Makamu wa rais

Makamu wa rais

Sangarara

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2011
Posts
13,104
Reaction score
5,665
Hivi Kazi ya Makamu wa Rais katika nchi yetu ni nini? inawezekana hii ikana ni issue ya kuadress kwenye Katiba yetu pia? Huwa najiuliza ni kwa nini Makamu wa Rais haonekani kwenye ulingo wa kisiasa, kwa mfano ni kwa nini hatumuoni akijishughulisha na kulisimamia baraza la mawaziri kama ambavyo tunamtegemea Rais kufanya? Kwa nini simsikii japo akijifaragua kupambana na Rushwa? au basi tatizo la kuporomoka kwa kiwango cha Elimu nchini? au tatizo la Ajira? au ulinzi na usalama? au swala la kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu? au tatizo la umeme? au utoroshaji wa wanyama hai kwenda nje ya nchi? au mfumuko wa bei? au mchakato wa kuandika katiba mpya? au tatizo la vifo vya mama na watoto wakati wa kujifungua? au Malaria basi?

Au katika kipindi cha miaka miwili iliyopita ni wakati Gani Makamu wetu wa Rais alipata kuassume full presidential position?

Nauliza maswali haya kwa dhati kwa sababu nafasi hii ni ya kikatiba, na tunatumia mapesa mengi sana kuimaintain.

Chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuna wizara mbili, Wizara ya Muungano na wizara ya Mazingira, Hasa Makamu wa Rais wa sasa, mbona sijaona jitihada zake binafsi za kujishughulisha na chokochoko za Muungano hata baada ya kushambuliwa na mawimbi makubwa makubwa? au hiyo wizara ya mambo ya muungano inajishughulisha na mambo gani haswa?

Kuna wizara ya mazingira, mbona haonekani japo kwa usanii basi kushughulikia swala la uchafuzi wa mazingira unaofanywa na viwanda hapa nchini? sijawahi kumsikia akizungumzia uchafuzi wa mazingira uliosababisha athari kubwa kwa wakazi wa ny'amongo, majuzi kuna hoteli imebainika kumwaga kinyesi baharini iko oesterbay, mbona hakuweka japo neno?

Tatizo ni personality yake au ndio tatizo lile lile la CCM?

Nashukuru kwamba, baada ya post hii, kama sio coincidence
Wizara ya Mazingira iliyo chini ya ofisi ya makamu wa rais imeifungia hotel ya Double Tree Hilton kwa sababu za uchafuzi wa mazingira ya bahari ya hindi.
 
Hivi Kazi ya Makamu wa Rais katika nchi yetu ni nini? inawezekana hii ikana ni issue ya kuadress kwenye Katiba yetu pia? Huwa najiuliza ni kwa nini Makamu wa Rais haonekani kwenye ulingo wa kisiasa, kwa mfano ni kwa nini hatumuoni akijishughulisha na kulisimamia baraza la mawaziri kama ambavyo tunamtegemea Rais kufanya? Kwa nini simsikii japo akijifaragua kupambana na Rushwa? au basi tatizo la kuporomoka kwa kiwango cha Elimu nchini? au tatizo la Ajira? au ulinzi na usalama? au swala la kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu? au tatizo la umeme? au utoroshaji wa wanyama hai kwenda nje ya nchi? au mfumuko wa bei? au mchakato wa kuandika katiba mpya? au tatizo la vifo vya mama na watoto wakati wa kujifungua? au Malaria basi?

Au katika kipindi cha miaka miwili iliyopita ni wakati Gani Makamu wetu wa Rais alipata kuassume full presidential position?

Nauliza maswali haya kwa dhati kwa sababu nafasi hii ni ya kikatiba, na tunatumia mapesa mengi sana kuimaintain.

Chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuna wizara mbili, Wizara ya Muungano na wizara ya Mazingira, Hasa Makamu wa Rais wa sasa, mbona sijaona jitihada zake binafsi za kujishughulisha na chokochoko za Muungano hata baada ya kushambuliwa na mawimbi makubwa makubwa? au hiyo wizara ya mambo ya muungano inajishughulisha na mambo gani haswa?

Kuna wizara ya mazingira, mbona haonekani japo kwa usanii basi kushughulikia swala la uchafuzi wa mazingira unaofanywa na viwanda hapa nchini? sijawahi kumsikia akizungumzia uchafuzi wa mazingira uliosababisha athari kubwa kwa wakazi wa ny'amongo, majuzi kuna hoteli imebainika kumwaga kinyesi baharini iko oesterbay, mbona hakuweka japo neno?

