Makongoro Nyerere: Lowassa nisamehe sana, ila ni Lazima tukuvue gamba haraka!

Hey Jf kumekucha,

Hali si shwari kati ya kapteni Makongoro Nyerere na Edward Lowassa. Taarifa za kina zinaeleza vuta nikuvute hiyo imezidi kupamba moto huku safari hii Makongoro akiamua kuvunja ukimya na kuweka bayana maamuzi yaliyofikiwa na NEC ya kumvua gamba Lowassa ni lazima yafanyike mara moja pasipo kusita.

Taarifa zaidi ambazo tumezinasa kwa njia ya simu kutoka huko Dar es salaam maeneo ya Kinondoni Biafra kutoka kwa mwandishi mmoja wa gazeti la Dira ya Mtanzania zinabainisha kuwa ni Makongoro Nyerere ndiye aliyeanika taarifa za Lowassa kutaka kuyaanika maovu ya Kikwete wiki moja iliyopita na huku wiki hii Makongoro huyohuyo akiibuka na madai mengine mazito kuhusu azma ya Kikwete kuwakingia kifua Lowassa na Chenge ili wasitemwe kwenye kikao kijacho, Makongoro amekaririwa akisema "hata kama kiwete akitaka amlinde huyu lowassa, kweli kaka yangu lowassa atatusamehe ni lazima tumng'oe bila kusita, itabidi tupinge hoja za kikwete kwa maana hana ubavu wa kutulazimisha"

Kwakuwa Umeshakula Ban Sichangii Ng'o.
 
Hey Jf kumekucha,

Hali si shwari kati ya kapteni Makongoro Nyerere na Edward Lowassa. Taarifa za kina zinaeleza vuta nikuvute hiyo imezidi kupamba moto huku safari hii Makongoro akiamua kuvunja ukimya na kuweka bayana maamuzi yaliyofikiwa na NEC ya kumvua gamba Lowassa ni lazima yafanyike mara moja pasipo kusita.

Taarifa zaidi ambazo tumezinasa kwa njia ya simu kutoka huko Dar es salaam maeneo ya Kinondoni Biafra kutoka kwa mwandishi mmoja wa gazeti la Dira ya Mtanzania zinabainisha kuwa ni Makongoro Nyerere ndiye aliyeanika taarifa za Lowassa kutaka kuyaanika maovu ya Kikwete wiki moja iliyopita na huku wiki hii Makongoro huyohuyo akiibuka na madai mengine mazito kuhusu azma ya Kikwete kuwakingia kifua Lowassa na Chenge ili wasitemwe kwenye kikao kijacho, Makongoro amekaririwa akisema "hata kama kiwete akitaka amlinde huyu lowassa, kweli kaka yangu lowassa atatusamehe ni lazima tumng'oe bila kusita, itabidi tupinge hoja za kikwete kwa maana hana ubavu wa kutulazimisha"

