Makamba ataka TTCL ichunguzwe na CAG

Makamba ataka TTCL ichunguzwe na CAG

mgomba101

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2011
Posts
1,822
Reaction score
711
Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknoloji, January Makamba, ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuichunguza Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL).

Makamba alitoa agizo hilo jana baada ya kukutana na wafanyakazi wa kampuni hiyo ambao waliwasilisha matatizo, changamoto na kuwataja hadharani watu wanaoihujumu kampuni hiyo ikiwemo menejimenti.

Alisema endapo yaliyosemwa na wafanyakazi yatabainika kuwa ni ya kweli, hatua za kisheria zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kuwaburuza mahakamani.

"Hawa ni wa kufungwa pingu si wa kuwalea, ni lazima wawajibishwe kama ni kweli kuna watu wanaihujumu kampuni kwa kiasi hiki na mimi taarifa nilikuwa nazipata siku nyingi na wafanyakazi waliniomba nikutane nao ili wanielezee shida zao," alisema.

Aliongeza kuwa kutokana na mazingira yaliyopo kwa sasa katika kampuni hiyo hatoshangaa kuona kwamba bodi inakataa kupitisha uamuzi wa kufanyiwa ukaguzi ndani ya kampuni hiyo.

Aidha alisema kuwa anatarajia kuvunja uongozi mzima wa kampuni hiyo na kuweka mpya huku akielezea pia uchunguzi utakaofanyika utategemeana na maamuzi ya bodi ambayo atakutana nayo keshokutwa.

Awali wafanyakazi wakiwakilishwa na Lucas Ishengoma, walisema walikusanya sh bilioni 79.9 katika ofisi ya Dar es Salaam, Mkoa wa Kusini, lakini sh bilioni tatu hazikuonekana na kwamba zimetafunwa na wajanja.

"Kila mwezi tunafanya majumuisho na tulipata sh bilioni 7.9 Dar es Salaam, Mkoa wa Kusini, tulipotaka kujua fedha ziko wapi uongozi ukawa unatisha watu kuhamishwa na kuwabambikia kesi. Hii ni hatari waziri, ingilia kati," alisema.

Alisema wanataka kubadilishiwa meneja wao Karim Babhia kupelekwa Mkoa wa Mwanza kutokana na kuhoji fedha zilipokwenda, kitendo alichoeleza kuwa ni cha unyonyaji.
 
management TTCL ni hatari kwa taifa ili mh Makamba wafanyakazi TTCL wana imani na wewe naamini hutawaangusha
 
Januari Makamba alikuwa wapi siku zote hizi?? Tangu ateuliwe Unaibu Waziri wa Mawasiliano pamoja na Waziri wake Mbarawa ni hawasikiki wala hawaonekani ni kimya kabisa kana kwamba hawapo!!. Tulishasema muda mrefu kuwa TTCL inahitaji ukaguzi wa CAG maana kuna ubadhrifu wa kutisha!!Kuna mabilioni ya Shilingi yanatafunwa na kunufaisha wachache ilhali Kampuni ilizidi kuporomoka.

Kuna kikundi ndani ya Manejiment ya TTCL kimeifanya kampuni kama mali yao binafsi. TTCL ilitakiwa iwe chini ya Waziri mwenye dhamana kama Mwakyembe. Kwamba yale anayoyafanya TPA(Mamlaka ya Bandari) yanatakiwa yafanyike ndani ya TTCL.

Tunaomba Makamba na Waziri wake Mbarawa wafanye kweli ndani ya TTCL. Kama hawajui la kufanya basi wakatafute ushauri kwa Waziri Mwakyembe ili awape mikakati ya jinsi ya kushughulikia matatizo ndani ya TTCL.
 
Na majibu ya kisisiasa. Uchunguzi ukimamikilika, na kama kweli utafanyika, utasikia hadithi nyingine. TTCL in bodi pamoja na mahesabu yake kukaguliwa, Je siku sote hizi walikuwa hawaoni. Ikiwa kuna baadhi ya vigogo wa CCM wakikutwa wamo si mambo yataishia hapo.
 
kuchunguzwa sawa na vodacom ya dada yako ichukuliwe hatua kwa pia kwa kusambaza sms za chuki na ubaguzi wakati wa uchaguzi wa 2010
 
ivi kwann mawasiliano na uchukuzi isiwe wizara moja chini ya Mwakyembe ili aifagie TTCL na awabane mbavu mashirika ya simu?
 
Kuna hitajika Waziri kama Mwakyembe ambae ni mtendaji na si mwanasiasa zaidi, Prof Mbawala aliongea na wafanyakazi siku nyingi na kuelezwa hayo matatizo lakini mpaka sasa hajachukua hatua zozote kama alivyoahidi matokeo yake anaongelea mambo ya Airtel kwenye vikao vyao badala ya TTCL, yaani siasa bwana we acha tu, viongozi wengi ni siasa tu na hawatendi wanachomaanisha
 
Serikali hii hii ya ccmasalia ndio imeua ttcl

Hatua ya huyu dogo ni pre-emptive, hujuma zinazofanywa na simu za mkononi hasa Airtel na Voda ni kubwa. Historia ya Airtel ilivyoanza kama Celtel inadhihirisha. Makambas ni wafaidika wa hujuma hizi, sasa unategemea nini? Kuteuliwa kwa huyu dogo ni muendelezo wa mradi huu wa kifamilia. Suburini tu wenye uchungu na nchi hii washike madaraka, wanadhani hawafahamiki.
 
