Makonda umewaelimisha Makonda

Makonda umewaelimisha Makonda

hps300

Senior Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
170
Reaction score
152
Siku za kadhaa kuna habari ambayo Mheshimiwa Makonda kwa kushirikiana na chama wamiliki wa Dalala Dar es Salaam (DARCOBOA) Umoja wa wasafirishaji abiria (UWADAR) na chama cha wafanyakazi madereva (TAWDU) wamekubaliana kuwa walimu wa shule za msingi na sekondari katika manispaa za Kinondoni, Ilala na Temeke wasafiri bure kwenda na kurudi kazini, hii ni kuanzia saa 11 asubuhi mpaka saa mbili asubuhi na wakati narejea jioni kuanzia saa 9 mpaka saa 11.

Tumezoea kuona haya kwa askari wa majeshi ya ulinzi na usalama, yaani askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, Polisi, Magereza na wengine. Pamoja na kuwa kundi hili huwa wako kwenye mavazi maalumu na pia kutokana na unyeti wa kazi Makonda ( makondakta ) wamekuwa wakiwaogopa kidogo, lakini hutoacha kusikia maneno ya kejeli kama tumjaza mawe nk.

Sina uhakika walimu wataepukaje madhira ya kudharirishwa na wahudumu hawa wa daladala ukizingatia wengi wa walimu katika mji mikubwa ni wanawake. Pia sina hakika kama wao wanalifurahia hili,mi nadhani hiyo hela ingelipwa kupitia mishahara yao kwa maana ya transport allowance, au kuwe na mabasi maalumu (staff bus) ikiwa kweli huu mpango endelevu na unalenga kumaliza kero za walimu, lakini pia walimu hawako Dar peke yao na mikoani je itakuwaje? itakuwaje ikiwa mwalimu wa Dar ana high value tofauti na mwalimu wa Pwani?

Tuchukulie mfano, mwalimu atajisikiaje kupanda daladala na mwanafunzi wake, lakini mwanafunzi akilipa nauli na huku akiwa amesimama ili kumpisha mkubwa wake ambaye ni mwalimu?

Katika hili, sitashangaa kusikia zikiibuka kauli za ajabu kutoka kwa makondakta na wengine, hasa wakati watakapokuwa wanakusanya nauli kutoka kwa abiria na kukuta mwalimu akiwa amekaa kwenye kiti, lakini bila kulipa nauli huku mwanafunzi akiwa amelipa na kusimama kwenye daladala.
 
= madhila
= kudhalilishwa
Bahati nzuri sana hakuna mwandishi aliyewahi kuandika akawa sawa moja kwa moja lazima kuwepo na watu wa kufanya editing kama wewe je umelewa ujumbe wangu? pia mimi si mwalimu wa kiswahili na si mwandishi siyo, naweza andika vyovyote na chochote ili ujumbe ufike hivo.
 
Makonda amejitahidi kadri ya uwezo wake kupambana na walimu lkn napata Shaka juu ya walimu kukebehi hii offer nabkutaka kuwe na mbadara..
wafadhilaka wapundaka..
 
Makonda amejitahidi kadri ya uwezo wake kupambana na walimu lkn napata Shaka juu ya walimu kukebehi hii offer nabkutaka kuwe na mbadara..
wafadhilaka wapundaka..
Kwani Ww Unavyojua, Shida Za Waalimu Wa TANZANIA Ni Kukosa Nauli Za Kwenda Na Kurudi Kazini!!??
 
Siku za kadhaa kuna habari ambayo Mheshimiwa Makonda kwa kushirikiana na chama wamiliki wa Dalala Dar es Salaam (DARCOBOA) Umoja wa wasafirishaji abiria (UWADAR) na chama cha wafanyakazi madereva (TAWDU) wamekubaliana kuwa walimu wa shule za msingi na sekondari katika manispaa za Kinondoni, Ilala na Temeke wasafiri bure kwenda na kurudi kazini, hii ni kuanzia saa 11 asubuhi mpaka saa mbili asubuhi na wakati narejea jioni kuanzia saa 9 mpaka saa 11.

Tumezoea kuona haya kwa askari wa majeshi ya ulinzi na usalama, yaani askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, Polisi, Magereza na wengine. Pamoja na kuwa kundi hili huwa wako kwenye mavazi maalumu na pia kutokana na unyeti wa kazi Makonda ( makondakta ) wamekuwa wakiwaogopa kidogo, lakini hutoacha kusikia maneno ya kejeli kama tumjaza mawe nk.