MAKONGORO NYERERE NA UJASIRI HUU WA NADRA CCM!
Johnson Mbwambo: Toleo la 182 20 Apr 2011
KINACHOJADILIWA kwa sasa, sehemu mbalimbali nchini, si tena kinachoitwa ‘tiba ya ajabu ya Babu wa Loliondo'; bali ni kilichotokea, hivi karibuni, huko Dodoma kinachoitwa ‘kujivua gamba kwa CCM'.
Mitaani, sokoni, kwenye mabaa, vijiweni na hata maofisini kinachozungumzwa sasa na kinachojadiliwa, ni kuhusu yaliyojiri huko Dodoma ambako CCM ‘kilijivua gamba' kwa kuwatosa viongozi wake maarufu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Kote huko maswali kibao yanaibuliwa; Je, ni kweli CCM imefanikiwa kujivua gamba? Je, ni kweli Rais Kikwete kawatosa moja kwa moja maswahiba wake – Rostam Aziz, Edward Lowassa na Andrew Chenge au ni ‘usanii' wake mwingine? Je, uamuzi wa Dodoma wa kuwataka watuhumiwa hao wajiuzulu nafasi zao za uongozi katika Chama utafuatiwa na hatua za kisheria za vyombo vya kisheria dhidi yao?
Je, CCM sasa kinaweza kujigamba kwamba ni shwari; ilhali aliyeyalea magamba hayo (Kikwete) bado anaendelea kushikilia hatamu za uongozi?
Je, kina Lowassa, Rostam na Chenge wakishajiuzulu nyadhifa zao CCM, kama walivyotakiwa na NEC, watabaki ndani ya chama hicho kama wanachama wa kawaida au wataanzisha chao au watajiunga na vyama vilivyopo vya upinzani?
Haya ni baadhi tu ya maswali mengi yanayoulizwa hivi sasa na wananchi kote nchini wanapojadili matokeo ya kikao hicho cha Dodoma. Ni dhahiri ni maswali yasiyo na majibu ya moja kwa moja ya uhakika, na ni dhahiri ni maswali ambayo ni muda tu ndio utatoa majibu yake. Waingereza wanasema; time will tell.
Vyovyote vile; naandika kumpongeza Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mara, Makongoro Nyerere, kwa mchangao wake ndani ya vikao hivyo vya CCM ambao ulikuwa ni wa kijasiri, kiungwana, kifalsafa na usio wa kinafiki. Ni mchango ulioweka mbele maslahi ya Taifa kuliko ya kwake binafsi.
Habari za uhakika nilizozipata kutoka kwa waliohudhuria mkutano huo, zinasema kwamba ni yeye pekee aliyekuwa na ujasiri wa kuuanika mbele ya wajumbe udhaifu wa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika kuwashughulikia mafisadi ndani ya Chama na ndani ya Serikali.
Ni udhaifu huo wa Kikwete wa kuchelewa kuchukua hatua dhidi yao ambao umekifanya chama hicho kipoteze kwa kasi umaarufu wake kwa CHADEMA. Kwa maneno mengine, kama angelichukua hatua mapema wakati wa awamu yake ya kwanza ya uongozi, pengine mambo ndani ya CCM yasingekuwa shaghalabagala kama yalivyo sasa.
Sitakwenda ndani zaidi kulijadili suala hilo; kwa sababu wachambuzi wengine wamelijadili kwa umahiri mkubwa ndani ya gazeti hili. Isitoshe, kama nilivyoeleza mwanzoni, hoja yangu ya leo ni kupongeza tu ujasiri wa Makongoro Nyerere. Laiti kungekuwa na viongozi wengi jasiri kama yeye ndani ya CCM na ndani ya Serikali…..!
Mtoa habari wetu anasema kwamba wakati wa mkutano huo wa Dodoma, Makongoro alisimama ukumbini na akamtazama, kwa macho makavu, Mwenyekiti Jakaya Kikwete, na kisha maneno yafuatayo yakamtoka kinywani mwake:
"Lowassa ni ndugu yangu. Sina matatizo naye. Najua ananipenda, nami nampenda. Lakini kule ‘site' wanasema hapana. Atoke. Tena nawe Mwenyekiti ulipokwenda Monduli, ukainua mkono wake juu, ukasema hujapata kuona kama yeye (Lowassa), kule ‘site' wakauliza; sasa hii ndiyo nini?"
Rostam simfahamu vizuri. Ninakotembelea yeye hawezi kuja, na mimi anakotembelea siwezi kwenda. Sina ugomvi naye. Lakini kule ‘site' wanasema naye hapana. Ulipokwenda Igunga ukamuamsha mkono ukasema yeye ni kama timu ya mpira iliyokamilika. Watu kwenye ‘site' wakauliza, sasa hii ndiyo nini?"
