Makato na tozo yamefika pabaya, wahusika fanyeni hima mrekebishe hali

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Mimi ni mteja wa NMB Bank. Katika kurahisisha huduma zangu za kibenki, nimejiunga na huduma ya NMB Mobile Banking. Huwa nafanya miamala yangu kutoka na kwenda benki yangu. Juzi, nilitaka kufanya muamala wa kutoa pesa benki kupeleka kwenye tigopesa.

Kila nikijaribu kuingia kwenye menu ya NMB Mobile sifanikiwi. Sikuwa najua tatizo na hivyo sikufanikisha muamala wangu. Mambo yangu niliyotaka kuyafanya yakakwama. Niliamua kumshirikisha mwenzangu mwenye huduma kama yangu. Yeye ndiye aliyenifumbua macho.

Akaniambia na mimi nikathibitisha kuwa kama huna salio la vocha kwenye simu yako basi huwezi kuingia kwenye menu ya NMB Mobile. Nikaambiwa na kuthibitisha kuwa kila unapoingia menu hiyo, vocha hukatwa. Kumbe, muamala wangu haukufanikiwa kwakuwa sikuwa na vocha!

Kuna makato kwenye vocha na fedha inayotumwa. Makato na tozo kulia na kushoto. Nimeambiwa (bado sijathibitisha) kuwa hata kuingia kwenye menu ya tigopesa kunahitaji uwepo wa vocha simuni ili nayo ikatwe. Tozo na makato yamefika pabaya, yanayafanya maisha yetu kuwa magumu zaidi.

Wahusika fanyeni hima mrekebishe hali hii. It is too much!
 
Kwa hali ilivyo hata kama umejiunga na kifurushi cha sms haisaidii! Kwa nini kuwe na tofauti katika matumizi ya kifurushi?

Na ukiweka tuseme vocha ya sh. 500, baada ya kumaliza muamala wako wa simbanking hutajua balance itakavyotoweka.

Upuuzi mtupu!
 
Mkuu malalamiko ya nini? Mbona makato kidogo sana haya. Tuwe wazalendo kwa kulipa kodi. Hutaki viongozi wetu wapate nafuu ya kuongoza? Hili litawezekana tu kama utalipa kodi tena kwa kiwango kikubwa sana. Usifikirie yale maV8 yanaendeshwa kwa maji!!!
 
Kuhusu makato kweny huduma za kibenki kwa watumiaji wa Vodacom wana fahamu yalikuwepo mda mrefu tu ambapo walikua wakichaji 20 Tshs/sec kila ukiingia kwenye ile Menu ya benki ukiwa huna salio maanake huwezi kuaccess huduma ya kibenk

Tigo ndio wame anza mwezi huu august huo utaratibu wao wanachaj tshs 100 ili uweze kupata huduma ya kibenk kwa hiyo sio jambo geni

ila Mama ana upiga mwingi balaaaaa
 
... fikiria scenario hii;

... uko mbali ila una kabiashara mahali ambako umeajiri kijana ambako kana-make max. of 30,000/= profit per day. Huyu kijana kila ikifika jioni ni lazima akurushie mauzo ya siku hiyo na kwa kuwa kesho yake anahitaji kufanya manunuzi ya bidhaa kwa ajili kesho ni lazima kesho yake umrushie fedha kwa ajili hiyo.

Kwa hiyo utaratibu ni yeye kukurushia jioni baada ya mauzo ya siku na wewe kumrushia asubuhi kufanya manunuzi. Imagine hizo tozo! VAT na kodi nyingine sijui za manispaa bila kusahau pango (through LUKU), n.k. ziko pale pale! Tozo hii ni mbaya, inafilisi biashara haifai!
 
Install nmb app ndugu.
Hii unaingia katika menu ya bank bila kuhitaji kuwa na salio la vocha zaidi ya bundle la internet, of which inatumia internet kidogo. Lakini pia ukiangalia salio la akaunt yako kwa nmb app hawakuchaji kitu wakati kwenye menu ya kuingia kawaida wanakuchaji sh 600 kwenye akaunt yako
 
Mimi ni mteja wa NMB Bank. Katika kurahisisha huduma zangu za kibenki, nimejiunga na huduma ya NMB Mobile Banking. Huwa nafanya miamala yangu kutoka na kwenda benki yangu. Juzi, nilitaka kufanya muamala wa kutoa pesa benki kupeleka kwenye tigopesa.

Kila nikijaribu kuingia kwenye menu ya NMB Mobile sifanikiwi. Sikuwa najua tatizo na hivyo sikufanikisha muamala wangu. Mambo yangu niliyotaka kuyafanya yakakwama. Niliamua kumshirikisha mwenzangu mwenye huduma kama yangu. Yeye ndiye aliyenifumbua macho.

Akaniambia na mimi nikathibitisha kuwa kama huna salio la vocha kwenye simu yako basi huwezi kuingia kwenye menu ya NMB Mobile. Nikaambiwa na kuthibitisha kuwa kila unapoingia menu hiyo, vocha hukatwa. Kumbe, muamala wangu haukufanikiwa kwakuwa sikuwa na vocha!

Kuna makato kwenye vocha na fedha inayotumwa. Makato na tozo kulia na kushoto. Nimeambiwa (bado sijathibitisha) kuwa hata kuingia kwenye menu ya tigopesa kunahitaji uwepo wa vocha simuni ili nayo ikatwe. Tozo na makato yamefika pabaya, yanayafanya maisha yetu kuwa magumu zaidi.

Wahusika fanyeni hima mrekebishe hali hii. It is too much!
Sijawahi Ona kitu kama hiki nazani watawala akili zao zimefika mwisho wa kufikili,kwa Sababu katika Hali ya kawaida huwez kufanya yaliyofanyika .Hawa watu Wana laana tayali,inauma Sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom