Makabila makubwa vs Makabila madogo

Makabila makubwa vs Makabila madogo

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,623
Reaction score
164,679
Wadau,kuna hii idea isiyo rasimi na wala si ya kikatiba kwamba, makabila fulani fulani makubwa hapa nchini, ni hatari kuingia Ikulu na ni bora makabila haya madogo madogo.

Now,lets be realistic.Is this true?

Or, in other words,does this idea still hold so far?
 
Wadau,kuna hii idea isiyo rasimi na wala si ya kikatiba kwamba, makabila fulani fulani makubwa hapa nchini, ni hatari kuingia Ikulu na ni bora makabila haya madogo madogo.

Now,lets be realistic.Is this true?

Or, in other words,does this idea still hold so far?

That was just the paranoia of our early post-independence leadership!
BUT, ALAS!, SOME PEOPLE STILL JUSTIFY THOSE FEARS EVEN TODAY!
JUST MAKE A RESEARCH IN ANY OFFICE WHERE THE BOSS IS FROM SOME WELL KNOWN TRIBES AND SEE THE PERCENTAGE OF SUBORDINATES FROM THE TRIBE!
 
Wewe mtoa mada.... Kigali is that way ------------------------>

Naona Intarahamwe wengine bado hawajarudishwa kwao
 
zilikuwa ni baadhi ya fikra mgando za nyerere hzo. Mtu hapimwi kwa kabila lake bali uwezo wake kiutendaji
 
MTU kweli hapimwi Kwa kabila alilotoka au alilozaliwa. Kwani hakuna anayepanga kuzaliwa kabisa Fulani inatokea out of his will. Katika sifa za uongozi kabila si moja ya sifa. Sifa ni uzalendo, uadilifu, ubunifu, elimu, uzoefu, upendo,uwazi ongeza na sifa zingine za kikatiba. Na kama hoja ya kwamba kabila dogo ndiyo bora basi taifa hili lingekuwa mbali sana kimaendeleo kwani waliongoza wote ni kutoka kabila dogo . yaani wazanaki,wakwere,wamakua na mndengereko.
 
Ni kweli. Vipi na kabila dogo kama wa kwe.re sijui kwale mbona ametokea mmoja halafu ni mpigaji hatari?? Au anafidia na vizazi vyote vilivyopita? Huyu jamaa ilitakiwa asiugue tezi dume ilitakiwa apate stroke kabisa.
 
hatutamchagua kwa kabila .hatutamkataa kwa kabila:Nyerere hayo mengine uzushi unaotokana na ubinafsi na ubaguzi.Makabila yanayobaguliwa ni wanyachusa,wasukuma ,wachaga,wahaya.na wanyamwezi.Jambo la kushangaza hawa wasiotakiwa ndio wenye kura nyingi.maana yake wanaruhusiwa kupigia wengine kura ila hawaruhusiwi kugombea uongozi
 
Mleta uzi kajivunjia heshima. Porojo za mtaani za miaka mingi unazileta hapa jukwaani? Hebu kua mkuu.
Ova
 
zilikuwa ni baadhi ya fikra mgando za nyerere hzo. Mtu hapimwi kwa kabila lake bali uwezo wake kiutendaji
Hazikuwa fikra mgando mkuu! Kwa wakati ule zilikuwa na mantiki kweli, ila kwasasa nadhani hazina maana tena ukiangalia jinsi nchi ilivyojichanganya.
 
Wakwere ni kabila dogo sana. Huyo ambaye leo ni Rais kafanya nini la maana kwa miaka hii inayoelekea kumi? Wala sijui vision yake iliyomsukuma kuutaka urais ilikuwa ni nini? Labda kama ni ufisadi basi kafanikisha. Nothing else...
 
Wadau,kuna hii idea isiyo rasimi na wala si ya kikatiba kwamba, makabila fulani fulani makubwa hapa nchini, ni hatari kuingia Ikulu na ni bora makabila haya madogo madogo.

Now,lets be realistic.Is this true?

Or, in other words,does this idea still hold so far?
Mkuu Kitini cha Mshahara, hili nimewahi kulizungumza hapa Sumu ya Siasa za Udini, Ukanda na Ukabila, "Is It Real?

Wanabodi,
Wanabodi nauliza, hii sumu ya siasa za ukabila na ukanda are they real au ni dhana tuu?!.

Jee Watanzania hawana makabila yao?, Lazima tukubali tukatae, Tanzania kuna dorminant tribes na makabila madogo madogo. Kati ya hizi dorminant tribes lazima tukubali kuna baadhi yake wana ukabila wa kutisha!, kuna baadhi yake wana nyodo za ajabu!, kwani iliwahi kutamkwa au kuandikwa popote kuwa watu wamakabila fulani sio hawafai kuchukua urais wa nchi hii, bali hawawezi kupewa kwa sababu matokeo tunayajua!, hivi tuu walivyo na hizo nafasi kubwa kubwa tayari ni miungu watu, wakiukwaa urais si ndio wataota pembe kabisa!. Ni general unwritten public opinion kuwa rais wa nchi hii asitokee kwenye hizi dorminant tribes!. Kuna wagombea fulani walinyimwa kura maeneo fulani kwa kuitwa wakuja!. Kuna mikoa fulani mgombea ambaye sio mzawa huitwa "chasaka" na wanakuambia kabila letu kamwe haliwezi kumchagua "chasaka"!. Jee hii ni dhana tuu ya ukabila au ndio ukweli wenyewe?.

Jee mbegu hii ya sumu kaipanda nani?, jee tunaweza kuipiga vita kwa kuikanusha tuu (denial) au tunatakiwa kuubali ukweli mchungu na kukabiliana nao (facing the problem)!.

Nauliza tuu?

Pasco
 
MTU kweli hapimwi Kwa kabila alilotoka au alilozaliwa. Kwani hakuna anayepanga kuzaliwa kabisa Fulani inatokea out of his will. Katika sifa za uongozi kabila si moja ya sifa. Sifa ni uzalendo, uadilifu, ubunifu, elimu, uzoefu, upendo,uwazi ongeza na sifa zingine za kikatiba. Na kama hoja ya kwamba kabila dogo ndiyo bora basi taifa hili lingekuwa mbali sana kimaendeleo kwani waliongoza wote ni kutoka kabila dogo . yaani wazanaki,wakwere,wamakua na mndengereko.

Mwinyi mndgereko?
 
Mleta uzi kajivunjia heshima. Porojo za mtaani za miaka mingi unazileta hapa jukwaani? Hebu kua mkuu.
Ova


Mkuu Kitini cha Mshahara, hili nimewahi kulizungumza hapa Sumu ya Siasa za Udini, Ukanda na Ukabila, "Is It Real?


sasa boss wako lowasa anatumia makanisa nalo unapinga..


Udini sio kuwa tayari kuchangia au kuchangia maendeleo ya kanisa au msikiti tena kwa wazi na sio kwa siri kama zile za Escrow kwa Askofu Kilaini.

Udini ni kuhimiza au kuwezesha vikundi vya dini fulani ili kupambana na dini nyingine kisiasa.

Kuhamasisha michango ya wazi ni kujenga uzalendo na kuondoa utegemezi toka nje ambao unaweza kuja na ugaidi na ushoga kwa taasisi za dini.
 
Back
Top Bottom