"Nasikia Chenge wanamwita Mzee wa Vijisenti. Ni ndugu yangu. Sina hakika kama anavyo vijisenti kiasi hicho. Lakini kwenye ‘site', si mimi, watu wanasema naye hapana. Ulikwenda pia Rombo, ukamuamsha mkono Mramba, kule kwenye ‘site' watu wakatuuliza; sasa hii ndiyo nini?"
Ndugu zangu, hiyo ni sehemu tu ya mchango mkubwa wa Makongoro Nyerere alioutoa ndani ya vikao hivyo vya CCM vya kujivua gamba, mjini Dodoma. Nina hakika, mpenzi msomaji, utakubaliana nami kwamba Makongoro alionyesha ujasiri mkubwa kwa kumkosoa kiungwana Rais Kikwete ndani ya kikao hicho.
Ni ujasiri ambao ni nadra kuuona siku hizi ndani ya vikao vya juu vya CCM au vya Serikali; kwa maana ya Baraza la Mawaziri. Ni ujasiri mkubwa hasa ukizingatia kwamba wakubwa wetu wengi, hivi sasa, hufurahia kusifiwa tu, na huona raha kuzungukwa na court jesters (waimba sifa na walamba miguu ya wakubwa) ambao hucheka rais anapocheka, hununa rais anaponuna na ambao huwafanya maadui binafsi wa rais kuwa maadui zao pia!
Hawa court jesters hawawezi, kamwe, kumtonya Rais; hata pale inapoonekana dhahiri kwamba anakosea. Ilimradi mambo yao yanakwenda vizuri, watakaa kimya kwa sababu hawataki kumuudhi mkubwa wasijeenguliwa madarakani.
Ndiyo maana anapotokea mtu wa sampuli ya Makongoro Nyerere na kumtazama Rais na Mwenyekiti wa Chama kwa macho makavu, na kisha, kiungwana kabisa na kwa upole kabisa, akamwambia kwamba; "nawe ulikosea", lazima tuupongeze ujasiri wa mtu huyo.
Ninasema hivyo; kwa sababu Rais Kikwete si Mungu au malaika asiyekosea. Rais au Mwenyekiti wa Chama naye pia ni binadamu kama sisi, na hufanya makosa kama sisi, na hivyo ni wajibu wetu kumfahamisha, kiungwana kabisa, pale anapokosea. Ni wajibu wetu kutamka "Mfalme yu uchi" inapotokea kweli "yu uchi".
Ni kwa mantiki hiyo Makongoro Nyerere alisimama na kumwambia ‘Mfalme': "Ulipokwenda Monduli ukainua mkono wake juu (Lowassa) ukasema hujapata kuona kiongozi kama yeye , kule ‘site' wakauliza sasa hii ndiyo nini?"…. ulipokwenda Igunga ukamuamsha (Rostam) mkono ukasema amekamilika kama timu ya mpira; watu kwenye ‘site' wakauliza sasa hii ndio nini?"
Kwa hakika, maneno hayo ya Makongoro yanachoma na kupenya nyoyo. Sina hakika Mwenyekiti Kikwete alijisikiaje wakati Makongoro akiyatamka maneno hayo; lakini nadhani alijutia kitendo kile alichokifanya Rombo, Monduli na Igunga; maana kilimuonyesha mbele ya Watanzania wote, ikiwa ni pamoja na kwenye mkutano huo, udhaifu wake kama kiongozi.
Kwa mara nyingine tena nimpongeze Makongoro Nyerere kwa kumkosoa Kikwete kipole, kiungwana na kifalsafa. Kwa Watanzania wengine wote ambao hatukuwemo kwenye ukumbi ule, Makongoro alitusemea, alitufikishia hisia zetu kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wetu.
Makongoro alitumia neno ‘site' (eneo ambako ndiko anakoshinda kusimamia shughuli zake za miradi ya ujenzi) kuwasilisha ujumbe wake, lakini ukweli ni kwamba ‘site' aliyoizungumzia inamaanisha kote nchini. ‘Site' ni sisi sote tulioshangazwa na hatua hiyo ya Kikwete ya kuwakampenia Lowassa, Mramba na Rostam; ilhali wanaandamwa na kashfa nzito za ufisadi.
Wenye kumbukumbu nzuri watakumbuka kwamba wakati wa kampeni za mwaka jana za Uchaguzi Mkuu nilipata kuandika, kwenye safu hii, kuhusu kitendo hicho cha Rais Kikwete cha kuwakampenia ubunge watuhumiwa hao wa ufisadi.
