Majibu yangu kwa Mohamed Said dhidi ya habari za Chifu David Kidaha

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,273
Nimelazimika kujibu uzi wa mzee wangu na mwalimu wangu katika historia bwana Mohamed Said katika uzi wake huu Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Ndani ya uzi huo anasema kuwa "nafasi ya president wa TANU nafasi ile ilikuwa ya Chief Kidaha Makwaia lakini alikataa ndipo bahati ikamuangukia Julius Nyerere"

Mimi nimeamua kumjibu kwa kutumia andiko, Sura ya Pili, ukurasa wa 207 katika Kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, kinaeleza kwa undani suala hili, nanukuu kama ifuatavyo:

"Mkataba wa Versailles ulianzisha aina mpya ya maeneo yaliyowahi kuwa ama koloni au majimbo ya nchi zilizoshindwa katika vita. Koloni zote za Ujerumani pamoja na sehemu kubwa ya majimbo ya Milki ya Osmani ya awali ziliwekwa chini ya mamlaka ya Shirikisho la Mataifa na kukabidhiwa kwa nchi washindi wa vita. Zilipewa hali ya pekee kama maeneo ya kudhaminiwa. Tofauti na koloni za kawaida nchi wadhamini hazikupewa mamlaka yote jinsi iliyokuwa katika koloni zao za kawaida bali zilipokea maeneo ya kudhaminiwa chini ya masharti fulani pamoja na kulinda haki kadhaa za wenyeji na KUZIANDAA nchi hizi kwa uhuru.

Hapo mwanzoni tofauti kati ya koloni na eneo la kudhaminiwa haikuwa kubwa lakini baadaye masharti ya udhamini yalikuwa muhimu. Kwa mfano hali ya Tanganyika kuwa eneo ka kudhaminiwa ilisababisha Uingereza kutokukubali walowezi wengi kuja Tanganyika. Vivyo hivyo hali ya Afrika ya Kusini Magharibi kuwa eneo la kudhaminiwa ilizuia sehemu hii kuwa jimbo la Afrika Kusini na kuwa msingi kwa uhuru wake kama nchi ya Namibia.

Jukumu la kuandaa nchi hizo kupata uhuru kwa sehemu kubwa liliratibiwa na shirika la kijasusi la kanisa Katoliki la Jesuiti kwa ustadi mkubwa bila baadhi ya makoloni kujua, lakini lilikumbana na kikinza kutoka katika shirika la kijasusi la Fabian Sociaty lililokuwa linamilikiwa na Umalkia wa Kiingereza ambalo nalo lilikuwa na jukumu la kuratibu uhuru wa Afrika katika makoloni ya Uingereza, mgogoro huo ulikuzwa kwakuwa Anglikana nao tayari walikuwa wameanza kumuandaa Chifu David Kidaha Makwaia kukabidhiwa uhuru na kuwa rais wa kwanza Tanganyika, maandalizi yote yakiratibiwa kupitia taasisi yao ya Fabian Sociaty iliyokuwa maalumu kwaajili ya kuwaandaa vijana wa kiafrika kukabidhiwa nchi zao.

Barani Afrika Jesuiti ilibadili mbinu kwakuwa dola la Kiingereza lilikuwa kikwazo kwa sehemu fulani, haikujikita kwenye dola isipokuwa ilisimama katika muundo wa shirika likifanya shughuli zake ndani ya Kanisa. Dhamiri ilikuwa lazima itimie, kama ilivyosemwna huko mwanzo kuwa hawa ndio wabobevu wa elimu ya juu kwa kila nyanja na ndio wanaotawala ulimwengu, hivyo vikwazo havikukwamisha wao kufikia malengo. Mwisho Malkia wa Uingereza aliamua kuungana tu na Jesuiti ili Julius Nyerere apewe nchi.

