Mimi ninapingana sana na wewe mtoa mada.
Mbinu aliyotumia Makonda ni mbinu aliyoibuni yeye na kuiona kuwa ingemsaidia kufanikisha mapambano. Hakuna kiongozi yeyote katika mihimili yote ya serikali aliyethubutu angalao kujaribu kwa mbinu yoyote ile kuianzisha vita hii kwa miaka yote tangu itangazwe.
Hao polisi unaodai walipewa orodha na Kikwete ili wafuatilie, ndiyo hao mojawapo uliosikia wameswendemwa ndani. Kupewa majina hayo kwao ilikuwa ni kugawiwa utajiri.
Nikuulize ni miaka mingapi kwa jambo moja kushindwa kutolewa maamuzi ya kuanzishwa?
Hao wahusika ambao majina yao yalikabidhiwa polisi, taja ni nani mojawapo aliyefuatiliwa akabainika na kutangazwa kama ni adui wa taifa katika biashara hiyo haramu?
Hivi wote waliotajwa, hakuna hata mmoja aliyebainika kujihusisha na biashara hiyo, kwamba walibambikiwa kama unavyotaka kutuaminisha?
Vyovyote iwevyo, tafsiri ya Makonda kutaja majina hakudhamiria hao mateja wafungwe, ila alitaka wawataje wahusika wakuu ambao serikali ina uchu wa kuanza nao. Hakuhitaji kithibiti, ndiyo maana aliwaita kwa kusema anawaita akutane nao ili wamueleze kwa nini wanatajwa katika sakata hilo. Mbinu aliyoitumia ni njema kabisa na imesaidia sana kuweza kupata mnyororo wa wafanya biashara hiyo. Hao vidagaa alielewa kuwa si wahusika wakuu ndiyonaana hakuhitaji kuwashitukiza na kuwapekua, ingawa uwezo wa kufanya hivyo ulikuwepo.
Wewe umetoa mchango wako kwa uelewa wako, lakini yaweza kuwa mawazo hayo umepachikiwa kutokana na kampeni zinazopigwa sasahivi za kudhoofisha vita hii. Ninasema hayo kutokana na ujazo wa vina vya thread yako.
Kila kitu hapa duniani huwa kina faida na hasara, wewe umetaja hasara tupu za matokeo ya uanzishwaji wa vita hiyo, haukutaja faida ya mbinu hizo alizotumia.
Kaa ukijua nchi hii watu wameelimika kuweza kuchuja jambo jema, la ukweli na figisu za ghiriba pia wanazijua.
Fanyeni muwezavyo kutetea ili kudhoofisha vita hii, lakini raia wema wanamuunga mkono sana mheshimiwa Makonda na rais wake Magufuli, kwa kuwa wanayotenda ni kwa manufaa yetu sote na si kwa manufaa yao binafsi.