Filipo
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 9,342
- 5,536
Makamba amewaambia wanachama wa ccm maneno hayo wakati akiwaaga baada ya kuondolewa kwenye nafasi ya ukatibu mkuu wa chama hicho jana. Mimi ni m1 kati ya watu waliofadhaishwa sana na kuondoka kwa mzee huyu. Amefanya mambo mengi sana yaliyosaidia kukijenga chama chetu! Ni chini ya uongozi wake chama chetu kimetata ushindi mkubwa katika uchaguzi uliopita. Kashfa za ufisadi, Upuuzi wake na mamluki (akina Tambwe) wake ndani ya chama ilisaidia kukipukutisha chama hicho na kuimarisha chetu na nilitamani aendelee kuwepo hadi 2015 ili aendelee "kukijenga" chama chetu. Nimefadhaishwa sana.