Sina uhakika walimu wataepukaje madhira ya kudharirishwa na wahudumu hawa wa daladala ukizingatia wengi wa walimu katika mji mikubwa ni wanawake. Pia sina hakika kama wao wanalifurahia hili,mi nadhani hiyo hela ingelipwa kupitia mishahara yao kwa maana ya transport allowance, au kuwe na mabasi maalumu (staff bus) ikiwa kweli huu mpango endelevu na unalenga kumaliza kero za walimu, lakini pia walimu hawako Dar peke yao na mikoani je itakuwaje? itakuwaje ikiwa mwalimu wa Dar ana high value tofauti na mwalimu wa Pwani?

Tuchukulie mfano, mwalimu atajisikiaje kupanda daladala na mwanafunzi wake, lakini mwanafunzi akilipa nauli na huku akiwa amesimama ili kumpisha mkubwa wake ambaye ni mwalimu?

Katika hili, sitashangaa kusikia zikiibuka kauli za ajabu kutoka kwa makondakta na wengine, hasa wakati watakapokuwa wanakusanya nauli kutoka kwa abiria na kukuta mwalimu akiwa amekaa kwenye kiti, lakini bila kulipa nauli huku mwanafunzi akiwa amelipa na kusimama kwenye daladala.
Mkuu Naomba Kuweka Sawa Kidogo Hapa, Hayo Makundi Yote Yalioyataja Na Yanayoaminika Kupata Hiyo Huduma Ya Kusafiri Bure, Wana Usafiri Wao Wa Ofisi (STAFF BUSES) Huo Usafiri Wa Daladala Ni Wa Ziada Tu, Je Hao Waalimu Ikoje!!!!?
 
mmmhhh!!!

na weekend vip buuree??!!😀
 
kwahiyo ni full vitambulisho ety!!!

hehee sipati picha huo ugomvi wa waalimu na makonda wa daladala teh!!
 
Hapa Dar.hakuna siku mtu amelala kazini kwa kukosa nauli ya kurudi nyumbani.
 
Kuna namna nyingi Makonda angeweza kuwasaidia mwalimu zaidi ya hii...Kwanza amewasaidia watu ambao hawakumwomba na hawako tayari kwa hilo na sijui mkuu wa wilaya alijuaje kuwa kero kubwa ya walimu ni nauli kweli sijui..
 
angeleta mabasi tu hapo ingeleta heshma ! huu si ugomvi huu !! loh!
 
Kwani Ww Unavyojua, Shida Za Waalimu Wa TANZANIA Ni Kukosa Nauli Za Kwenda Na Kurudi Kazini!!??
Yeye ni mkuu wa wilaya ya Kinondoni na kwa maelezo yake analijua shida zao sasa kaonyesha njia ili wengine wawajibike juu yao..
 
Makonda amekurupuka. Angefanya la maana kama angefanya kikao na walimu ili apate mawazo yao kama kweli ana nia ya kuboresha maisha ya walimu
 
Mimi natabiri kushamiri kwa vitambulisho feki vya walimu raia wenye haja ya kusafiri bure maana sidhani kama namna iliyowekwa ili kudhibiti hali.
 
Bahati nzuri sana hakuna mwandishi aliyewahi kuandika akawa sawa moja kwa moja lazima kuwepo na watu wa kufanya editing kama wewe je umelewa ujumbe wangu? pia mimi si mwalimu wa kiswahili na si mwandishi siyo, naweza andika vyovyote na chochote ili ujumbe ufike hivo.
Unapokosolewa kumbuka unajifunza.

Hakuna anaejua/anaeweza kila kitu.

Wote tunajifunza.

Usiwe mkali, unachotakiwa kufanya ni kumshukuru anaekukosoa.

Kwakuwa anaekukosoa anakupenda.

Na ukae ukijua kwa kosa lako wewe utakalokosolewa, ujue mwingine/wengine tunajifunza kupitia makosa yako.

Neno moja,

Ahsante
 
Kwani Ww Unavyojua, Shida Za Waalimu Wa TANZANIA Ni Kukosa Nauli Za Kwenda Na Kurudi Kazini!!??
Kilio cha walimu ni cha mda mrefu sana na hiyo Idara kiujumla inakila aina ya changamoto si Tza tuu hata kwenye nchi nyingi zinazoendelea na zilizoendelea,Sasa pale panapopatikana MTU wa kuanza kukunjua mbawa zake na kuanza kuzikabiru baadhi ya changamoto asibezwe..
Tza ya leo ni Wafadhilaka wapundaka haswa kwenu nyinyi baya kwenu halifai na zuri alitakiwi kabisa na wala halifai..
 
Back
Top Bottom