Makanisa yamegeuka biashara.

Makanisa yamegeuka biashara.

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,932
Reaction score
11,849
Wachungaji wengi siku hizi hasa makanisa ya kilokole wamegeuka wapiga dili, mahubiri yao yamejaa toa ndugu toa ulinacho nacho ukienda makanisani wengi wanahubiri utoaji mwanzo hadi mwisho wa ibada wamegeuza nyumba za ibada biashara, na yule anaetoa kanisani hata kama ni mtenda dhambi mkubwa anaheshimika kuliko yule masikini anaemwabudu Mungu kwa haki hata kama hamtolei ipasavyo, ukienda kwenye 90% ya mafundisho ni toa toa toa na harambee za kila siku hubirini neno la Mungu achaneni na tamaa unajisikiaje wewe mchungaji kutembelea gari nzuri wakati muumini wako anashindia mlo mmoja tena ambao sio mlo kamili kwanini mmegeuza nyumba za Mungu vitega uchumi vyenu, mbona masheikh hawatembelei magari mazuri kama nyie wachungaji.
 
Wachungaji wengi siku hizi hasa makanisa ya kilokole wamegeuka wapiga dili, mahubiri yao yamejaa toa ndugu toa ulinacho nacho ukienda makanisani wengi wanahubiri utoaji mwanzo hadi mwisho wa ibada wamegeuza nyumba za ibada biashara, na yule anaetoa kanisani hata kama ni mtenda dhambi mkubwa anaheshimika kuliko yule masikini anaemwabudu Mungu kwa haki hata kama hamtolei ipasavyo, ukienda kwenye 90% ya mafundisho ni toa toa toa na harambee za kila siku hubirini neno la Mungu achaneni na tamaa unajisikiaje wewe mchungaji kutembelea gari nzuri wakati muumini wako anashindia mlo mmoja tena ambao sio mlo kamili kwanini mmegeuza nyumba za Mungu vitega uchumi vyenu, mbona masheikh hawatembelei magari mazuri kama nyie wachungaji.

Akili zako sio nzuri. Jana ulikoment ujumbe flan kua mada za dini zimezidi,leo unaamka na mada ya dini. Akili yako imejaa udini kama lukuvi.
 
Akili zako sio nzuri. Jana ulikoment ujumbe flan kua mada za dini zimezidi,leo unaamka na mada ya dini. Akili yako imejaa udini kama lukuvi.

Lazima tuseme ukweli ulivyo sio kila kitu ni udini mengine ni ukweli mtupu.
 
Morembe hata mimi natafuta mtaji nianzishe langu tena ni kazi rahisi sio lazima niwe mchungaji natafuta jamaa anaeweza kusema sana na kuhamasisha anakula mkataba ndio dill mjini we uko wapi bwani .
 
Morembe hata mimi natafuta mtaji nianzishe langu tena ni kazi rahisi sio lazima niwe mchungaji natafuta jamaa anaeweza kusema sana na kuhamasisha anakula mkataba ndio dill mjini we uko wapi bwani .

Mkuu ukipata eneo zuri unikumbuke kwenye ufalme wako unipe na cheo cha mhasibu wa kanisa.
 
Molembe10% ya kipato chako cha siku ambayo inajulikana kama FUNGU LA KUMI hii ni lazima umtolee Mungu!! hili si mjadala na halikwepeki.
 
Molembe10% ya kipato chako cha siku ambayo inajulikana kama FUNGU LA KUMI hii ni lazima umtolee Mungu!! hili si mjadala na halikwepeki.

Mkuu unatoa fungu la kumi unatoa sadaka lakini bado unakumbana na mchango wa kumpeleka mchungaji Israel kumnunulia mchungaji gari wakati anajua watu wake ni masikini.
 
Utoaji sio Kutapeliwa... Kutoa ni agizo la Mungu... Tatizo ni kwamba kuna baadhi ya matapeli ambao wamefikia hatua ya kujiita wachungaji na kufungua makanisa na sasa ndio wanao chafua hali halisi ya kanisa....

Hivyo jambo la msingi ni kuondoka kwenye makanisa hayo kwani hayasisitizi mtu ili akue kiroho n.k.

Tafuta kanisa lenye injili iliyo hai linalo mruhusu Roho mtakatifu kutembea na linalo kemea dhambi asilimia 100%

Huko nako hata kama hawasisitizi juu ya kutoa..
Ww uwe mwaminifu katika kutoa fungu la kumi na sadaka na dhaka,, Ukijenga imani ya kubarikiwa iliyoambatana na Utakatifu

HAKIKA UTABARIKIWA
 
Mkuu unatoa fungu la kumi unatoa sadaka lakini bado unakumbana na mchango wa kumpeleka mchungaji Israel kumnunulia mchungaji gari wakati anajua watu wake ni masikini.

Kutoa sadaka za aina mbalimbali ni maagizo ya Mungu, watumishi wanastahili kula mezani kwa Bwana. kuwahudumia watumishi ni desturi iliyojengeka kulingana na Biblia, walihudumiwa wakati wa Agano la kale pia tukiona mifano kadhaa kwenye Agano jipya. Kumwezesha mtumishi kusafiri ni jambo la kawaida likionekana kwa kujirudia kwenye Nyaraka za Paulo.
"Usije Nyumbani mwa Bwana mikono mitupu".
Salaam.
 
Kutoa sadaka za aina mbalimbali ni maagizo ya Mungu, watumishi wanastahili kula mezani kwa Bwana. kuwahudumia watumishi ni desturi iliyojengeka kulingana na Biblia, walihudumiwa wakati wa Agano la kale pia tukiona mifano kadhaa kwenye Agano jipya. Kumwezesha mtumishi kusafiri ni jambo la kawaida likionekana kwa kujirudia kwenye Nyaraka za Paulo.
"Usije Nyumbani mwa Bwana mikono mitupu".
Salaam.

Point!!
 
Back
Top Bottom