Makada CCM wakata rufaa ubunge wa Lema

Makada CCM wakata rufaa ubunge wa Lema

Ndallo nimependa sana maoni yako!


Hawa jamaa wanaotaka kukata rufaa inatakiwa wafungwe na baada ya kifungo wachapwe viboko kumi na viwili siku wakitoka wakawaadisie wake zao na mabwana zao na bila kusahau kumlipa fidia Lema!
 
Last edited by a moderator:
wanatakiwa kulipa mil 250 gharama zote za mpaka rufaa wakishindwa tena hii zinapanda nafikiri itakuwa mil 350 watashangaa
 
Maripota wetu wanapaswa kupigwa msasa kidogo wa "court reporting", kesi inazo hatua tatu muhimu, hatua ya kwanza ni kufungunguliwa kwa shauri na kusikilizwa hadi kutolewa hukumu, hatua ya pili ni ama utelelezwaji wa hukumu ama kukatwa rufaa!, hatua ya tatu ni kusikilizwa kwa rufaa na hukumu ya rufaa!, kesi ikishafika kwenye rufaa kama ilivyo hiyo kesi ya Lema, auamuzi wa rufaa ni final, yaani ni uamuzi wa mwisho!, kesi imemalizika!.

Kinachoendelea sasa, ni huyo wakili njaa, kuwadanganya hao wateja wake kuwa bado anaweza kufanya kitu ili aendelee tuu kuvuta mshiko kuendelea kuishi, au anaomba review ili kufanya dilly dallying ya delay tactics kuchelewesha hao masikini wa Mungu kulipa gharama za kesi!. Mleta shauri anapokuwa hajaridhika na uamuzi wa rufaa, usually that is the end!, hawezi kukataa rufaa anapoomba review, yaani mapitio, hii sio kukata rufaa, bali ni kuiomba mahakama rufaa kufanya consideration tuu!. Kwa kifupi hiyo ni wastage of time kwao wenyewe tuu kujipotezea muda kwa sababu kwenye review, Lema wala wakili wake hawaitwi kuulizwa chochote!. Kusema ukweli kwenye katiba mpya iwekwe kuwa wakili anapowadanganya wateja wake ili kuvuta tuu mshiko, huku anaelewa wazi hakuna kitu, awe anastahili adhabu ya kulipishwa fidia ya wastage of time and money ya wananchi masikini.

Kwa mfumo wetu wa haki Tanzania, hao majaji watatu ndio full bench yetu so far, japo full bench ya ukweli ni majaji 5!, Tanzania unaweza tuu ukaomba court review kwenye issues tatu za prerogative orders ambazo ni mandamus, prohibition na certiorari (samahani hazina majina rasmi ya Kiswahili) na sio rufaa kuikatia rufaa tena!.
Pasco.
 
Kwa sisi tunaoamini kwenye miujiza, ninaamini, unawezekana ukafanyika muujiza CCM wakaweza wakabahatisha kusimamisha mgombea na wakabahatisha kusinda jimbo la Ohi, US but si Arusha! Wasahau! o
Wafungwe tu, wana faida gani hao?
 
chakupewa ni noma sana, ukipewa nyama, usitegemee wakuletee na tooth pick, else wamekuheshimu, sasa hao vilaza wakajitaftie njiti wajichokonoe ili mambo yao yasonge
 
hivi ni viashiria vya kufa kwa ccm.
Waomba hukumu ya Mahakama ya
Rufaa ipitiwe upya


Makada watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliopinga ubunge wa Mbunge
wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema na kufanikiwa kumvua ubunge
kabla ya Mahakama ya Rufaa kumrejesha wadhifa wake, wamewasilisha maombi
ya kutaka hukumu ya mahakama hiyo ipitiwe upya.

Kwa mujibu wa
taarifa za kimahakama, makada hao waliwasilisha maombi yao Februari 13,
mwaka huu chini ya hati ya dharura wakitaka yasikilizwe
haraka.


Desemba 21, mwaka
jana Mahakama ya Rufaa ilimrejesha tena Lema bungeni baada ya kukubali
rufaa yake dhidi ya hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha iliyomvua
ubunge wake.


Makada hao
waliolalamikia ushindi wa Lema wakiwa ni wapigakura wa Jimbo la Arusha
Mjini, wanadai kuwa na sababu sita za kutaka mahakama hiyo ipitie uamuzi
wake kwa madai kuwa kuna maeneo ambayo hayakuamuliwa vizuri. Jana
NIPASHE ilizungumza na Wakili wa Lema, Method Kimomogoro, ambaye
alithibitisha kuwa na taarifa za maombi hayo na kuahidi kutoa ufafanuzi
baadaye.


Naye wakili wa
wanachama wa CCM, Alute Mughway, jana alithibitisha kuwa wateja wake
wamewasilisha maombi hayo Mahakama ya
Rufaa.


Wanachama hao wa
CCM, ambao ni Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel, walifungua
kesi dhidi ya Lema katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, kupinga ushindi
wake alioupata katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka
2010.


Walikuwa wakidai
kuwa katika kampeni zake, Lema alikuwa akitumia lugha za matusi, kejeli
na ubaguzi wa kijinsia dhidi ya aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk. Batilda
Buriani.


Kufuatia kesi
hiyo, Lema alivuliwa ubunge na mahakama hiyo, Aprili 5, mwaka huu,
katika hukumu iliyotolewa na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga,
Gabriel Rwakibarila, aliyesikiliza kesi hiyo. Jaji Rwakibarila
aliisikiliza kesi hiyo baada ya Jaji Aloyce Mujulizi aliyekuwa
amepangiwa kuisikiliza kesi hiyo kujitoa kufuatia ombi la Lema kuwa
hakuwa na imani naye.


Hata hivyo,
baadaye mwishoni mwa mwaka jana, Lema kupitia mawakili wake, Kimomogoro
na Tundu Lissu, alikata rufaa kupinga hukumu hiyo iliyomvua ubunge
wake.


Hukumu ya
kumrejeshea ubunge Lema ilitolewa na jopo la majaji watatu wa Mahakama
ya Rufaa, wakiongozwa na Nathalia Kimaro. Wengine ni Salum Massati na
Bernard Luanda.
 
very hopeless!ni lazima tukubali kuwa lema ni moto wa tipper pale Arusha.Majaji watatu waionee CCM kweli?hapana haki ilitendeka waendelee na mambo mengine
 
Hapa wtu wanakwepa kulipa ghara za kesi. Hukumu inawataka wamlipe Lemma naona kwao nakuwa rahisi zaidi kukata rufaa nyingine na kesi itakaa huko hadi uchaguzi ujao na pengine kusahaulika.
 
Hukumu iliagiza kuwa mtu asiyehusika haruhusiwi kukata rufaa. Anayetakiwa kukata rufaa ni Batilda sio hao wasiokuwa na kazi za kufanya. Maoni yangu Mahakama iwape sharti kwamba walipe kwanza ile fedha wanayotakiwa kumlipa Lema na gharama za kesi kwanza.

Safi sana mkuu..hili liwe ndio sharti. Hawa jamaa wanaendelea kutumia rasilimali zetu vibaya, majaji wenyewe wana kesi kibao watu wanataka hukumu zao, watu wa Arusha wamenyimwa haki yao ya kutumikiwa na mbunge wao kipenzi kwa miezi kadhaa.

Hivi hawa watu hawafikirii hata maslahi mapana katika jambo hili?
 
Back
Top Bottom