Katika Tanganyika chini ya Udhamini wa Jumuiko la Kimataifa, kulikuwa na harakati za hapa na pale za kudai haki za kiraia kwa wenyeji. Ifahamike kuwa vyama vya harakati hizo Tanganyika vilikuwa vingi sana, na vipo vilivyokuwa vikipingana vyenyewe kwa vyenyewe.
Mwaka 1927 hadi 1929 kanisa Katoliki nchini chini Joseph Gabriel Zelger, lilibainika kuingiza siasa katika utendaji kazi zake, kitendo hiki kiliwakwaza wakuu wa mamlaka ya kikoloni na kupelekea majasusi wakikoloni wapendekeze aachishwe uongozi wa kanisa nchini. Ni kweli tarehe 12 februari 1929 Zelger alistaafu wadhifawake kwa lazima. Ni mwaka huohuo wa 1927 ndio Chama cha African Assosiotion (AA) kilianzishwa na Gavana Sir David Cameron maaluma kwaajili ya kuratibu sherehe za watu weusi huko pembeni ya mji huko mtaa wa Stanley (leo Lumumba) na kuwapa ofisi mahali leo wanapojiita TANU ilizaliwa.

Lakini historia ya Tanganyika haiwataji waasisi wa AA, Rais wa kwanza Mwalimu Cesil Matola (msomi wa mwanzo kabisa enzi za mjerumani kutoka kabila la Wayao), katibu mkuu wa kwanza Klest Sykes (Mzulu Baba yake alikuwa mateka wa kikoloni toka Afrika Kusini), Mwekahazina Ali Ramadhan (mzaramo na mvuvi maarufu wa pwani la Azania).

Hao ndio mwaka 1927 waliounda Chama cha kwanza kabisa cha kutetea maslahi ya weusi Tanganyika na shughuli zake zilikuwa ni kuratibu sherehe za waafrika tu. (Chama cha walevi kwa lugha nyingine). Mwaka 1933 Mwalimu Cesil Matola alifariki na nafasi yake ikakaimiwa na katibu mkuu wa chama hicho bwana Klest, mpaka ilipofika mwaka 1948 yakatokea mapinduzi yaliyoongozwa na mtoto wa Klest aliyeitwa Abdulwahid Sykes huyu alikuwa ametoka kupigana vita vya pili vya dunia huko Burma, na aliporudi alikuwa na mawazo ya ujana toka vitani, akampindua baba yake kwa kumpiga ngumi puani, mapinduzi yaliyoitwa “ondoa wazee”.

Kisha AA ikabadilishwa jina na kuitwa TAA, Rais wake wa Kwanza akawa Dr Vedasto Kyaruzi (Mhaya), huyu ndie dakitari wa binadamu wa kwanza kabisa wa kiafrika Tanganyika, Katibu mkuu akawa Abdulwahid Sykes na Mweka hazina akawa Dosa Azizi, utawala huo ulienda mpaka mwaka 1953 uchaguzi ulipofanyika na Nyerere akashinda pale kwenye ukumbi wa Anautoglo Mnazimoja leo, mwaka 1954 Nyerere akabadili jina la chama na kuwa TANU jina ambalo lilibuniwa na Abdulwahid Sykes, TANU ilikwenda mpaka mwaka 1977 na kisha kikazaliwa chama kiitwacho CCM baada ya Muungano wa ASP na TANU".

Dowload hapa chini sasa..
Amazon.com: Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi (Afrikaans Edition) eBook: YERICKO NYERERE: Kindle Store

IMG_20160601_143231.jpg
 
Nimelazimika kujibu uzi wa mzee wangu na mwalimu wangu katika historia bwana Mohamed Said katika uzi wake huu Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Ndani ya uzi huo anasema kuwa "nafasi ya president wa TANU nafasi ile ilikuwa ya Chief Kidaha Makwaia lakini alikataa ndipo bahati ikamuangukia Julius Nyerere"

Mimi nimeamua kumjibu kwa kutumia andiko, Sura ya Pili, ukurasa wa 207 katika Kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, kinaeleza kwa undani suala hili, nanukuu kama ifuatavyo:

