Peter Moris ( 33 ) fundi ujenzi Mkazi wa Mlole anashikiliwa na Polisi Kigoma kwa kutuhumiwa kuhusika na mauaji ya Watu saba yaliyotokea katika Kijiji cha Kiganza Mkoani Kigoma huku sababu zikitajwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.
Kamishina wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi Tanzania, Lebaratus Sabas amethibitisha kukamatwa kwa Mtuhumiwa huyo baada ya siku tatu za upelelezi juu ya tukio hilo lililotokea usiku wa kumkia July 3,2022.
Katika mahojiano na Polisi Mtuhumiwa Peter Moris anadai kumtuhumu January Mussa ambaye nae amefariki katika tukio kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Mke wake na hivyo kupelekea kutenda tukio hilo.
Majina ya Watu waliofariki ni Tilifera Toyi ( 70), January Mussa (34) Sara Dunia(28), Joel Mussa (40), Christina Razalo (9), James Joel (7) na James January (3).