Tatizo ni personality yake au ndio tatizo lile lile la CCM?

Kutembea na Mikasi
 
Nadhani hii nafasi iliwekwa kwa ajili ya muonekano wa muungano tu. Ila kiuhalisia ambao tunauona wananchi wa kawaida, waziri mkuu ana nguvu kuliko VP.
 
Au katika kipindi cha miaka miwili iliyopita ni wakati Gani Makamu wetu wa Rais alipata kuassume full presidential position?

Swali la msingi.

Hivi katiba inasemaje kuhusu wajibu wake kipindi Rais hayupo?

Nakumbuka ishu ya Pinda na Jairo kusema mkuu hayupo ila ingekuwa uwezo wake angemfukuza
 
Swali la msingi.

Hivi katiba inasemaje kuhusu wajibu wake kipindi Rais hayupo?

Nakumbuka ishu ya Pinda na Jairo kusema mkuu hayupo ila ingekuwa uwezo wake angemfukuza

Kama Rais hayupo yeye ndio anakuwa Rais, sasa hili mbona huwa hatulioni kwa uhalisia? kwa mfano kwenye hiyo issue ya Jairo kama president hakuwepo kwa nini hakuirefer kwa makamu wa rais?

Au hajiamini?
 
Nadhani hii nafasi iliwekwa kwa ajili ya muonekano wa muungano tu. Ila kiuhalisia ambao tunauona wananchi wa kawaida, waziri mkuu ana nguvu kuliko VP.
Inapray role gani kwenye kuimarisha Muungano?
 
its another waste of money and resources!!!!!
 
Walitaka Raisi akitoka bara, makamu anatoka visiwani na kinyume chake. Naungana na hoja kwamba hii nafasi iingaliwe kwa upya hasa majukumu ya makamu wa raisi.

Unajua ni dhihaka kubwa sana kwa watanzania kuanzisha nafasi nakuipa jina kubwa namna hiyo wakati msingi wake ni kuifanya kama kichaka cha kuwapumzishia watu wenye hasira za melengo yao ya kisiasa kuzimwa na chama chao??
 
hebu tueleze kule marekani Joe Baden ni nani? na anafanya kazi gani. nini tofauti kati ya Dr. Bilali na baden?
 
hebu tueleze kule marekani Joe Baden ni nani? na anafanya kazi gani. nini tofauti kati ya Dr. Bilali na baden?
Hilo waachie wamarekani wanajua umuhimu wa nafasi hiyo kwenye ustawi wa Taifa lao. by the way kutaka kufananisha jambo lolote kati ya Marekani na Tanzania ni kama ujuha.
 
Jamani Makamu wa Rais ni celemonial post,na kusubiri miaka 10 yao...wapate viinua mgongo vyao,wale taratibu hadi mauti yawakute!
 
This position must be questioned! Ipo kama kiraka tena bora kiraka maana mantiki yake ni kuziba tundu katika nguo. Ni bora nafasi isiwepo basi nafasi ya waziri mkuu iwe mbadala, yaani atoke upande mwingine wa muungano.
 
Is it play or pray kama kizungu hukijui bro bora changia kiswahili tuu tutafahamu
Nakiri kukosea, lakini sidhani kama nilikuwa naandika kizungu lakini? nadhani hapa mwenye mapungufu makubwa kati yangu na wewe anaeleweka kirahisi zaidi.
 
Katiba mpya ni lazima tupunguze matumizi makubwa ya serika watu hawa awana kazi yeyte; vice presda, deputy ministers their daily roles can be played by general secretary , ma dc wote, wakuu wa polisi wa wilaya, hakuna aja ya kua na mikoa mingi 2vigawe kikanda mfano kanda ya kaskazini, kanda ya ziwa, kanda ya kati , kanda pwani, nyanda za juu kusini n.k hapo 2nakua na mkuu wa mkoa wa kuchaguliwa na wananchi na cyo kuteuliwa alafu majimbo yanabaki vile vile.
 
Ni nafasi zilizo wekwa kisiasa kwa nia ya kuimaliza zanzibar kwani zamani RAIS wa Znz ndio alikuwa makamo wa Kwanza wa Rais.

nafikiri ni kitu bora kabisa kijadiliwe kwa kina sana katika katiba mpya ikiwezekana kiondoshwe kabisa kwa mustakabali wa mvungano wenu.
 
Back
Top Bottom