Makapuku Forum

NUKUU NO 1#

Ni wakati sasa kwa wananchi wa Tanzania kuamka kutoka usingizini.
Lazima tufanye kazi kwa bidii.
Tumenyonywa vya kutosha, tumedhalauriwa vya kutosha na kuuzwa hadharani katika minada kama mbuzi kwa ajili ya unyonge wetu
Sasa lazima tuamke na tuungane pamoja ili tusinyonywe tena wala kudharauliwa tena.


Maneno haya yamepata kutamkwa na Mwalimu Julius Nyerere, Feb 7,1969, Handeni Mkoani Tanga, alipokuwa akifungua shule mpya ya msingi eneo la Mzundu ambayo ujenzi wake uligharimu shilingi 17,500
 
NUKUU NO 2#

Wananchi pia walizungumzia hifadhi ya Jamii, hasa kwa wazee
Wanasema wafanyakazi wanamifuko ya hifadhi ya Jamii na mishahara yao inaongezwa kila wakati

Kwa wakulima, mapato yao ni madogo na wakizeeka hawana hifadhi yoyote.
Hata matibabu ya wazee sio bure kama utaratibu wa serikali unavyoelekeza, kwa shart wanunue dawa wakati uwezo wao wa kifedha ni mdogo

Maneno haya yalisemwa na aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba, jaji Joseph Warioba, katika hotuba yake kwenye bunge maalumu la katiba, Mach 2014
 
NUKUU NO 3

Wanachokitaka watu wetu ni kushirikishwa katika kufanya uamuzi wa ngazi mbali mbali kuhusu maisha yao, ili hatimaye, wawe na fursa ya kusimamia moja kwa moja uamuzi huo hadi kufika kilele cha mafanikio

Maneno haya yalipata kutamkwa na aliyekuwa Rais wa Namibia, Samuel Daniel Nujoma
Alizaliwa Mei 12,1929
 
Ufafanuzi murua kabisa.
Uwe unatusaidia kwenye mambo haya ya Muziki, wengine kama mimi hatupo nondo.
 
Hapo sawa mkuu
 
hahaha gharama za ujenzi ni 17,500.

Hela ambayo hata Mchele kilo 10 haitoshi.
 
 

Walimsumbua tu kuandika katiba wkt tyr walikuwa na katiba yao mfukoni
........
 

Anayejua Kireno atafsiri
.......
 

Attachments

  • IMG_20161010_184713.jpeg
    14.4 KB · Views: 27
Jaji Warioba a.k.a Mzee Kigogo namkubali sana.

Hawa ndio Viongozi wa mwishomwisho ambao ni Wazalendo na sio wale waliojijengea maduka ya dawa majimboni mwao badala ya wilayani kwenye Hospitali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…