Makapuku Forum

TETESI:

Klabu ya Simba imemalizana na nyota kutoka klabu ya Teungueth ya Senegal, Pape Ousmane Sakho mwenye umri wa miaka 24. Taratibu zote za usajili zimefikia pazuri na atajiunga na timu Morocco.

 
PAPE OUSMANE SAKHO is [emoji837]

Silaha nyingine kwenye kikosi cha Simba [emoji881]

Karibu Msimbazi fundi wa kuchezea mpira msenegali Pape Ousmane Sakho (24).

Simba Nguvu Moja
 
SIMBA YAPANGIWA KITONGA, IYOO MAKUNDI
.
Droo ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2021/2022 imeiweka Simba katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya makundi kama itachanga vyema karata zake kwenye mechi ya hatua ya awali (32 Bora)
.
Simba inaonekana kuwa na mchekea kwani itaanzia raundi ya kwanza kwa kuvaana na mshindi kati ya ya Jwaneng ya Botswana na DFC Beme ya Afrika ya Kati.
.
Simba ikishinda mechi ya raundi ya kwanza itafuzu moja kwa moja hatua ya Makundi na kuvuna kuna kiasi cha $ 550,000 (Sh bilioni 1.3)
.
 
Siphiwe Tshabalala [emoji654] Yanga [emoji352]
.
Taarifa kutoka Sauzi [emoji1221] zinaeleza kuwa klabu ya Yanga SC imewasiliana na wakala wa staa Siphiwe Tshabala ili kunasa saini yake msimu huu.
.
Yanga wanataka kuongeza wachezaji wenye uzoefu zaidi kwenye kikosi chao kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa ya CAF.
.
Inaelezwa kuwa Tshabalala kwa sasa yuko huru baada ya hivi karibuni kutemwa na klabu ya AmaZulu kwa sababu zinazotajwa kuwa ni umri mkubwa (36).
 
Baada ya kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Brentford je, Kocha wa Arsenal Mikel Arteta anastahili kupewa muda au inatosha atafutwe mwingine?

Eti mashabiki wa Arsenal mnasemaje [emoji1787][emoji1787] nyie kuna mambo yanafurahisha

Tatizo la Arsenal lipo kwa kocha? wachezaji? au Menejimenti?
 
Ofisi ya Bunge imetoa ufafanuzi kuhusu taarifa za upotoshaji zinazosambaa kwenye baadhi ya mitandao zinazodai Wabunge ambao hawatachanja chanjo ya Covid 19 hawatoruhusiwa kuingia Bungeni.

Ofisi ya Bunge imesema taarifa hizo sio za kweli na kwamba Wabunge kuchanja ni hiari.
 
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia amethibitisha kuwa vilabu vya Tanzania vitaruhusiwa kusajili wachezaji 12 kutoka nje ya Tanzania, ambapo wachezaji nane pekee ndiyo wataruhusiwa kuanza kwenye mechi moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…