njundelekajo
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 310
- 227
Engelbert Kiondo, bila shaka umesoma sheria na katika sheria imeainisha kazi halali na kazi isiyo halali. Tunaposema kazi halali inayompa mtu kipato ukahaba si kazi halali japo unampa mtu kipato lakini si kazi halali, Afande kazi hii wanawake hawa wanaifanya si kwa lengo la ora kwa Kila Mtanzania" tuliyoahidiwa lakini nadhani hata muasisi wa "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" hawezi kuungana na wewe kuhusu hili. Tusiendelee kulea maovu kiasi hiki. Nyie Polisi mmekuwa mkiwaua raia je hili liko kwenye katiba? Najua utasema Polisi huwa wanajihami, je raia wakijihami mbona mnasema haiko katika katiba. Samahani ingekuwa Ndugu yako wa karibu kabisa katika zoezi lenu la kuwaondoa machangudoa ukakutana na ndugu yako wa damu ungemwambia dada endelea katiba inakuruhusu.
Una maana gani unaposema zoezi hilo la Kenyela haliko kwenye katiba kwa hiyo ni hahali kuendelea kufanyika???. Ningekuwa IGP ningekuvua vyeo vyako, maana wenzio wanakemea maovu wewe unahubiri maovu.
yaaaankwa wino mwekundu kabisaaaa,,,,yumekuelewa