwahi kusema kilichompata Edward Lowassa katika sakata la Richmond Development Company LLC ni ajali ya kisiasa, kwa maana nyingine, alijikwaa kisiasa na anaweza kusimama na kuendelea na safari yake ya kisiasa.
Hivi hawa baadhi ya viongozi wa CCM wanataka kutueleza Edward Lowassa wa leo ni tofauti na yule wa 2012 ambaye jina lake lilikidhi vigezo vyote na kupitiswa na vikao vikuu vya CCM kuwa mgombea Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM-Taifa ili kupambana na Dr. Salash Mokosyo Toure na Nanai Taon Konina ambapo aliwashinda kwa kura nyingi.
Kwani siyo huyu Edward Lowassa ambaye Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, amemmwagia sifa wakati wa ziara yake mkoani Arusha na kusema ni miongoni mwa viongozi waliotekeleza kikamilifu ilani ya chama hicho.
Ni Edward Lowassa yupi ambaye baadhi ya viongozi wa CCM wanataka kutuaminisha kwa sasa kama jina lake linaweza kukatwa na Kamati Kuu kutokana na mapungufu kwenye vigezo 13 vya kuwachuja watia NIA wa nafasi ya Urais Tanzania kama ilivyotangazwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula.
Kiongozi yupi wa CCM mwenye uwezo wa kumvika paka kengele?
Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Jakaya Kikwete, akimnadi mgombea ubunge jimbo la Monduli mkoani Arusha, Edward Lowasa, kwa wapiga kura wa jimbo hilo wakati wa mkutano wa kampeni 2010.
Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa akiwa na Edward Lowassa wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Arusha.
Kwani siyo huyu Edward Lowassa ambaye Mwenyekiti wa CCM-Taifa, Rais Kikwete aliwahi kusema kilichompata Edward Lowassa katika sakata la Richmond Development Company LLC ni ajali ya kisiasa, kwa maana nyingine, alijikwaa kisiasa na anaweza kusimama na kuendelea na safari yake ya kisiasa.
Hivi hawa baadhi ya viongozi wa CCM wanataka kutueleza Edward Lowassa wa leo ni tofauti na yule wa 2012 ambaye jina lake lilikidhi vigezo vyote na kupitiswa na vikao vikuu vya CCM kuwa mgombea Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM-Taifa ili kupambana na Dr. Salash Mokosyo Toure na Nanai Taon Konina ambapo aliwashinda kwa kura nyingi.
Kwani siyo huyu Edward Lowassa ambaye Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, amemmwagia sifa wakati wa ziara yake mkoani Arusha na kusema ni miongoni mwa viongozi waliotekeleza kikamilifu ilani ya chama hicho.
Ni Edward Lowassa yupi ambaye baadhi ya viongozi wa CCM wanataka kutuaminisha kwa sasa kama jina lake linaweza kukatwa na Kamati Kuu kutokana na mapungufu kwenye vigezo 13 vya kuwachuja watia NIA wa nafasi ya Urais Tanzania kama ilivyotangazwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula.
Kiongozi yupi wa CCM mwenye uwezo wa kumvika paka kengele?