Muuza unga fuatilia kwa makini
Watabisha mpaka kunakucha.... they don't know what's going on behind this fake pastor...
Muuza unga fuatilia kwa makini
Hahahhahaa! Mbona huna jipya avoid repetition! Kiburi cha uzima kinakusumbua, while hujui one second ahead utakuwa kwenye hali gani!! Utanyooka tu utakapoanza kuvuna matunda ya mdomo wako! kuhusu wanangu...nimeshawaandalia kabla hata ya kuwapata! wewe fedha zako kazana kuzipeleka kwenye madanguro na vilabu vya gongo...mavuna yapo. napenda sana andiko lisemalo 'kila mtu atavuna alichopanda' yan sio hadi ufe..hapahapa duniani! mwanaume mzima kazi kushadadia umbea, na wanawake tufanyaje sasa! aibu zako!
Pale kwa Gwajima wakizidi sana ni waumini 2000.....
Kama Gwajima anajaza watu 70000 basi uwanja mpya wa Taifa unaingiza watu million 100...
Wanabodi,
Kama ni kweli Ngwajima ana waumini wasiopungua elfu sabini na wanaenda kanisani mara mbili kwa wiki basi Ngwajima anaingiza zaidi ya bilioni tatu kwa mwaka (makadirio ya chini kabisa)
NI HIVI:
Tufanye kila muumini wake hutoa sadaka ya sh. 500 tu-hiyo ni flat rate, ina include waliotoa elfu kumi, waliotoa sh mia na wasio toa kabisa.
Hivyo basi kwa siku moja kwa waumini 70,000 wakitoa sh 500 ni sawa na sh milioni 35. Kwa wiki wanaenda mara mbili hivyo ni sawa na sh milioni 70.
Kama kwa wiki anaingiza milioni 70, je kwa mwezi anaingiza kiasi gani? Uki cross multiplication utapata milioni 280
Kama kwa mwezi anaingiza milioni 280, je kwa mwaka anaingiza kiasi gani? uki cross tena multiplication utapata bilioni 3 na milioni 360. Sasa piga hesabu kwa miaka yote aliyotoa huduma ameingiza sh ngapi?
Kwa mantiki hiyo pesa aliyonunulia Hummer aliipata ndani ya mwezi mmoja tu.
Achilia mbali fungu la kumi na pesa mbali mbali anazopewa kama zawadi, hapo tumepiga hesabu ya sadaka tu.
NAMALIZIA, Biblia inasema "vya madhabahuni vitaliwa na wamadhabahuni" full stop.
Posted by: MCHUNGUZI HURU (Associate Professor)
hao maaskofu wengine walipewa uaskofu na nani? si na binadamu!? tena kwa taratibu zilizowekwa na binadamu. yaan kulikuwa na wa kwanza aliyeanzisha hiyo kitu! Mungu hajawahi kushuka akampa mtu uaskofu, ni taratibu za duniani. au kwa kuwa unakosali taratibu zilianzishwa na wazungu zamani kabla hujazaliwa ndo unaona big deal!! halafu pia, wewe huko kwa hao wanaolawiti vitoto vinavyotumikia kanisani unakosali...hutoagi sadaka? so unaliwa? maana kama kutoa sadaka kila muumini wa popote hutoa sadaka anaposali, lakini walokole kwa kuwa tunasali makanisa ambayo viongozi wake wa juu ni wa-TZ wenzetu ndo mnaona tunaliwa? nyie kwa kuwa waanzilishi ni wazungu tena msiowajua ndo hamliwi?? kuna nini kwenye kichwa chako? ni ubongo kweli??
mmmmmmh nianzishe kanisa na mm thikubaliii
Ukifahamu kama kuna kuingiza ujue kuna na kutoa vile vile. Mimi niko kwenye kamati ya kanisa lililoko mjini, makusanyo ya sadaka ni kidogo sana ukilinganisha na matumizi - mishahara, umeme, ulinzi, vifaa vya ibada mara si mara moja matumizi ya kawaida kugharamiwa na michango ya maendeleo kama harambee za ujenzi.
Mleta mada vile vile ukumbuke wale wanaomzunguka Gwajima na suti zao nao wana familia zao zinazohitaji kuhudumiwa vizuri na hizo hizo sadaka
Sijawahi kuona kanisa linalochukua idadi kubwa ya waumini inayofikia elfu ishirini hapa nchini achilia mbali elfu Sabin. Labda kanisa la TB Joshua huko Nigeria
Mtoa mada jaribu kutuletea zinazotumika baa,kasino,gesti ,night club na sehemu kama hizo ili watu waumie wamrudie Mungu.Wewe mtu katoa sadaka kanisani wala hajalazimishwa wewe inakuhusu nn.Kwanza watoaji wenyewe Wakristo wanajua siri ya kumtolea Mungu.Uliwaona wanaomtolea Mungu wamefilisika?Au lengo lako hasa nn?Mbona Ibrahim alimtoa mwanae sembuse pesa.
Watu wanaacha kupga mahesabu ya TRA jinsi yanavoliwa na maCCM mnakuja na vijihesabu vya kataasis ambako hata hakatugusi wengine, acheni majungu nyiny, lete hesabu zenye maslahi mapana ya nchi bwana mnaboa sana
Hata 20000 bado ni hypothetical....Msitake kudanganya watu, idadi ya watu elfu 70 sio mchezo. tazama tuu uwanja wa taifa wakitoka uwanjani barabara zote zinajaa, hakuna nafasi. na hao ni 60,000. ije kuwa hao wawili hapo kwa gwajima.? yaani kama wengi sana ni 20,000 sio zaidi. na data zipo sahihi kabisa.
Hata 20000 bado ni hypothetical....
Pale kwa Gwajima wakizidi sana ni watu 2000..