Niliandika wakati huo kwamba haingii akilini mwangu (kwa mfano) kwa Kikwete kuusifia utendaji kazi wa Mramba kwenye mkutano wa kampeni Rombo; ilhali Serikali yake anayoiongoza tayari ilishamfikisha mtu huyo mahakamani kujibu tuhuma za ufisadi, na kesi ilikuwa inanguruma!
Niliandika vilevile kushangazwa kwangu na Rais Kikwete kuwaomba wananchi wa Monduli na Igunga wawape kura za kishindo Lowassa na Rostam; ilhali watu hao wanahusishwa na kashfa ya ufisadi wa Richmond na Dowans, na hata mmojawao (Lowassa) kulazimika kujiuzulu uwaziri mkuu kwa tuhuma hizo.
Leo, nafarijika kwamba amejitokeza kijasiri Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa (Makongoro), na bila unafiki akamweleza Rais Kikwete (kwa kiungwana kabisa) udhaifu wake aliouonyesha kiuongozi katika suala hilo la mafisadi.
Ni hoja yangu kwamba kama Kikwete angekuwa na washauri makini, bila shaka, wangemweleza mara moja makosa aliyofanya ya kumsifu Mramba hadharani na kumuombea kura kwenye mkutano wa kampeni Rombo na athari zake za baadaye kwa Chama. Nina hakika, pamoja na u-hambiliki wake, angelifikiria mara mbili mbili kabla hajalirejea tena kosa hilo huko Monduli na baadaye Igunga.
Nina hakika vilevile kwamba ni kosa hilo la kuwapigia debe watuhumiwa wa ufisadi wakati wa kampeni, lililochangia kwenye kura chache alizopata kwenye uchaguzi huo ukilinganisha na za mwaka 2005.
Aidha, ni kwa sababu ya kosa hilo hilo watu sasa wanahoji juu ya uwezo wake wa uongozi, na wengi wanajiuliza; kama na yeye si gamba ambalo katika hali ya kawaida lilipaswa nalo kuvuliwa!
Na wananchi wana haki ya kuwa na hisia hizo; maana itakuaje Rais na Mwenyekiti wa CCM (Kikwete) awamwagie sifa kemkem watuhumiwa hao wa ufisadi kwamba ni waadilifu na wachapakazi hodari, na kisha miezi sita baadaye Rais huyo huyo tena aongoze kikao cha chama cha kuwavua uongozi wa CCM watu hao hao kwa tuhuma za ufisadi?!
Kwa nini linapokuja suala la ufisadi tusitilie shaka uwezo wake wa kupima mambo (sense of judgement)? Kiongozi wa nchi anawezaje kuwa na sura mbili katika jambo hilo hilo moja; tena ndani ya kipindi kifupi tu?
Je, tuamini kwamba msimamo wake huu wa sasa (yeye na NEC nzima ya CCM) dhidi ya watuhumiwa hao wa ufisadi, ni wa kudumu na kwamba hataubadili tena huko mbele ya safari?
Je, sasa tuamini kwamba kweli CCM imejivua gamba, na haitawakumbatia tena watuhumiwa wa ufisadi katika ngazi zote? Kama nilivyoeleza mwanzo, haya ni maswali ambayo yatajibiwa na muda tu!
Vyovyote vile; nafarijika kwamba ametokea jasiri (Makongoro) kumweleza hadharani Rais Kikwete udhaifu wake na makosa aliyoyafanya ya kuwakumbatia maswahiba wake hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi; hata kama ni miezi sita imeshapita tangu ayatende, na hata kama tayari yameshaiathiri CCM.
Kwa hakika, mafanikio ya CCM baada ya kujivua gamba, yatategemea mwelekeo wa Mwenyekiti wake, Jakaya Kikwete. Sichelei kusema kwamba kama naye hatabadilika (akajivua gamba lake binafsi), CCM itakuwa ile ile ya jana na leo hadi tunaingia uchaguzi mkuu mwingine wa mwaka 2015.
Nihitimishe safu yangu kwa kusema kwamba hata kama kauli zake hizo za Dodoma zitakuja kumponza Makongoro huko mbele ya safari, angalau historia itamtetea kwamba alikuwa na ujasiri wa kutamka: "Mfalme yu uchi" wakati wengine ndani ya ukumbi huo walikwepa kumhusisha na uozo huo wa CCM.
Je; Mheshimiwa Rais kajifunza kitu kutoka katika kosa hilo, na kutoka katika yaliyojiri Dodoma? Ni suala la muda tu tutapata jibu la swali hili.Tafakari.
- See more at: Raia Mwema - Makongoro Nyerere na ujasiri huu wa nadra CCM!


