MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,255
- 8,027
Huyu bwana kuna kauli ambayo mpaka leo wazalendo tunaitafakari nini hatima yake, "Atakayeandamana ni halali yangu" .Hii halali yake kapewa na nani? Kiongozi aliyepewa dhama ya kuwa mbele ya wananchi wenye itikadi mbali mbali unatamka kauli kama hii anamtisha nani?
Nashangaa sana viongozi wa dini wapo kimya kwenye kauli kama hizi, sijui wanafikiria nini, kwanini hakuna kiongozi hata mmoja wa kujitokeza na kukemea kauli kama hii? Viongozi wetu wa dini ni Mungu yupi wanaotuhubiria tumwabudu? Tuwaamini kwa lipi ilihali mambo muhimu kama haya wanaogopa kuyakemea? Wako nyuma ya nani?
Wanamuogopa nani?Nafasi yao kwenye amani ya taifa letu tulivu ni nini? Inauma sana kwakweli.
Nashangaa sana viongozi wa dini wapo kimya kwenye kauli kama hizi, sijui wanafikiria nini, kwanini hakuna kiongozi hata mmoja wa kujitokeza na kukemea kauli kama hii? Viongozi wetu wa dini ni Mungu yupi wanaotuhubiria tumwabudu? Tuwaamini kwa lipi ilihali mambo muhimu kama haya wanaogopa kuyakemea? Wako nyuma ya nani?
Wanamuogopa nani?Nafasi yao kwenye amani ya taifa letu tulivu ni nini? Inauma sana kwakweli.