Januari Makamba alikuwa wapi siku zote hizi?? Tangu ateuliwe Unaibu Waziri wa Mawasiliano pamoja na Waziri wake Mbarawa ni hawasikiki wala hawaonekani ni kimya kabisa kana kwamba hawapo!!. Tulishasema muda mrefu kuwa TTCL inahitaji ukaguzi wa CAG maana kuna ubadhrifu wa kutisha!!Kuna mabilioni ya Shilingi yanatafunwa na kunufaisha wachache ilhali Kampuni ilizidi kuporomoka.

Kuna kikundi ndani ya Manejiment ya TTCL kimeifanya kampuni kama mali yao binafsi. TTCL ilitakiwa iwe chini ya Waziri mwenye dhamana kama Mwakyembe. Kwamba yale anayoyafanya TPA(Mamlaka ya Bandari) yanatakiwa yafanyike ndani ya TTCL.

Tunaomba Makamba na Waziri wake Mbarawa wafanye kweli ndani ya TTCL. Kama hawajui la kufanya basi wakatafute ushauri kwa Waziri Mwakyembe ili awape mikakati ya jinsi ya kushughulikia matatizo ndani ya TTCL.
Nadhani umshukuru kwa kuwa at last amefikia na kuahidi kulishugulikia. Kuna mawaziri wanasubiri salary slip tu hutakaa kuwasikia wakishugulikia jambo lolote mfano Sophia Simba. JM anastahili kupongezwa na sio kubezwa, ila kasi yake haitoshi
 
Top manag yote ni wabadhilifu wachunguzwe watimuliwe na kupelekwa mahakamani ili kuinusuru ttcl
 
Hapo TTCL Top Managers ni Mizee tena inaamini sana MaCCM ya magogoni.Kuna zee Moja Linaitwa Shaibu Makande Jinsi Kishenzi.
 
hapo ttcl top managers ni mizee tena inaamini sana maccm ya magogoni.kuna zee moja linaitwa shaibu makande jinsi kishenzi.

dawa yao ipo jikoni........kupiga chini mizee yote inayofanya kazi kwa mazoea na kuweka 'mchechu' type..mziki wake lazima waritae
 
management TTCL ni hatari kwa taifa ili mh Makamba wafanyakazi TTCL wana imani na wewe naamini hutawaangusha

Corporate governance hapa nchini ni ovyo kabisa na hii inatokana na ujinga wa kila kitu na mtu kuteuliwa na rais, na muda mrefu naona Mtendaji mkuu wa TTCL somebody ISSA anakaimu kwa muda mrefu nafikri hata miaka 10 inafika, je huoni utawala bora?. ni ujinga tu.TTCL inauwezo wa kukusanya fedha za kufa mtu kwa kutoa huduma chache kama vile Data telecommunication tu kwa makampuni mbali na voice lakini ulaji na strategizing ni ovyo.Je Msajili wa Hazina anafanya nini kama kampuni haikaguliwi na wakaguzi wa ndani na wa nje ?.
 
huyu dogo hajui alifanyalo ,anataka aone nini humo wakati celtel ilianza na rasilimali za ttcl huku ikijibadili majina kila kukicha .
 
Mkamba hana lolote la msingi na hawezi kufanya anochosema. Huyu jamaa ni mzuri wa kujibu hoja na kutoa alternatives lakini hawezi kusimamia.

Nakumbuka swala la TCRA an mitandao ya simu kuhusu gharama za muda wa maongezi. Pia kwa nchi za wenzetu, wizara kama hii ndo inapelekewa makachero wa kimarekani. Ni sehemu za kuibua vipaji vya kisayansi na sera za kufanya nchi ijitegemee siyo kukusanya maduhuri kama Tanzania. Ukisikia Irani, Israel, India, China, S. Africa, Singapore, Korea ya Kusini n.k. unaongelea nguvu ya wizara kama hii.

Hebu, tuache Tanzania. Kila mtu anaangalia aende wapi ili apate posho.

 
Ni aibu sana...Kashfa baada ya kashfa..tangu ubinafsishaji...malumbano ya hisa kati ya serikali na Wawekezakaji na hatimaye serikali kurudishiwa TTCL mifupa na wawezekezaji kuichukua Celtel kijumla..Saskatel as managing Operators na kutukuwa na mikakati au kuidhoofisha makusudi ili private operators wasambae nchini kuizidi TTCL ni mkakati mbovu unaolitafuna hili shirika kwa sasa! Kwa hio kila mwenye nafasi anachukua chake mapema.Some "Devils are made by the government".. Good luck CAG.. Its is never late to tackle anything but time is running out!!
 
Back
Top Bottom