Makapuku Forum

KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA [emoji471]
.
AZAM FC [emoji1241] [emoji739] [emoji1093] PYRAMIDS FC
[emoji354] 09:00 jioni
[emoji909] Azam Complex
.
Nyota za zamani wa Al Ahly na Brighton, Ramadan Sobhi ndiye mchezaji wa kuchunga zaidi katika kikosi cha Pyramids FC kutokana na uwezo wake binafsi wa kufunga mabao na kupiga pasi za mwisho.
.
Kila la kheri Azam
 
| MNYAMA ametua salama Gaborone, Botswana
.
SIMBA imetua Botswana kutekeleza majukumu mazito ya kimataifa dhidi ya Jwaneng Galaxy.
.
Mmoja wa viongozi wa Simba amefunguka kwamba wamedhibiti mianya yote ya hujuma Botswana na wameafikiana kwamba timu hiyo ifikie nje kidogo ya mji lakini siyo mbali na Uwanja wa mechi ili kuzuia hujuma.
.
Amesisitiza ndani ya kambi hiyo kutakuwa pia na ulinzi mkali kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa.View attachment 1976377
 
Kisa Kombe la Dunia, Lingard kusepa United
.
Barcelona na AC Milan zinaonekana kuwa na nafasi kubwa ya kuipata saini ya kiungo wa Manchester United na England, Jesse Lingard, 28, dirisha lijalo la usajili.
.
Lingard mwenyewe ndio anatamani kuondoka kwa sababu anahofia kutupwa nje ya kikosi cha England kitakachoshiriki kombe la Dunia mwakani. Mkataba wake wa sasa unamalizika mwisho wa msimu.
 
[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

Siku kadhaa nyuma takribani mwezi na nusu niliandika kitu kuhusu UMUHIMU WA NETWORK haswa nikiigusia klabu ya Simba

Network nikasema zipo nne! FEEDER CLUB vs BIG CLUBS, CLUBS VS AGENCIES, CLUBS VS MEDIA na CLUBS vs FEDERATION, Nikatoa Maelezo yangu na kuliacha lipite

Kutokana na changamoto za COVID 19 hivi sasa kumekuwa na idadi maalum ya Mashabiki kuingia viwanjani hii ikiwa inasimamiwa na CAF wenyewe! Ila inatofautiana kati ya klabu na klabu

Simba imetoka taarifa kuwa mechi yao wanaruhusiwa Mashabiki 15,000 kwenye dimba la Mkapa, Biashara ni mashabiki 5,000 pale pale kwa Mkapa na Azam ni 2,000 pekee

Nikatweet kitu kukumbusha post yangu ya miezi nyuma kuhusu NETWORKING! Haswa kwenye CLUB VS FEDERATIONS, yani Klabu na Shirikisho eidha ni TFF au CAF Ila mahusiano yenu Yanaleta tija kubwa kwenye jambo lolote

Nikutumia mfano wa msemo mwepesi sana unasema “The corporate world works differently from the streets” kifupi taasisi zinaendesha mambo yao tofauti na watu wa mtaani wajuavyo, bila mahusiano mazuri ni kuteseka ni lazma ujenge mahusiano

Tanzania Leo hii amepata mkopo kutoka IMF simply ni Network, Ahly anafanya vizuri ukiachana na uwekezaji basi ni Network nzuri na Mashirikisho, hivyo ndivyo taasisi hufanya Kazi duniani

Rais wa CAF Patrick Motsepe ni Rafiki wa karibu na Mwekezaji wa Simba, Rais wa CAF ile klabu yake ni Marafiki wa karibu na Simba, Rais wa CAF ni Rafiki wa karibu na CEO wa Simba, Klabu ya Simba ni marafiki wa karibu na CAF mpaka kuwatambua kwenye SUPERLEAGUE, hizi ni networks

Ulaya hao Real Madrid, Manchester United na miamba mingi mpaka ikasemekana wanapendelewa na UEFA ikazuka HEATED BALLS SCANDAL, Lakini ni watu tu kutojua kuwa Network nzuri inaleta matokeo chanya

Nitaomba takwimu ya timu inayoingiza Mashabiki wengi zaidi ya Simba ukanda huu wa CECAFA kwa ruksa ya CAF, nitaomba takwimu Kama kuna klabu au timu ya taifa imeingiza Mashabiki wengi kwa ruksa ya CAF hivi karibuni zaidi ya hii ya SIMBA

The corporate world works differently from the streets

 
[emoji3578][emoji3578] Farhan Jr

KOCHA THIERRY HITIMANA, BINADAMU BORA NJE YA UWANJA (final) 2

….. yule Staff pale akaniambia benchi lote la Ufundi la Simba linaishi kwenye hotel ile hivyo nikaunganisha picha kuwa yule Mzungu alieniita mwanzo sikukosea ni Kocha pia wa Simba

Sasa wakati Thierry anacheck game ya Namungo kwenye TV, wachezaji wale watatu wakawa wanapiga nae stori za kawaida tu, wakamuuliza mbona yuko pale reception wakati ule?

Kocha Thierry akajibu kuna materials zake kutoka Ujerumani zimefika na Rafiki yake sasa amekaa pale kwa muda ila hajafika hivyo anafanya utaratibu aende yeye ila hotel aliyomtajia haijui

Basi kwakuwa sisi tulikua tunaondoka, Rafiki yangu mmoja ambaye ni Mchezaji wa Yanga akamwambia basi Mwalimu sisi tutakufikisha hiyo hotel kwakuwa ni njia yetu ya kupita

Kocha alishukuru sana tukaenda nae mpaka kwenye gari, wakati tunakuja ile siti ya mbele alikaa Mwanangu wa Yanga, ila akarudi siti ya nyuma nikamuuliza kwanini alinijbu ni nidhamu sahihi Kocha kukaa mbele na wachezaji nyuma

Basi tukaanza safari wachezaji watatu, Kocha na Mimi ila bahati mbaya tairi ya mbele ilipata pancha mbele tu kidogo, ikatulazimu sote tushuke, tena ni Kocha alikuwa wa kwanza kugundua gari haipo Sawa

Sote tukasema Mwalimu tukuitie BOLT au UBER wewe uwahi ila akasema hapana, tulikua sote safari moja na kwakuwa mmesahau spare tyre basi ngoja niende hotelini pale nimuombe Kocha mwenzangu gari yake kisha niondoke na mmoja wenu tukafate spare

Basi akarudi hotelini na akarejea na funguo ya gari ya Kocha wa Makipa wa Simba, kisha akamwambia Mchezaji mmoja aende nae wachukue spare warudi tufunge kisha tuondoke sote pamoja na sio yeye kutuacha

Basi ikawa hivyo pale, mmoja akaondoka na Mwalimu kisha kurudi na tyre nyingine ikafungwa na tukaondoka wote kumpeleka Mwalimu safari yake

Katika hali ya kawaida angekuwa mwingine angetuacha pale, imagine eneo ambalo hata garage ni tabu kupatikana! Huo ndio UBINADAMU! Wachezaji walikuwa Binadamu na Kocha alikuwa Binadamu
 
Leo ni kujipimia [emoji23]

Dakika ya 8 tayari tunaongoza kwa mabao 2-0.
TotalEnergiesCAFCL
NguvuMoja

Nyieeeee na hii ndio simba bwana [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…