Makapuku Forum

EDO: UGONJWA WA KUMLAUMU SAMATTA UTAKWISHA LINI?
.
Mara baada ya kumalizika kwa pambano kati ya Tanzania dhidi ya Benin pale Uwanja wa Mkapa, mwandishi mmoja asiyejitambua alimfuata Mbwana Samatta na kumuuliza swali. “Mashabiki wamekuwa wakisema wewe hauna mchango mkubwa ukirudi nyumbani tofauti na Ulaya.” Kudai kwamba mwandishi asiyejitambua ni kitu sahihi zaidi. Huyu alikuwa mwandishi wa michezo au alikuwa mwandishi wa siasa? Huyu alikuwa mwandishi wa masuala ya jamii au alikuwa mwandishi wa masuala ya mazingira?
.
Hii ilikuwa ni mechi ya soka ambayo Mwandishi alikuwepo uwanjani. Mwandishi hana maoni yoyote ya maana licha ya kuutazama mpira kwa dakika tisini. Wakati yeye ndiye ambaye alipaswa kutoa mwongozo kwa mashabiki, bahati mbaya yeye ndiye ambaye anapewa mwongozo na mashabiki.
.
Samatta anacheza vizuri akiwa na Stars ingawa kwa sasa hajafunga sana. Akiwa na Stars anacheza chini. Anachukua mipira, anakokota, anapiga pasi za kuunganisha timu. Inawezekana anafanya haya kwa sababu ya timu yetu ilivyo. Alipokuwa kule Genk aliwahi kuniambia kwamba kocha wake alimtaka asimame katikati tu na kufunga. Ni tofauti na mpira alioondoka nao akiwa Simba ambapo alikuwa anakokota kwa muda mrefu na kufunga. Kule walikuwepo kina Leon Bailey wa kumfanyia kazi hizi. Yeye alihitajika kusimama pale katikati tu. Huku Tanzania Samatta anacheza ule mpira wake wa zamani. Kuna akina nani zaidi wa kumfanyia kazi? inabidi pia ajifanyie kazi nyingi ambazo Ulaya huwa anafanyiwa zaidi na kujikuta akiwa mviziaji.
.
Mwandishi hawezi kuliona hili kwa sababu kila mtu anasubiri Samatta afunge tu basi. Samatta asipofunga anabebeshwa mzigo wa lawama mitaani na katika mitandao ya kijamii. Ni kitu cha kawaida kwa sababu amekuwa mhanga wa ukubwa wake. Na hasa linapokua suala kwamba yeye ni Mtanzania.
.
Watanzania wamezoea lawama. Hawawapendi watu wao ambao wamekuwa wakubwa. Samatta anastahili heshima kubwa nchi hii. ameamsha ndoto za vijana wengi ambao waliona kuna baadhi ya mambo hayawezekani.
 
TOP 10 WANASOKA WA KIAFRIKA WENYE MKWANJA MREFU [emoji383]
.
1. Samuel Etoo - $ 95m [emoji3591] (Sh 218.5 bilioni)
2. Didier Drogba - $90m
3. Gnegneri Yaya Toure - $ 70m
4. Emmanueli Sheyi Adebayor - $ 45M
5. Michael Esien - $ 35m
6. John Obi Mikel - $ 30m
7. Asamoah Gyan - $ 23m
8. Sadio Mane - $ 20m
9. Seydou Keita - $ 10m
10. Christopher Samba - $ 7m
.
NB: Usiseme watu hawana pesa, sema huna pesa.
 
[emoji3578][emoji3578][emoji3578] Farha Jr

KOCHA THIERRY HITIMANA, BINADAMU BORA NJE YA UWANJA

Jioni moja baada ya Ligi kuu bara kusimama kupisha mechi za kimaitaifa hizi zinazochezwa sasa! Nikipokea simu ya 'wanangu' wanaocheza Ligi Kuu niwasindikize kwenye recovery

Ilikuwa waende swimming kwenye hotel moja hapa Jijini Dar Es Salaam, ofcourse tukaongozana kwenye gari ya Mchezaji mmoja! Wachezaji wapo watatu wa Ligi kuu na Mimi wanne msela tu

Wakati 'Wanangu' hao watatu wameanza kuogelea Mimi sijazoea hayo mambo nikawa nimetulia nachezea simu, walioga kwa muda kidogo ghafla nikaitwa na Mtu nisiemfahamu

Alikuwa ni Mzungu yule tukasalimiana kwa Kiingereza kisha akaniambia wale uliofika nao ni wachezaji mpira kama sikosei! Nikajibu Ndio! Akaniambia wameoga muda mrefu sana waambie yatosha, kwa afya ya misuli kutokana na temperature ya maji

Niliporudi eneo la pool sikuwaambia kuna Mtu kasema inatosha bali nikawaambia, Wanangu tuwahini muda umeenda mimi nawahi kuandaa kipindi basi tukakubaliana tukawa tunatoka nje

Wakati tunatoka bado nikawa nazoom sura ya yule Mzee, nikahisi kama nimewahi kumuona sehemu kwenye mpira wa miguu nilihisi ni Kocha moja wapo wa Simba ila sikuwa na uhakika sana, nikaamua kupotezea

Sasa tulipofika mapokezi ghafla tunakutana na Kocha wa Simba, Thierry Hitimana akiwa ameketi anatazama mechi ya Namungo vs Kagera iliyokuwa inapigwa Ilulu mkoani Lindi

Wale wachezaji wote watatu ambao ni Wanangu wakaenda kumsalimia Mwalimu, kumbuka ni wachezaji wa timu tatu tofauti dhidi ya Kocha wa timu tofauti, Mwalimu anawafahamu vyema wakasalimiana

Nikarudi nyuma kidogo kumuuliza Mhudumu wa pale kuwa Kocha huyo anaishi pale? Akaniambia ndio bench la ufundi lote la Simba linaishi hotelini hapo, nikaunga ile picha ya nyuma kuwa ni kweli yule wa mwanzo alikuwa Kocha wa Simba pia (yule Mzungu)

Sasa Kocha Hitimana kuna sehemu alikuwa anataka kwenda lakini hapafahamu.... ITAENDELEA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…