"Mkataba wa Versailles ulianzisha aina mpya ya maeneo yaliyowahi kuwa ama koloni au majimbo ya nchi zilizoshindwa katika vita. Koloni zote za Ujerumani pamoja na sehemu kubwa ya majimbo ya Milki ya Osmani ya awali ziliwekwa chini ya mamlaka ya Shirikisho la Mataifa na kukabidhiwa kwa nchi washindi wa vita. Zilipewa hali ya pekee kama maeneo ya kudhaminiwa. Tofauti na koloni za kawaida nchi wadhamini hazikupewa mamlaka yote jinsi iliyokuwa katika koloni zao za kawaida bali zilipokea maeneo ya kudhaminiwa chini ya masharti fulani pamoja na kulinda haki kadhaa za wenyeji na KUZIANDAA nchi hizi kwa uhuru. Hapo mwanzoni tofauti kati ya koloni na eneo la kudhaminiwa haikuwa kubwa lakini baadaye masharti ya udhamini yalikuwa muhimu. Kwa mfano hali ya Tanganyika kuwa eneo ka kudhaminiwa ilisababisha Uingereza kutokukubali walowezi wengi kuja Tanganyika. Vivyo hivyo hali ya Afrika ya Kusini Magharibi kuwa eneo la kudhaminiwa ilizuia sehemu hii kuwa jimbo la Afrika Kusini na kuwa msingi kwa uhuru wake kama nchi ya Namibia.

Jukumu la kuandaa nchi hizo kupata uhuru kwa sehemu kubwa liliratibiwa na shirika la kijasusi la kanisa Katoliki la Jesuiti kwa ustadi mkubwa bila baadhi ya makoloni kujua, lakini lilikumbana na kikinza kutoka katika shirika la kijasusi la Fabian Sociaty lililokuwa linamilikiwa na Umalkia wa Kiingereza ambalo nalo lilikuwa na jukumu la kuratibu uhuru wa Afrika katika makoloni ya Uingereza, mgogoro huo ulikuzwa kwakuwa Anglikana nao tayari walikuwa wameanza kumuandaa Chifu David Kidaha Makwaia kukabidhiwa uhuru na kuwa rais wa kwanza Tanganyika, maandalizi yote yakiratibiwa kupitia taasisi yao ya Fabian Sociaty iliyokuwa maalumu kwaajili ya kuwaandaa vijana wa kiafrika kukabidhiwa nchi zao.

Barani Afrika Jesuiti ilibadili mbinu kwakuwa dola la Kiingereza lilikuwa kikwazo kwa sehemu fulani, haikujikita kwenye dola isipokuwa ilisimama katika muundo wa shirika likifanya shughuli zake ndani ya Kanisa. Dhamiri ilikuwa lazima itimie, kama ilivyosemwna huko mwanzo kuwa hawa ndio wabobevu wa elimu ya juu kwa kila nyanja na ndio wanaotawala ulimwengu, hivyo vikwazo havikukwamisha wao kufikia malengo. Mwisho Malkia wa Uingereza aliamua kuungana tu na Jesuiti ili Julius Nyerere apewe nchi.

