MAJIRA: NCCR waibomoa CHADEMA

MAJIRA: NCCR waibomoa CHADEMA

the horse

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2011
Posts
652
Reaction score
442
Chama Cha NCCR-Mageuzi, juzi kimeuteka mji wa Kahama, mkoani Shinyanga na kufanikiwa kuzoa wanachama wapya 220 kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wanachama hao walijiunga na Chama hicho katika mkutano wa hadhara ambao ni mwendelezo wa operesheni ya "Uzalendo amka Kahama" uliofanyika katika Kata za Basoka na Mwendakulima.

Operesheni hiyo imelenga kuwazindua wakazi wa kahama wajue misingi ya kudai haki zao bila kupoteza uhai wao, kujihadhari na baadhi ya wanasiasa ambao wako tayari kusababisha machafuko ili wafanikishe malengo yao.

Akihutubia Mkutano huo, katibu wa Habari na Uenezi wa Chama hicho Taifa, Kitengo cha Vijana, Bw.Deogratius Kisandu aliwataka vijana wasikubali kutumika kisiasa kwa manufaa ya vyama bali watangulize masilahi ya Taifa.

Alisema wanachama hao kutoka CHADEMA, waliamua kukihama chama hicho kutokana na mwenendo usioridhisha ambapo kati ya wanachama hao 98 wametokea katika Kata hizo ambapo 122 wametokea Mjini Kahama.
 
Mh!!! Haya bana kama ni kweli. Sasa unapigana na nduguyo badala ya adui. Sasa hapa tukisema mtu katumwa inakuwa unakosea kweli?
 
WALEWALE NA MBINU NI ZILEZILE: Watabeba sana hizo kadi na kuwakabidhi watu ili warudishe katika mikutano yao kwa malengo ya kujikuza kisiasa. Wakati huo CHADEMA wanaendelea kujikita katika mioyo ya watanzania. MBONA KITAELEWEKA 2015.
 
Kwa hiyo NCCR wanawataka kuwakomboa watanzania kutoka kwa nani? au sielewi maana ya ukombozi?

Je hiyo kata wanachama ni CHADEMA tu hakuna vyama vingine?
 
Nilikuwa sijui kwamba NCCR ni wapinzani wa CHADEMA na siyo CCM!! Siku zote nadhani malengo ya chama cha upinzani ni kupambana na chama tawala ili kushika dola, kumbe wenzetu malengo yao ni kuibomoa CHADEMA!!
 
sambamba na mkakati wa CCM wa kujaribu kuwachafua, kuwachonganisha na kuwadhalilisha viongozi waandamizi wa CHADEMA na wanachama wake kupitia magazeti na mitandao mbalimbali ya kijaamii, pia wameamua kuyatumia baadhi ya magazeti na mitandao ya kijamii kuuaminisha umma wa WATANZANIA kuwa CHADEMA sio chama makini bali NCCR-MAGEUZI.
HUU NI MPANGO ULIYOSUKWA ILI TU KUJARIBU KUWAYUMBISHA WATANZANIA, ILI KUIPUNGUZIA NGUVU CHADEMA, na ndio maana kila uchao ni habari za NCCR kuvuna wanachama wapya , tena wote ni kutoka CHADEMA.......TAFAKARI!
 
Tukisema mmeolewa na masisiem mnang'aka kwa hiyo leo chadema imekuwa chama kikuu na wapinzani ni nccr,kafu(mke wa masisiem)na wengineo!!!Ukombozi upo karibu makamanda tusonge mbele!!!
 
Chama Cha NCCR-Mageuzi, juzi kimeuteka mji wa Kahama, mkoani Shinyanga na kufanikiwa kuzoa wanachama wapya 220 kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wanachama hao walijiunga na Chama hicho katika mkutano wa hadhara ambao ni mwendelezo wa operesheni ya "Uzalendo amka Kahama" uliofanyika katika Kata za Basoka na Mwendakulima.Operesheni hiyo imelenga kuwazindua wakazi wa kahama wajue misingi ya kudai haki zao bila kupoteza uhai wao, kujihadhari na baadhi ya wanasiasa ambao wako tayari kusababisha machafuko ili wafanikishe malengo yao.Akihutubia Mkutano huo, katibu wa Habari na Uenezi wa Chama hicho Taifa, Kitengo cha Vijana, Bw.Deogratius Kisandu aliwataka vijana wasikubali kutumika kisiasa kwa manufaa ya vyama bali watangulize masilahi ya Taifa.Alisema wanachama hao kutoka CHADEMA, waliamua kukihama chama hicho kutokana na mwenendo usioridhisha ambapo kati ya wanachama hao 98 wametokea katika Kata hizo ambapo 122 wametokea Mjini Kahama.
Mbona ule mkutano tulikuwa na coverage nao humu jamvini na watu waliohudhuria hawakufika 50 picha ziko humuhumu,vinginevyo labda kama wamejiunga kwa e mail na SMS ila kwenye mkutano palikuwa blank
 
Unauhakika wote ni CDM siyo CUF. Hakika maajabu mengine saba ya dunia sisimizi kumkanyaga TEMBO na tembo kauawa
 
Huu ni usanii tu!mi sie mwanachama wa chama chochote niko Kahama,nikionacho mimi ni vijana wengi wamewapuuza sana na hasa kwa viele wanajua agenda yao ya kupunguza kasi ya upinzani hususan kutoka CDM!Na iwapo vijana wengi hapa wangekuwa na access na jukwaa hili ungeamini haya ninayoandika.Ukuta wa Yeriko utaanguka tu!Sisi hatuna kadi lakini tunaombea demokrasia,uhuru, haki na uwajibikaji makini serikalini na hatimaye kwa raia wote.Wapiganiao yote hayo ndio chaguo letu!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Chama Cha NCCR-Mageuzi, juzi kimeuteka mji wa Kahama, mkoani Shinyanga na kufanikiwa kuzoa wanachama wapya 220 kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wanachama hao walijiunga na Chama hicho katika mkutano wa hadhara ambao ni mwendelezo wa operesheni ya "Uzalendo amka Kahama" uliofanyika katika Kata za Basoka na Mwendakulima.Operesheni hiyo imelenga kuwazindua wakazi wa kahama wajue misingi ya kudai haki zao bila kupoteza uhai wao, kujihadhari na baadhi ya wanasiasa ambao wako tayari kusababisha machafuko ili wafanikishe malengo yao.Akihutubia Mkutano huo, katibu wa Habari na Uenezi wa Chama hicho Taifa, Kitengo cha Vijana, Bw.Deogratius Kisandu aliwataka vijana wasikubali kutumika kisiasa kwa manufaa ya vyama bali watangulize masilahi ya Taifa.Alisema wanachama hao kutoka CHADEMA, waliamua kukihama chama hicho kutokana na mwenendo usioridhisha ambapo kati ya wanachama hao 98 wametokea katika Kata hizo ambapo 122 wametokea Mjini Kahama.

hii ni kuthibitisha watanzania wote wameikubali chadema,kila chama cha siasa kikiwemo ccm(magamba) wanahangaika kutafuta wanachama wapya ambao tayari ni chadema ,big up m4c somo limeanza kuelewa.
 
Back
Top Bottom