Makonda, Jitokeze hadharani utuombe radhi wanasheria

Makonda, Jitokeze hadharani utuombe radhi wanasheria

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Mh. Paul Makonda,Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,nakusalimu. Ndugu Makonda,umesikika ukisema kuwa umewaajiri wanasheria saba kwa kuwasaidia wananchi kwenye kuingia mikataba au kufungua kesi kwenye mahakama. Ingawa wazo na nia yako ni njema,umedhalilisha tasnia ya sheria.

Umesema kuwa unawalipa wanasheria hao asilimia sabini na tano ya mshahara wako kwa mwezi. Pamoja na kutojua mshahara wako kwa mwezi,nina hakika asilimia hiyo haiwezi kuwalipa wanasheria saba. Tasnia ya sheria ni moja ya tasnia kongwe,adhimu na ghali hapa duniani. Madai yako yanaidhalilisha tasnia hii ya sheria. Wanasheria saba walipwe asilimia 75 ya mshahara wako!? Hakika hiyo ni dharau.

Ndugu Makonda,najua wewe ni mwanasiasa na kiongozi wa kiserikali. Kauli zako zinapaswa kuchujwa vyema kabla ya kutolewa. Kwa taarifa yako,hakuna wanasheria saba wanaoweza kuajiriwa kwa mshahara wa kiudhalilishaji kama huo. Hata wanafunzi wa sheria huwezi kuwapata,seuse wanasheria.

Natoa rai kwako Ndugu Paul Makonda kujitokeza hadharani na kuwaomba radhi wanasheria wa nchi hii kwa kauli yako ya kushusha thamani yao. Nikiwa mwanasheria,nimeshtushwa na kusikitishwa na kauli yako.
 
Kuna tofauti kati ya wanashaeria ma mwananchi anayejua/mwenye uzoefu na sheria! Sijui amewaajiri wapi kati ya hao.
 
Wewe unafikiri kumpiga vibao mtu mzima mchezo? Lazima uweweseke tu
 
wanasheria wengi sana kitaani hawana kazi tunawatoa mkwanja wa kula sasa peter unalalamika nini,degree ya sheria imekuwa kama ya education.mh hajatudharau ila ndo hali halisi huku mtaani kila mwaka llb wanagraduate 5000 unadhani wote wanaenda wapi au unatafuta umahalufu.
 
Ni vema tukapata hiyo nukuu ya bwana Makonda, au neno kuajiri linareflect full time?

Maana inaweza kuwa masaa manne kwa wiki wajameni..Ila huyo Madereva mwenyewe simfagilii.
 
Paul Makonda dharau n moja ya sifa zake
.........mshahara wa Pinda ni million 25 per month (kwa tetesi nilizonazo) yeye anapata mshara kias gan hadi 70% ya mshahara wake awalipe wanasheria7? Labda kama kawasomesha yeye sasa ndo wanalipa gharama alizotumia kuwapeleka shule
 
Ungekua wewe ungekuja kujibu ombi too low kama hili?hizi ndo type ya siasa za maji taka discuss issues not people
 
Ungeiweka kimahesabu ingekaa vizuri zaidi.
Mkuu wa wilaya hulipwa mmilioni 2 kama mshahara

75% ya mshahara wake ni milioni moja na laki tano.

1500000/7 = 214,285.7

Kweli wanasheria wa Tanzania wanalipwa kidogo sana, hadi makonda anaweza kuajiri 7?.

acha urongo,huo sio mshahara wa mkuu wa wilaya.Tafuta taarifa sahihi,ila huo siyo mshahara wao
 
Back
Top Bottom