Makamba vs Upinzani?

Kisendi

JF-Expert Member
Jan 29, 2009
699
178
BAADA ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kushinda uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Katibu Mkuu wake, Yusuph Makamba amesema muungano wa vyama vya upinzani hauna mwelekeo sawa paka wanne waliofungwa kamba mikiani.

Makamba alitoa jana katika uwanja wa Pasua, mjini Moshi wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 32 ya chama hicho ambayo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Aman Abeid Karume.

Makamba ambaye hupenda siasa za vijembe, kama kawaida yake alisema kwa ukiwafunga paka wanne pamoja mikiani na kisha kuwawekea panya mbele yao, wote watakatika mikia kwa kila mmoja kukimbilia panya huyo.

Alisema hayo akimaanisha kuwa, muungano wa upinzani sasa umevunjika kutokana na kila chama kutaka maslahi katika uchaguzi huo.

Hata hivyo, aliwaagiza wanachama na wakereketwa wa CCM kutokubali chama chao kuhusishwa na ufisadi na kutangaza rasmi kwamba, kuanzia sasa watakula sahani moja na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

"Hoja yao kubwa sasa (Chadema), ni ufisadi, wanasema CCM mafisadi na kila tukipita na nguo zetu za kijani wanasema mafisadi haooo…Tuwaombe wanachama na wakereketwa wetu wakatae kuitwa mafisadi," alisema Makamba huku akishangiliwa.

Makamba alirejea maagizo ya Karume alipozungumza na wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM (UV-CCM) mjini Dodoma, ambako aliwataka wasihofu Operesheni Sangara iliyotangazwa na Chadema kwani wako imara kujibu mapigo.

Makamba alitumia mifano ya dini ili kuhakikisha anafikisha ujumbe wake pale alipohoji iwapo kama yeye atazini lawama zitamwendea Sheikh au Mungu?

"Hivi Yusuph Makamba akizini lawama zitapelekewa Mungu au Sheikh? Au akizini mkatoliki lawama zitaenda kwa Kadinali Pengo au Mlutheri lawama ni kwa Askofu Malasusa? Lawama atabeba aliyezini, hivyo na ufisadi usihusishwe na chama," alisisitiza na kuongeza akitoa mfano:

"Kama Mbowe anatuhumiwa kwa ufisadi, Sisi hatusemi Chadema ni mafisadi bali tutasema Mbowe na kama ni Mrema, atatuhumiwa kukwapua mabilioni akanunua nyumba, basi fisadi si TLP bali ni Mrema".

Kwa upande wake Rais Karume, alisema licha ya kuwepo kwa majimbo na kata zenye wabunge au madiwani wa upinzani, ni lazima viongozi hao wafahamu kuwa Tanzania inaongozwa na serikali zote mbili ya Muungano na ile ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ), ambazo zitahudumia majimbo yote bila kuchoka.

Alisema upinzani wa Tanzania bado haujakomaa na ni wa kupinga kila jambo jema linalofanywa na serikali ya CCM na kwamba, chama hicho hakitakoseshwa usingizi na kauli zisizo za kweli za viongozi wa vyama vya upinzani nchini.

Katika sherehe hizo zilizohudhuriwa pia na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa, Katibu Mwenezi, John Chiligati, Rais Karume alipokea wanachama wapya 1,321 waliojiunga na chama hicho na jumuiya zake.

Katika tamko lake lililosomwa na Katibu wa mkoa, Mauldine Kastico, CCM mkoa Kilimanjaro ilisema imejipanga kikamilifu na kiko makini kushinda chaguzi za serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa 2010 kwa kishindo.
Mwananchi Source: 01/02/2009
 
BAADA ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kushinda uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Katibu Mkuu wake, Yusuph Makamba amesema muungano wa vyama vya upinzani hauna mwelekeo sawa paka wanne waliofungwa kamba mikiani.

Kwa hili ni sawa kabisa; niliwahi kumsikia mwenyekiti was NCCR akionyesha jinsi alivyo negative na CHAMEMA [ndio paka hao ambo kila mmoja anahisi mwenzake anavuta mkia badala ya kugeukiana wang'ate kamba ziishe]

Makamba ambaye hupenda siasa za vijembe, kama kawaida yake alisema kwa ukiwafunga paka wanne pamoja mikiani na kisha kuwawekea panya mbele yao, wote watakatika mikia kwa kila mmoja kukimbilia panya huyo.
Ni kweli mkia ulikatika pale mbeya

Alisema hayo akimaanisha kuwa, muungano wa upinzani sasa umevunjika kutokana na kila chama kutaka maslahi katika uchaguzi huo.

Hata hivyo, aliwaagiza wanachama na wakereketwa wa CCM kutokubali chama chao kuhusishwa na ufisadi na kutangaza rasmi kwamba, kuanzia sasa watakula sahani moja na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Hapa kazi kubwa maan mswahili ukimtuma kula sahani moja utajuta

"Hoja yao kubwa sasa (Chadema), ni ufisadi, wanasema CCM mafisadi na kila tukipita na nguo zetu za kijani wanasema mafisadi haooo…Tuwaombe wanachama na wakereketwa wetu wakatae kuitwa mafisadi," alisema Makamba huku akishangiliwa.

Makamba alirejea maagizo ya Karume alipozungumza na wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM (UV-CCM) mjini Dodoma, ambako aliwataka wasihofu Operesheni Sangara iliyotangazwa na Chadema kwani wako imara kujibu mapigo.

Makamba alitumia mifano ya dini ili kuhakikisha anafikisha ujumbe wake pale alipohoji iwapo kama yeye atazini lawama zitamwendea Sheikh au Mungu?

"Hivi Yusuph Makamba akizini lawama zitapelekewa Mungu au Sheikh? Au akizini mkatoliki lawama zitaenda kwa Kadinali Pengo au Mlutheri lawama ni kwa Askofu Malasusa? Lawama atabeba aliyezini, hivyo na ufisadi usihusishwe na chama," alisisitiza na kuongeza akitoa mfano:

"Kama Mbowe anatuhumiwa kwa ufisadi, Sisi hatusemi Chadema ni mafisadi bali tutasema Mbowe na kama ni Mrema, atatuhumiwa kukwapua mabilioni akanunua nyumba, basi fisadi si TLP bali ni Mrema".


Kweli Makamba lazima umepata coaching kidogo maana utumbo umepungua, nadhani wapinzani have eyes, kwamba huyu old dog anapata new tricks

Kwa upande wake Rais Karume, alisema licha ya kuwepo kwa majimbo na kata zenye wabunge au madiwani wa upinzani, ni lazima viongozi hao wafahamu kuwa Tanzania inaongozwa na serikali zote mbili ya Muungano na ile ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ), ambazo zitahudumia majimbo yote bila kuchoka.

Mwananchi Source: 01/02/2009

Wakati wapinzani wanaumana... Babu Issa Matona kapata nafasi ya mipasho
 
Hizi ndo siasa za Tanzania bwana...Siasa za vijembe,kutukanana/kukashfiana,kulialia na kuviziana..Ujinga mtupu
 
Last edited:
Makamba afafanisha wapinzani na paka
Daniel Mjema na Ally Sonda, Moshi

BAADA ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kushinda uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Katibu Mkuu wake, Yusuph Makamba amesema muungano wa vyama vya upinzani hauna mwelekeo sawa paka wanne waliofungwa kamba mikiani.

Makamba alitoa jana katika uwanja wa Pasua, mjini Moshi wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 32 ya chama hicho ambayo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Aman Abeid Karume.

Makamba ambaye hupenda siasa za vijembe, kama kawaida yake alisema kwa ukiwafunga paka wanne pamoja mikiani na kisha kuwawekea panya mbele yao, wote watakatika mikia kwa kila mmoja kukimbilia panya huyo.

Alisema hayo akimaanisha kuwa, muungano wa upinzani sasa umevunjika kutokana na kila chama kutaka maslahi katika uchaguzi huo.

Hata hivyo, aliwaagiza wanachama na wakereketwa wa CCM kutokubali chama chao kuhusishwa na ufisadi na kutangaza rasmi kwamba, kuanzia sasa watakula sahani moja na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

"Hoja yao kubwa sasa (Chadema), ni ufisadi, wanasema CCM mafisadi na kila tukipita na nguo zetu za kijani wanasema mafisadi haooo…Tuwaombe wanachama na wakereketwa wetu wakatae kuitwa mafisadi," alisema Makamba huku akishangiliwa.

Makamba alirejea maagizo ya Karume alipozungumza na wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM (UV-CCM) mjini Dodoma, ambako aliwataka wasihofu Operesheni Sangara iliyotangazwa na Chadema kwani wako imara kujibu mapigo.

Makamba alitumia mifano ya dini ili kuhakikisha anafikisha ujumbe wake pale alipohoji iwapo kama yeye atazini lawama zitamwendea Sheikh au Mungu?

"Hivi Yusuph Makamba akizini lawama zitapelekewa Mungu au Sheikh? Au akizini mkatoliki lawama zitaenda kwa Kadinali Pengo au Mlutheri lawama ni kwa Askofu Malasusa? Lawama atabeba aliyezini, hivyo na ufisadi usihusishwe na chama," alisisitiza na kuongeza akitoa mfano:

"Kama Mbowe anatuhumiwa kwa ufisadi, Sisi hatusemi Chadema ni mafisadi bali tutasema Mbowe na kama ni Mrema, atatuhumiwa kukwapua mabilioni akanunua nyumba, basi fisadi si TLP bali ni Mrema".

Kwa upande wake Rais Karume, alisema licha ya kuwepo kwa majimbo na kata zenye wabunge au madiwani wa upinzani, ni lazima viongozi hao wafahamu kuwa Tanzania inaongozwa na serikali zote mbili ya Muungano na ile ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ), ambazo zitahudumia majimbo yote bila kuchoka.

Alisema upinzani wa Tanzania bado haujakomaa na ni wa kupinga kila jambo jema linalofanywa na serikali ya CCM na kwamba, chama hicho hakitakoseshwa usingizi na kauli zisizo za kweli za viongozi wa vyama vya upinzani nchini.

Katika sherehe hizo zilizohudhuriwa pia na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa, Katibu Mwenezi, John Chiligati, Rais Karume alipokea wanachama wapya 1,321 waliojiunga na chama hicho na jumuiya zake.

Katika tamko lake lililosomwa na Katibu wa mkoa, Mauldine Kastico, CCM mkoa Kilimanjaro ilisema imejipanga kikamilifu na kiko makini kushinda chaguzi za serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa 2010 kwa kishindo.

HUo ndio mtazamo wa Makamba na nadhani pia ni wa wa-CCM wote. Kama wapinzani bado hawajakomaa kuungana kuna haja gani ya kuandaa muswada ambao utawezesha vyama kuungana na kusimamisha mgombea mmoja wa urasi?

Naomba kuwasilisha hoja.
 
Hizo akili za kizee za Makamba ,sasa yeye hafahamu kuwa serikali imeundwa na Chama Chake mbona hatuoni hatua za kichama kuchukuliwa dhidi yao? Na huyo shehe au padire asipokemea nae huunganishwa pamoja na yeye aliozini katika hukumu za kidini sasa kama ni gurupu limezini hivyo lote huchanganywa na kiongozi wao ambae ni msimamizi asiewachukulia hatua wala kuwataja kwa majina wale wenziwe hivyo hata Makamba ni fisadi kwani amewakumbatia mafisadi kwenye Chama chake.
Viongozi ni lazima wawe waadilifu si kwa waiba kuku na mananasi bali hata hao mafisadi,wavueni Ubunge ili tujue hampo genge moja.
Na kama kiti cha uraisi au ubunge au chochote kile ni panya basi na wao wataingia katika kundi la Paka ila watakuwa wagonjwa ndio maana hawakufungwa kwa kuunganishwa mikia na kama si wagonjwa basi watakuwa...!
 
Huyu Makamba si material ya Sec. general na wakiendelea naye atakigarimu chama chake (Kama Dito enzi zile Dar).
 
Mimi chichemi kitu. Mambo ya Ngoswe namwachia Ngoswe. Haaa....subiri.... ninekumbuka kitu... ngoja nicheme: Jamani Watanzania heeee , Pale Serikali ya CCM inapofanya mazuri hebu kwapamoja....tu-appreciate.....tuwapigie makofi tafadhali....LAKINI pale INAPOBORONGA...SOTE kwa kauli moja tuikemee kwa jina la YESU na Mitume wengine kwa mujibu wa imani ya dini zetu. Tuwakemee mpaka wajirekebishe.....hata hivyo tumaendeleo wametufanya...tofauti na jinsi ilivyokuwa wakati wa mfumo wa chama kimoja.....Siku hizi CCM inajituma jamani...Hila waongeze kasi la sivyo tutawaovetake kwenye tuta.....mbele kwa mbele....
 
JE WAPINZANI MPO NA HII MINENO YA MAKAMBA?? Je ni kweli WATZ WOTE NI MBUMBU MAANA CCM
Sijaona sehemu yoyote ambayo Mh. Makamba amesema kuhusu umbumbu...! Si ajabu umbumbu huu ukawa ni wa mleta mada hii
 
Crazy as* Makamba again!! Where is his brain??, pole pole but we will get there, Rome was not built in a day! Down with the green guyz.
 
Japhet,
Anachojaribu kusema Makamba ni kwamba pale serikali ya Kikwete inapofanya mazuri tumsifie yeye Kikwete au mtu aliyefanikisha na sio CCM..kwa hiyo utaona wapi tunapingana naye..
Usemi wa Makamba unapotosha wananchi kiasi kwamba sifa kama hizi zitawarudia wananchi wenyewe watenda kazi na sidhani kama tunaweza kwenda popote ikiwa tutaanza kuhukumu watu ambao wanafuata maazimio ya chama husika. Kikwete akiboronga kutokana na maazimio ya CCM tutasema ubovu wa CCM, Mafisadi ni hawahawa viongozi wa CCM ambao chama kimeshindwa kuwakemea kwa sababu labda wanayoyafanya ni within their policies inapofikia kuwakinga viongozi..
Chama ni chombo cha usafiri na viongozi wake ni manahodha hivyo ktk kuzungumzia sifa na athari sidhani kama huyu Makamba unaelewa majukumu ya vyombo hivi..
Watu wakisema Bus lile bovu halifai kusafiri nalo inajumuisha chombo chenyewe na wahusika wake hata kama sababu ni dereva au utingo..
 
Wakuu,

Kuna mtu amesema kuwa huyu Makamba siyo "material" ya Secretary General.
Mimi nasema, "utaijua tabia ya mtu, ukiiangalia tabia ya watu anaotembea nao."

Kwa mfano huo, utaijua CCM ilivyo, ukimwangalia Secretary General wake. CCM haiwezi kuepuka kuitwa Chama cha Mafisadi kwa kuwaangalia Mafisadi ambao ni wanachama wanaotokana na chama hicho.

Halafu CCM haiwezi kuepuka kuitwa Chama cha Mafisadi, ukikiangalia chama hicho kinavyowakumbatia na kuwalinda wanachama wake hao Mafisadi.

Actions speak louder:

Inasemwa kuwa "nyani halioni mando lake." CCM kila mara inalalamika kuwa wapinzani hawana sera bali matusi tu katika mikutano yao. Hapo hapo wanapolalamikia matusi ya wapinzani, wanajisahau, wanasema, wapinzani ni paka waliofungwa mikia.

Majibu ya wapinzani yatakuaje? Si watasema CCM wezi wa EPA au wametumia pesa za wizi za EPA kushinda uchaguzi au mengine makubwa zaidi?
 
Hizi ndo siasa za Tanzania bwana...Siasa za vijembe,kutukanana/kukashfiana,kulialia na kuviziana..Ujinga mtupu
 
Mimi si mwana siasa na wala si mwana chama wa chama chochote cha siasa. Makamba haelewi kwanini Watanzania wanasema na kuimba kwamba CCM ni Mafisadi. Katiba ya CCM inakumbatia na kuwalinda Mafisadi, na pia inawatukuza mafisadi. Mkapa ni mwizi nambari one lakini kupelekwa mahakamani CCM wanasema ana kinga inamlinda. CCM walichota mapesa ya EPA kwa ajili ya uchaguzi sasa kwanini watanzania wasiwaite mafisadi?.
Makamba amepitwa na wakati na ubishi usio na shule ndani yake, anafanya mambo kama mzee jongo ama jangala. Penye ukweli Makamba anatafuta vijembe vya kiswahili ambavyo havina kichwa wala miguu.

CCM haina mpya, imeishiwa ni bora ikae pembeni mapema kulinda heshima yake. Watanzania wameichoka CCM kila dalili inaonekana wasingoje mpaka watu wabebe mapanga na mawe kuwafukuza kama wezi.
 
Mods

sasa naona mnafisadisha mpaka threads... ile ya subuhi changanyeni na this one... aaarrgghhhh
 
MBUNGE wa Moshi Mjini (Chadema) Phillemon Ndesamburo amemjia juu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Luteni Yusuph Makamba baada ya kutaka mbunge huyo, ang’olewe katika jimbo hilo.


Akizungumza na Mwananchi jana kwa njia ya Simu, kutoka bungeni Dodoma, Ndesamburo alisema Luteni Makamba hana ubavu wa kuwashawishi wakazi wa Moshi wamg’oe katika uchaguzi wa mwaka 2010, kwa kuwa wananchi wana imani naye.


Ndesamburo amelazimika kutoa majibu hayo baada ya Makamba na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Visiwani, Aman Abeid Karume kutoa kauli kuwa Ndesamburo aanze kujiandaa kuliacha la Jimbo hilo, kwa kuwa CCM wameweka mikakati kabambe ya kumg’oa katika uchaguzi ujao.



Makamba alitoa kauli hiyo juzi kwenye sherehe za uzinduzi wa miaka 32 ya CCM ambazo kitaifa zilifanyika kwenye kiwanja cha Shule ya msingi Mandela mjini Moshi.



Ndesamburo alisema Makamba hajui nguvu na uwezo wake kisiasa na kwamba endapo anataka kujua, waende kumuuliza aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM taifa na Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa ambaye kwa kushirikiana na mke wake, Anna Mkapa, mwaka 2000 walimsaidia mgombea Ubunge wa CCM ashinde lakini aliambulia patupu.



"Makamba anaeleza wananchi kuwa nikae mkao wa kuondoka, ataondoka yeye kwenye ukatibu wa CCM, mimi Ubunge hadi mwaka 2015, kama hajui nguvu yangu akamuulize Mkapa na Mama Anna nilivyowashughulikia, mimi nina watu jamani,"alitamba Ndesamburo.



Akimzungumzia Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Visiwani, Karume ambaye aliunga mkono kauli ya Makamba, alisema anamuheshimu sana Rais huyo na hapendi kulumbana naye.



Mbunge huyo, alimtaka Karume amalize matatizo yanayoikumba Tanzania Visiwani na kuligeukia jimbo la Moshi ambalo wananchi wake wanaishi kwa kupendana na kuheshimiana.



"Mimi namuheshimu sana Rais Karume, sipendi kumvunjia heshima yule kijana, sura yake inaonesha ni mtu muungwana sana, namuomba aniachie Makamba ili niweze kumshughulikia, Makamba ni saizi yangu,Tarime aliondoka usiku na gari, Moshi ataondoka usiku na Pikipiki,"alisema Ndesamburo.



Ndesamburo alisema kutokana na shughuli mbalimbali za maendeleo alizowafanyia wakazi wa Moshi Mjini, mwaka kesho ana uhakika wa kushinda tena Ubunge na kwamba kipindi hicho, kitakuwa cha mwisho, lakini akatamba kuwa bado Chadema itaendelea kuwa na Mbunge katika jimbo hilo.


Source: Gazeti la Mwananchi
 
Ndugu Ndesamburo usipoteze muda kubishana na chizi. Makamba hajui asemalo, afunguapo mdomo ni lazima aseme tena bila kufikiri. Hakuna co-ordination kati ya mdomo na ubongo.
 
Nigefurahi sana kama angempa ukweli kidogo Mh Karume kwamba yule ni accidental president ambaye hakupendwa na chama chake na hata ikulu ameingia kwa kuwaibia kura CUF mara 2. Kwa hiyo ushauri wa kumwambia akamalize matatizo ya Zanzibar ni kupoteza muda kwa kuwa hana uwezo huo. Yeye ni mtumishi wa wale waliompa urais. Wakitaka hao matatizo ya Zanzibar yanaisha kesho.
 
Mbunge wa Chadema amshambulia katibu mkuu CCM
Ally Sonda,Moshi

CCM MDANGANYE SHEMU ZINGINE SI MOSHI AU KWA WACHAGA TUMEELIMKA SI KAMA MAKABILA MENGINE?????? 2010 mtakiona cha moto

MBUNGE wa Moshi Mjini (Chadema) Phillemon Ndesamburo amemjia juu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Luteni Yusuph Makamba baada ya kutaka mbunge huyo, ang’olewe katika jimbo hilo.

Akizungumza na Mwananchi jana kwa njia ya Simu, kutoka bungeni Dodoma, Ndesamburo alisema Luteni Makamba hana ubavu wa kuwashawishi wakazi wa Moshi wamg’oe katika uchaguzi wa mwaka 2010, kwa kuwa wananchi wana imani naye.

Ndesamburo amelazimika kutoa majibu hayo baada ya Makamba na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Visiwani, Aman Abeid Karume kutoa kauli kuwa Ndesamburo aanze kujiandaa kuliacha la Jimbo hilo, kwa kuwa CCM wameweka mikakati kabambe ya kumg’oa katika uchaguzi ujao.



Makamba alitoa kauli hiyo juzi kwenye sherehe za uzinduzi wa miaka 32 ya CCM ambazo kitaifa zilifanyika kwenye kiwanja cha Shule ya msingi Mandela mjini Moshi.



Ndesamburo alisema Makamba hajui nguvu na uwezo wake kisiasa na kwamba endapo anataka kujua, waende kumuuliza aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM taifa na Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa ambaye kwa kushirikiana na mke wake, Anna Mkapa, mwaka 2000 walimsaidia mgombea Ubunge wa CCM ashinde lakini aliambulia patupu.



"Makamba anaeleza wananchi kuwa nikae mkao wa kuondoka, ataondoka yeye kwenye ukatibu wa CCM, mimi Ubunge hadi mwaka 2015, kama hajui nguvu yangu akamuulize Mkapa na Mama Anna nilivyowashughulikia, mimi nina watu jamani,"alitamba Ndesamburo.



Akimzungumzia Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Visiwani, Karume ambaye aliunga mkono kauli ya Makamba, alisema anamuheshimu sana Rais huyo na hapendi kulumbana naye.



Mbunge huyo, alimtaka Karume amalize matatizo yanayoikumba Tanzania Visiwani na kuligeukia jimbo la Moshi ambalo wananchi wake wanaishi kwa kupendana na kuheshimiana.



"Mimi namuheshimu sana Rais Karume, sipendi kumvunjia heshima yule kijana, sura yake inaonesha ni mtu muungwana sana, namuomba aniachie Makamba ili niweze kumshughulikia, Makamba ni saizi yangu,Tarime aliondoka usiku na gari, Moshi ataondoka usiku na Pikipiki,"alisema Ndesamburo.



Ndesamburo alisema kutokana na shughuli mbalimbali za maendeleo alizowafanyia wakazi wa Moshi Mjini, mwaka kesho ana uhakika wa kushinda tena Ubunge na kwamba kipindi hicho, kitakuwa cha mwisho, lakini akatamba kuwa bado Chadema itaendelea kuwa na Mbunge katika jimbo hilo.
 
Back
Top Bottom