Francis12
JF-Expert Member
- Sep 30, 2016
- 7,533
- 22,276
Paul Makonda umetokea UVCCM ghafla sasa hivi unawatisha watu na watumishi wa umma kwa kusema wewe sio Mwanasiasa..
Unawaita watumishi wa umma 'Vichaa' na kuwadhalilisha kwa kauli za kejeli na maamuzi yasiyozingatia utu, haki za binadamu, sheria zilizotungwa na Bunge na katiba ya nchi.
Unafika mahala unataka kuwaaminisha wananchi na watumishi wa umma kuwa uliposimama wewe amesimama Mungu, huko ni kutuingilia vibaya katika imani zetu na kulidhalilisha jina la Mungu ambalo kila alitajae kwa imani yake, analiheshimu.
Unaelekeza maamuzi ambayo sio ya ngazi yako, masuala ya ardhi, elimu, afya, ajira n.k. ni masuala ambayo uwakilishi wake ni ngazi ya Bunge na hoja kuelekezwa serikali kuu na sio TAMISEMI ngazi ya mkoa, masuala ambayo yanaligusa taifa zima ni masuala yanayopatiwa ufumbuzi na mawaziri na sio mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam.
Unafanya maamuzi ya kuwaweka ndani watumishi wa umma na viongozi wa serikali za mitaa kwa amri zako bila kujiridhisha na tuhuma zinazotolewa na wananchi kwa kutumia wataalamu na vyombo vya upelelezi kama Jeshi la polisi, TAKUKURU, n.k.
Unataka kuuaminisha Umma kuwa Tanzania ilipofikia sasa hakuna tena utawala bora unaozingatia sheria za nchi na katiba bali ni utashi wa kiongozi kutumia madaraka yake kumuwajibisha mtendaji aliyekosea kwa kumsweka ndani (rumande) bila mahakama kuthibitisha makosa.
Nilipolizungumza hili siku chache zilizotangulia, wengine waliniambia nimekurupuka kukosoa ziara zako na kwamba hawaniungi mkono.. Sasa nakumbuka usemi wa watu wa kale kuwa 'Mchonga meno, mji umemshinda", ni dhahiri Paul Makonda Dar es Salaam imekushinda na wananchi wanaelekea kukuchoka na kutokukupa ishirikiano.
Unawaita watumishi wa umma 'Vichaa' na kuwadhalilisha kwa kauli za kejeli na maamuzi yasiyozingatia utu, haki za binadamu, sheria zilizotungwa na Bunge na katiba ya nchi.
Unafika mahala unataka kuwaaminisha wananchi na watumishi wa umma kuwa uliposimama wewe amesimama Mungu, huko ni kutuingilia vibaya katika imani zetu na kulidhalilisha jina la Mungu ambalo kila alitajae kwa imani yake, analiheshimu.
Unaelekeza maamuzi ambayo sio ya ngazi yako, masuala ya ardhi, elimu, afya, ajira n.k. ni masuala ambayo uwakilishi wake ni ngazi ya Bunge na hoja kuelekezwa serikali kuu na sio TAMISEMI ngazi ya mkoa, masuala ambayo yanaligusa taifa zima ni masuala yanayopatiwa ufumbuzi na mawaziri na sio mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam.
Unafanya maamuzi ya kuwaweka ndani watumishi wa umma na viongozi wa serikali za mitaa kwa amri zako bila kujiridhisha na tuhuma zinazotolewa na wananchi kwa kutumia wataalamu na vyombo vya upelelezi kama Jeshi la polisi, TAKUKURU, n.k.
Unataka kuuaminisha Umma kuwa Tanzania ilipofikia sasa hakuna tena utawala bora unaozingatia sheria za nchi na katiba bali ni utashi wa kiongozi kutumia madaraka yake kumuwajibisha mtendaji aliyekosea kwa kumsweka ndani (rumande) bila mahakama kuthibitisha makosa.
Nilipolizungumza hili siku chache zilizotangulia, wengine waliniambia nimekurupuka kukosoa ziara zako na kwamba hawaniungi mkono.. Sasa nakumbuka usemi wa watu wa kale kuwa 'Mchonga meno, mji umemshinda", ni dhahiri Paul Makonda Dar es Salaam imekushinda na wananchi wanaelekea kukuchoka na kutokukupa ishirikiano.