 
Hey Jf kumekucha,

Hali si shwari kati ya kapteni Makongoro Nyerere na Edward Lowassa. Taarifa za kina zinaeleza vuta nikuvute hiyo imezidi kupamba moto huku safari hii Makongoro akiamua kuvunja ukimya na kuweka bayana maamuzi yaliyofikiwa na NEC ya kumvua gamba Lowassa ni lazima yafanyike mara moja pasipo kusita.

Taarifa zaidi ambazo tumezinasa kwa njia ya simu kutoka huko Dar es salaam maeneo ya Kinondoni Biafra kutoka kwa mwandishi mmoja wa gazeti la Dira ya Mtanzania zinabainisha kuwa ni Makongoro Nyerere ndiye aliyeanika taarifa za Lowassa kutaka kuyaanika maovu ya Kikwete wiki moja iliyopita na huku wiki hii Makongoro huyohuyo akiibuka na madai mengine mazito kuhusu azma ya Kikwete kuwakingia kifua Lowassa na Chenge ili wasitemwe kwenye kikao kijacho, Makongoro amekaririwa akisema "hata kama kiwete akitaka amlinde huyu lowassa, kweli kaka yangu lowassa atatusamehe ni lazima tumng'oe bila kusita, itabidi tupinge hoja za kikwete kwa maana hana ubavu wa kutulazimisha"
Makongoro hawezi kufanya lolote kwa lowasa.miaka yote vua gamba mwishowe siku tisini ziliisha na had leo hakuna anaesema hiyo habari.chezea lowasa
 
Wiwiwiwiiiiii...,.. Ondokeni wazeee, ishieni wazeee, kalaleni wazeeeeee.......mtajibeba na lichama lenu. Wenyewe kwa wenyewe kazi ipo.
 
Huyu ndiye yule 'Nyoka mwenye makengengeza msaka pesa'?:)

Hilo ndilo li ccm ndugu! Si unacheki rangi yake? Likikugonga wala hutajua umegongwa na nini! Maana linafanana na mazingira. Kisha kwa jembe wanakufukia chap chap huku wakiendelea kuchukua chako mapema.
 
Jambazi sugu na fisadi papa lowasa kamwe hawezi kuwa rais wa nchi hii........................ni dhaifu kuliko hata kikwete
 
Hey Jf kumekucha,

Hali si shwari kati ya kapteni Makongoro Nyerere na Edward Lowassa. Taarifa za kina zinaeleza vuta nikuvute hiyo imezidi kupamba moto huku safari hii Makongoro akiamua kuvunja ukimya na kuweka bayana maamuzi yaliyofikiwa na NEC ya kumvua gamba Lowassa ni lazima yafanyike mara moja pasipo kusita.

Taarifa zaidi ambazo tumezinasa kwa njia ya simu kutoka huko Dar es salaam maeneo ya Kinondoni Biafra kutoka kwa mwandishi mmoja wa gazeti la Dira ya Mtanzania zinabainisha kuwa ni Makongoro Nyerere ndiye aliyeanika taarifa za Lowassa kutaka kuyaanika maovu ya Kikwete wiki moja iliyopita na huku wiki hii Makongoro huyohuyo akiibuka na madai mengine mazito kuhusu azma ya Kikwete kuwakingia kifua Lowassa na Chenge ili wasitemwe kwenye kikao kijacho, Makongoro amekaririwa akisema "hata kama kiwete akitaka amlinde huyu lowassa, kweli kaka yangu lowassa atatusamehe ni lazima tumng'oe bila kusita, itabidi tupinge hoja za kikwete kwa maana hana ubavu wa kutulazimisha"

Kesi ya nyani .....
 
Makongoro hana tofouti na hao wengne wapo kwenye sytem hyo hyo ya ulaji..labda tu kwakuwa alikuwa anakunxwa gongo ngrinaro arusha na sahv yupo kwenye wine ndyo ananza kutunisha misuli.,infact hana lolote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom