Makongoro, Muhongo wageukia Ubunge

Makongoro, Muhongo wageukia Ubunge

Magazetini

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2014
Posts
593
Reaction score
1,713
makongoro_.jpg

Siku chache baada ya kutangaza kuridhika na mapendekezo ya Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya kutompitisha kupeperusha bendera ya chama hicho kwenye kinyang’anyiro cha urais, Charles Makongoro Nyerere amejitosa kuwania ubunge katika Jimbo la Kawe, Dar es Salaam.

Pia, Profesa Sospeter Muhongo ambaye naye alikuwa miongoni mwa wagombea urais wa CCM, alichukua fomu ya kuwania Ubunge wa Musoma Vijijini. Baada ya kuchukua fomu, Waziri huyo wa zamani wa Nishati na Madini aliandika katika ukurasa wake wa Facebook: “Leo nimechukua fomu nagombea ubunge wa Musoma Vijijini bado ninadhamira ya dhati ya kuwatumikia Watanzania. Tusikate tamaa.”

Aidha, aliyekuwa mgombea urais mwingine, Peter Nyalali amechukua fomu kuwania ubunge Jimbo la Mbagala, sanjari na Mwichumu Msomi na Dominic Francis Haule.

Baadhi ya wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, Katibu wa Rais ni miongoni mwa waliojitokeza jana kuwania ubunge maeneo mbalimbali nchini.

Kawe: Mbali ya Makongoro, makada wengine 14 walijitokeza kuwania kiti hicho wakiwemo; Mtiti Butiku, Yusuph Nassoro, John Mayanja, Dickson Muze na Dk Wilson Babyebonela.

CHANZO: Mwananchi
 
Makongoro anaogopa kumuudhi Mukono, lakini jimbo la Butiama angepita kirahisi. Kawe anahangaika bure, hatopata kitu. kwa ccm.
 
Huyu Mhongo sio mwanasiasa haya mambo ya ubunge atayaweza wapi..? Ana majibu ya nyodo na hanaga busara kwenye kujibu hoja za kuudhi.. Hebu arudie mambo yake ya kisomi aliyokuwa akiyafanya kabla ya kuingizwa siasani na JK..
 
Huyu Mhongo sio mwanasiasa haya mambo ya ubunge atayaweza wapi..? Ana majibu ya nyodo na hanaga busara kwenye kujibu hoja za kuudhi.. Hebu arudie mambo yake ya kisomi aliyokuwa akiyafanya kabla ya kuingizwa siasani na JK..

Huyu ndo atawanyosha mafisadi ya chinichini kama Mengi.
 
Makongoro anaogopa kumuudhi Mukono, lakini jimbo la Butiama angepita kirahisi. Kawe anahangaika bure, hatopata kitu. kwa ccm.
Jimbo la Butiama siyo la Mkono, Mkono yuko Msoma vijijini, jimbo ambalo limegawanywa, jimbo jipya ndo anagombea Muhongo
 
Hivi mwananchi wa kawaida anaweza akawa fisadi bila ya mfumo ulioko kuruhusu hilo. Jaribu kuukwepa kodi na hauna wa kukukingia kifua uone dawa yake. Wanyooshane kwanza wenyewe kwa wenyewe halafu uone kama kuna mwananchi wa kawaida atakuwa fisadi sio upande mmoja anajidai mkali na upende mwingine anajipendekeza.

Huyu ndo atawanyosha mafisadi ya chinichini kama Mengi.
 
haya tuone wanafiki chagadema kama wataendelea kumshabikia, nakumbuka walikuwa wanamshabikia sana kwenye kinyang'anyiro cha kupitisha mgombea urais ccm. hadi leo sijajua kwanini walikuwa wanamshabikia
 
Hivi mwananchi wa kawaida anaweza akawa fisadi bila ya mfumo ulioko kuruhusu hilo. Jaribu kuukwepa kodi na hauna wa kukukingia kifua uone dawa yake. Wanyooshane kwanza wenyewe kwa wenyewe halafu uone kama kuna mwananchi wa kawaida atakuwa fisadi sio upande mmoja anajidai mkali na upende mwingine anajipendekeza.


Kwahiyo unataka kuniambia wakati wa uchaguzi mbowe anavyokopesha chama mikopo hewa na baadae kudai na riba ya 100%....tatizo ni mtu mwenyewe au mifumo ya chama?
 
Kama hili ni la kweli nina hakika hawezi kufanya mwenyewe bila msaada wa wanachama wengine. Jambo zuri au baya linalofanywa na kukubaliwa na watu kadhaa katika chama chochote huo ni mfumo.

Muhongo sijui Magufuli hakuna mtu wanaweza mnyosha kama mfumo wao utabaki ulivyo. Wataishi porojo tu action sifuri.
Kwahiyo unataka kuniambia wakati wa uchaguzi mbowe anavyokopesha chama mikopo hewa na baadae kudai na riba ya 100%....tatizo ni mtu mwenyewe au mifumo ya chama?
 
Kama hili ni la kweli nina hakika hawezi kufanya mwenyewe bila msaada wa wanachama wengine. Jambo zuri au baya linalofanywa na kukubaliwa na watu kadhaa katika chama chochote huo ni mfumo.

Muhongo sijui Magufuli hakuna mtu wanaweza mnyosha kama mfumo wao utabaki ulivyo. Wataishi porojo tu action sifuri.

Tumemuweka Magufuli kwa ajili ya special assignment ya kubadili mfumo...tunataka kurudisha heshma ya chama. Over!
 
Mwanangu mwenyewe Makongoro kakurupuka sana nadhani hakupata washauri wazuri. Kawe sio pa rahisi kuna dalili za kuvuliwa nguo na Bi Halima.
 
Naona unakubaliana na ukweli mfumo lazima ubadilike na sio kurudisha heshima ya chama, kurudisha heshima ya Tanzania. Namtakia kila la heri yeyote mwenye nia ya kweli ya kulibadilisha taifa hili.
Tumemuweka Magufuli kwa ajili ya special assignment ya kubadili mfumo...tunataka kurudisha heshma ya chama. Over!
 
haa haa kama makongoro alikatwa na kamati kuu sembuse wana kawe? nadhani atapewa kipigo cha mbwa mwitu huko kawe. tusubiri tuone...
 
Ndio hilo hilo jimbo la Butiama limekatwa kutoka Jimbo la Musoma vijijini, kwa hiyo Mkono atagombea Jimbo jipya LA Butiama ambako ndio kwao na Mhongo atasimama Musoma vijijini ambalo liko upande wa majita ambako ndiko maeneo ya kwao.
 
Hawa sasa wale pro-Chadema waliokuwa wapo upande wa Makongoro Nyerere, wakiongozwa na Yeeicko, Makongoro anakuja Kawe kumuondoa Halima Mdee.

Teh teh teh
 
Back
Top Bottom