Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango ametoa onyo kwa baadhi ya viongozi wa umma wanaotumia madaraka yao vibaya kwa kulazimisha mahusiano ya kingono kazini, hasa kwa waandishi waendesha ofisi (makatibu mahsusi).
Dkt. Mpango alikuwa akizungumza katika mkutano wa 12 wa Chama cha Waandishi Waendesha ofisi Tanzania (TAPSEA) unaofanyika mkoani Arusha leo Mei 15, 2025.
“Wapo viongozi wanaojiita mabosi wachache wenye tabia mbaya wanatumia nafasi zao vibaya, jambo la aibu. Baadhi yao wanalazimisha penzi maofisini na waandishi waendesha ofisi. Wengine ni watu wa hovyo, sijui kwa nini bado hawajaacha kazi”. amesema Dkt. Mpango
Aidha, Dkt. Mpango ameeleza kusikitishwa na taarifa kwamba baadhi ya waandishi waendesha ofisi hunyimwa fursa au hata posho iwapo hawajakubali mahusiano yasiyofaa na viongozi wao.
“Wengine wanawanyima fursa mpaka wapewe penzi. Hata posho wanawekewa kauzibe. Haya hayakubaliki kabisa”. ameongeza Dkt. Mpango
Makamu wa Rais amewaagiza Mawaziri, Makatibu Wakuu, na viongozi wengine wa juu kutowafumbia macho watumishi wenye tabia hizo, na kuhakikisha kuwepo kwa utaratibu wa siri wa kupokea na kushughulikia malalamiko ya waandishi waendesha ofisi.
M
Dkt. Mpango alikuwa akizungumza katika mkutano wa 12 wa Chama cha Waandishi Waendesha ofisi Tanzania (TAPSEA) unaofanyika mkoani Arusha leo Mei 15, 2025.
“Wapo viongozi wanaojiita mabosi wachache wenye tabia mbaya wanatumia nafasi zao vibaya, jambo la aibu. Baadhi yao wanalazimisha penzi maofisini na waandishi waendesha ofisi. Wengine ni watu wa hovyo, sijui kwa nini bado hawajaacha kazi”. amesema Dkt. Mpango
Aidha, Dkt. Mpango ameeleza kusikitishwa na taarifa kwamba baadhi ya waandishi waendesha ofisi hunyimwa fursa au hata posho iwapo hawajakubali mahusiano yasiyofaa na viongozi wao.
“Wengine wanawanyima fursa mpaka wapewe penzi. Hata posho wanawekewa kauzibe. Haya hayakubaliki kabisa”. ameongeza Dkt. Mpango
Makamu wa Rais amewaagiza Mawaziri, Makatibu Wakuu, na viongozi wengine wa juu kutowafumbia macho watumishi wenye tabia hizo, na kuhakikisha kuwepo kwa utaratibu wa siri wa kupokea na kushughulikia malalamiko ya waandishi waendesha ofisi.