Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,498
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amemtaka Msajili wa Vyama vya Michezo nchini, Abel Ngilangwa kuipa Simba majibu ya kinachoendelea kuhusu mchakato wa mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji.
Makonda amesema kuwa msajili anatakiwa kabla ya mwezi huu kumalizika, awe ametoa majibu kwa Wanasimba.
Soma zaidi > Nini kinaendelea ndani ya Klabu ya Simba?
“Msajili wa michezo nilitaka mkamilishe taratibu za Simba. Na nilitaka niwahakikishie kwamba katika kipindi ambacho sheria na kanuni zitafuatwa sana ni hiki cha uongozi wangu.
“Kamilisha na ikiwezekana kabla ya mwezi huu uwape majibu Wanasimba. Tunachotaka sisi tuone timu hizi zikifanya vizuri. Kabla ya mwezi huu, jambo hili liwe limekamilika,” amesema Makonda.
Soma zaidi > Nini kinaendelea ndani ya Klabu ya Simba?
“Msajili wa michezo nilitaka mkamilishe taratibu za Simba. Na nilitaka niwahakikishie kwamba katika kipindi ambacho sheria na kanuni zitafuatwa sana ni hiki cha uongozi wangu.
“Kamilisha na ikiwezekana kabla ya mwezi huu uwape majibu Wanasimba. Tunachotaka sisi tuone timu hizi zikifanya vizuri. Kabla ya mwezi huu, jambo hili liwe limekamilika,” amesema Makonda.