Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,411
Paul Makonda anazunguka nchi nzima,anafanya maigizo kwa wananchi, kujidai wanaripoti matatizo kwake na yeye kuyatatua ambapo huenda ,so far amepita sehemu ambazo mteuzi wake hajafika.
Mwenezi anazunguka nchi nzima si KUTATUA kero za wananchi, bali anachokifanya ni kuuonesha umma kuwa hii nchi HAINA Serikali.
Kila anakokwenda raia wamejaa wamemzunguka na shida lukuki! Utakuta eneo lina RC, RAS, DC, DAS, DED mpaka OCD. Bado kuna TAKUKURU, maafisa ardhi, wajumbe wa nyumba 10/10 na kila idara nyeti lakini wote ni USELESS tu.
Wanatafuna tu kodi za wana-nchi! Hata kama ni fedha za CCM -lakini msafara una watu wanaolipwa na serikali ambayo ni fedha za wasio nawa CCM, watendaji wanaacha ofisi wanazurura Makonda kwenye ziara za maigizo kumtangaza mteuzi wake ambaye anajua fika hakubaliki, hakupigiwa kura lakini hata ambaye alipigiwa kura huenda si yeye aliyeshinda.
Kama tuna Mh Majaliwa[waziri mkuu mkali na mchapakazi], haya akaletewa Dotto Biteko [Naibu waziri mkuu] bado inaonekana wana-pwaya na sasa kum'leta Makonda haina shida ,ila sasa kukusanya watu muda wa kazi na kufanya maigizo ni kuwaonea maskini wa kitanzania ambao hawajitambui.
Jamaa anakusanya wananchi wanaoitwa 'wanyonge', halafu anawauliza "haya semeni matatizo yenu mmoja baada ya mwingine!" Kisha wananchi wanawataja viongozi wa maeneo yao kama DC, DED, wenyeviti wa mitaa kama chanzo cha matatizo yao – ambao wote hao ni wana chama tawala!
Cha kushangaza zaidi, Bashite anatoa 'maelekezo' kwa watu HAO HAO waliosababisha matatizo sugu kwa MIAKA yote kwamba waenda WAKAYATATUE ndani ya MASAA au SIKU! Wananchi nao WANAPIGA MAKOFI wakiamini shida zao zimetatuliwa. Utadhani hii ni mara ya kwanza kwa viongozi kufanya haya MAIGIZO! Msafara ukiondoka, kila mtu anarudi nyumbani amechoka, shida ziko pale pale.
Enyi wananchi, muda umefika wa kukataa ujinga kwa vitendo. Muda wa kudai #KatibaMpya
Mwenezi anazunguka nchi nzima si KUTATUA kero za wananchi, bali anachokifanya ni kuuonesha umma kuwa hii nchi HAINA Serikali.
Kila anakokwenda raia wamejaa wamemzunguka na shida lukuki! Utakuta eneo lina RC, RAS, DC, DAS, DED mpaka OCD. Bado kuna TAKUKURU, maafisa ardhi, wajumbe wa nyumba 10/10 na kila idara nyeti lakini wote ni USELESS tu.
Wanatafuna tu kodi za wana-nchi! Hata kama ni fedha za CCM -lakini msafara una watu wanaolipwa na serikali ambayo ni fedha za wasio nawa CCM, watendaji wanaacha ofisi wanazurura Makonda kwenye ziara za maigizo kumtangaza mteuzi wake ambaye anajua fika hakubaliki, hakupigiwa kura lakini hata ambaye alipigiwa kura huenda si yeye aliyeshinda.
Kama tuna Mh Majaliwa[waziri mkuu mkali na mchapakazi], haya akaletewa Dotto Biteko [Naibu waziri mkuu] bado inaonekana wana-pwaya na sasa kum'leta Makonda haina shida ,ila sasa kukusanya watu muda wa kazi na kufanya maigizo ni kuwaonea maskini wa kitanzania ambao hawajitambui.
Jamaa anakusanya wananchi wanaoitwa 'wanyonge', halafu anawauliza "haya semeni matatizo yenu mmoja baada ya mwingine!" Kisha wananchi wanawataja viongozi wa maeneo yao kama DC, DED, wenyeviti wa mitaa kama chanzo cha matatizo yao – ambao wote hao ni wana chama tawala!
Cha kushangaza zaidi, Bashite anatoa 'maelekezo' kwa watu HAO HAO waliosababisha matatizo sugu kwa MIAKA yote kwamba waenda WAKAYATATUE ndani ya MASAA au SIKU! Wananchi nao WANAPIGA MAKOFI wakiamini shida zao zimetatuliwa. Utadhani hii ni mara ya kwanza kwa viongozi kufanya haya MAIGIZO! Msafara ukiondoka, kila mtu anarudi nyumbani amechoka, shida ziko pale pale.
Enyi wananchi, muda umefika wa kukataa ujinga kwa vitendo. Muda wa kudai #KatibaMpya