Makamu Wa Rais Akutana Na Kibanda

Makamu Wa Rais Akutana Na Kibanda

Maswali magumu majibu mepesi a morden way of living in my everloved country Tanganyika
 
Kumbe makamu wa raisi yupo, anashinda wapi?
 
ayaaaa, tayari! hakuna Kibanda tena baada ya kikao. Tusubiri mwingine tena naye ang'olewe kucha bila ganzi, tulie kidogo, tuape kidogo, tuahidi kusema kidogo, jioni ifike, tusahau.
 
Baada ya kumng'oa jicho na meno, wanampa pole sasa... hawa jamaa ni wanafiki sana...
 
Siamini Bilal kama anaweza msaidia
 
Ila kama Kibanda hataweka wazi kilichotokea maana yeye ndiye anafahamu basi hakika waandishi wa habari mtakatwa vichwa na kutolea utumbo kama kuku na hakuna wa kuwatetea. Nilitegemea solidarity ya ajabu tena nilitegemea mnefanya hata mgomo kuandika habari za polisi hadi kieleweke lakini mpo tu kila mtu anahemea tumbo na kusujudia mwanasiasa wake. Achaneni na siasa fanyeni habari za weledi.
 
ukisoma ile makala yake kwenye gazeti la mawio la wiki ya jana kaweka wazi kabisa waliomteka na kumtesa ni maaskali kwani aliwasikia wakiambizana na kuita afande huyu hapa mpige risasi. Sasa habari kama hizo si nzuri kwa serikali kwani imekuwa ikituhumiwa na wadau wa habari, wanaharakati na wananchi kuwa inahusika na matukio yanayowakuta wanahabari . Hivyo dhamira ya mkutano huo moja kwa moja ni kumtaka rai kibanda asiliongelee suala hilo na si vinginevyo.
mkuu we ndo umeongea.yuko wapi dk ulimboka mpaka leo kimyaaa.chezea serikali wewe,huyu jamaa nae ndo basi tena hatutamsikia tena akisema chochote.nachukia sana wanaharakati wa namna hii.haya ndo keshakutana na serikali tena tuone kama harakati ataziendeleza
 
Hii movie kali, kikulacho kii nguoni mwako. Haya yetu macho.
 
Siko hizi kibao kimegeuka? Wagonjwa ndio wanaotembelea badala ya kutembelewa?
Kweli kuishi kwingi kuona mengi.
 
Kibanda anajua watesi wake, kama walikuwepo askari walitumika tu, lakini watesi wake ni hao hao anaowatumikia kutengeza mikakati ya kuwachafua wapinzani wao!

Anashindwa kuwataja kwa aibu, lakini ipo siku haya yote yatakuwa peupe na ndipo mtajua Kibanda ni nani!
 
hivi wewe ni Manyerere ninayemjua au siye? siamini kama unaweza kuandika huu utumbo!

pesa ni nini? watu wanataka kujua watesaji na hatua za kuchukua ili yasitokee tena,siyo kutibiwa na serikali.
wakianzisha operation ya kuwang'oa kucha na macho kisha wanawatibisha bure utakubaliana nao?
punguza tamaa ya pesa kamanda!

Kamanda unapiga chini ya mkanda siyo? Wewe unadhani pole kavukavu inasaidia nini? Kumbuka huyu Mheshimiwa ni rafiki wa Mwenyekiti Kibanda, suala la kujua waliomwumiza linakamilishwa. Kibanda ni mtu mweledi na mwenye msimamo, ukiona kaenda ofisi kwa Makamu ujue ametafakari.
 
Kibanda is no longer the same. It pains! They have weaken one of our lieutenants!!
 
Back
Top Bottom