Makada nguli wa CCM wahamia CHADEMA

Makada nguli wa CCM wahamia CHADEMA

One two

Member
Joined
May 27, 2013
Posts
95
Reaction score
36
Mwendelezo wa kampeni za kijiji kwa kijiji bado zina zidi kushika kasi ndani ya mbeya vijijini ambapo leo katika kata ya BONDE LA SONGWE kijiji cha IKUMBI wakina mama maalufu na wanachama mashuhuri wa chama cha mapinduzi wamehamia CHADEMA, Wakina mama hao wamakamo ya kutosha wamesema wamesha choshwa na uongo wa ccm katika ahadi zake, pia wamedai kutolidhishwa na jinsi ajira zilivo tolewa katika kiwanja kipya cha ndege cha songwe kwani hata nafasi za wafagizi hawajachukuliwa watoto wao ambao ni wazawa kama walivo ahidiwa.

Pia wamewatupia lawama za kutosha mwenye kiti wa kiji hicho kwa titeti ya ccm na diwani wa katata AMONI MWAKAPALAhiyo kwa jinsi walivo jigawia mbolea za luzuku na kuwaacha wanachi kwenye mataa, pia wanachi wakafika mbali na kukiomba radhi CHADEMA kwa makosa waliyo fanya 2010 kwani walimchagua diwani AMONI MWAKAPALA ambaye anajihusisha na maswala ya kijambazi katika kata ya BONDE LA SONGWE NA VIJIJI VYAKE wameapa kutofanya kosa kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa mpaka uchaguzi mkuu.








 
Hii ni habari njema
Ila CHADEMA vijijini bado
tunawaombeni mlifikirie hili jambo hata kama tatizo ni pesa mtuambie tuchangie
tunahitaji mabadiliko
 
M4C inapenya kimya kimya huko vijijini ambako ndiko ngome kuu ya CCM. Hakuna kijiji kitakachoachwa. Mtaji wa chama ni wanachama wake. CCM itajikuta bila wanachama wa kutosha 2015. Hata hizo kura za maoni hazitatosha. Wataitisha Mkutano Mkuu wa Dharura kubadilisha katiba yao kupunguza vigezo vya idadi ya wanachama watakaopiga kura za maoni. Suala ni: Zitatosha? Yaani itakuwaje mgombea achaguliwe na watu chini ya 10?
 
Ndo wakati wa kujitambua sasa na kuchukua maamuzi ya kweli na thabiti
 
Chadema wakaze buti, wakipenya hadi vijijini hata kwa nusu tu watakuwa wamelamba dume! Ccm kura wanachukulia vijijini kama waliweka! Ambako hakuna huduma za jamii. Mfano vijiji vingi vya mbinga mkoani ruvuma bado havijapitiwa na m4c!
 
Hivi hizi harakati ni kwamba zinakosa wahamasishaji au vipi? Mpaka leo bado kuna watu wanahama tu?
 
Back
Top Bottom