Katika Tanganyika chini ya Udhamini wa Jumuiko la Kimataifa, kulikuwa na harakati za hapa na pale za kudai haki za kiraia kwa wenyeji. Ifahamike kuwa vyama vya harakati hizo Tanganyika vilikuwa vingi sana, na vipo vilivyokuwa vikipingana vyenyewe kwa vyenyewe.
Mwaka 1927 hadi 1929 kanisa Katoliki nchini chini Joseph Gabriel Zelger, lilibainika kuingiza siasa katika utendaji kazi zake, kitendo hiki kiliwakwaza wakuu wa mamlaka ya kikoloni na kupelekea majasusi wakikoloni wapendekeze aachishwe uongozi wa kanisa nchini. Ni kweli tarehe 12 februari 1929 Zelger alistaafu wadhifawake kwa lazima. Ni mwaka huohuo wa 1927 ndio Chama cha African Assosiotion (AA) kilianzishwa na Gavana Sir David Cameron maaluma kwaajili ya kuratibu sherehe za watu weusi huko pembeni ya mji huko mtaa wa Stanley (leo Lumumba) na kuwapa ofisi mahali leo wanapojiita TANU ilizaliwa. Lakini historia ya Tanganyika haiwataji waasisi wa AA, Rais wa kwanza Mwalimu Cesil Matola (msomi wa mwanzo kabisa enzi za mjerumani kutoka kabila la Wayao), katibu mkuu wa kwanza Klest Sykes (Mzulu Baba yake alikuwa mateka wa kikoloni toka Afrika Kusini), Mwekahazina Ali Ramadhan (mzaramo na mvuvi maarufu wa pwani la Azania).
Hao ndio mwaka 1927 waliounda Chama cha kwanza kabisa cha kutetea maslahi ya weusi Tanganyika na shughuli zake zilikuwa ni kuratibu sherehe za waafrika tu. (Chama cha walevi kwa lugha nyingine). Mwaka 1933 Mwalimu Cesil Matola alifariki na nafasi yake ikakaimiwa na katibu mkuu wa chama hicho bwana Klest, mpaka ilipofika mwaka 1948 yakatokea mapinduzi yaliyoongozwa na mtoto wa Klest aliyeitwa Abdulwahid Sykes huyu alikuwa ametoka kupigana vita vya pili vya dunia huko Burma, na aliporudi alikuwa na mawazo ya ujana toka vitani, akampindua baba yake kwa kumpiga ngumi puani, mapinduzi yaliyoitwa “ondoa wazee”. Kisha AA ikabadilishwa jina na kuitwa TAA, Rais wake wa Kwanza akawa Dr Vedasto Kyaruzi (Mhaya), huyu ndie dakitari wa binadamu wa kwanza kabisa wa kiafrika Tanganyika, Katibu mkuu akawa Abdulwahid Sykes na Mweka hazina akawa Dosa Azizi, utawala huo ulienda mpaka mwaka 1953 uchaguzi ulipofanyika na Nyerere akashinda pale kwenye ukumbi wa Anautoglo Mnazimoja leo, mwaka 1954 Nyerere akabadili jina la chama na kuwa TANU jina ambalo lilibuniwa na Abdulwahid Sykes, TANU ilikwenda mpaka mwaka 1977 na kisha kikazaliwa chama kiitwacho CCM baada ya Muungano wa ASP na TANU".

Dowload hapa chini sasa..

Amazon.com: Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi (Afrikaans Edition) eBook: YERICKO NYERERE: Kindle Store

Wewe kila kazi unataka kufanya hata usizoziweza!..mara mashindano ya kiswahili mara udalali na sasa unauza vitabu...lkn poa tu watu kama nyinyi lazima muwepo hata nchi zilizoendelea watu kama wewe wapo
 
Mkuu uzuri wa Maalim Mohamed Said hata ikiwa saa 6 usiku atajibu tuu,nadhani muda huu yupo kwenye ibada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani tuvute subira
Anavuta pumzi akisubiri issue ijirekebishe kidogo apate pa kuingilia na kuanza sema wewe hujui mimi ndie najua. Nimeongea na kusikia toka kunywa cha farasi. Halafu apige porojo za futari kadhaa na Sykes etc. Kisha Watu waki potea ndio anaanza lazimisha hadithi zake anzoziita historian ya kweli.
 
Anavuta pumzi akisubiri issue ijirekebishe kidogo apate pa kuingilia na kuanza sema wewe hujui mimi ndie najua. Nimeongea na kusikia toka kunywa cha farasi. Halafu apige porojo za futari kadhaa na Sykes etc. Kisha Watu waki potea ndio anaanza lazimisha hadithi zake anzoziita historian ya kweli.
Nicholas humjui Mohamed Said unamsoma humu JF hujawahi kukutana nae,Mimi nafahamiana nae binafsi,Mwezi huu Mtukufu yupo kwenye ibada na ukitaka anapofanyia ibada nitakutajia hayo mambo ya porojo Maalim hana muda nayo.
Lakini pia mimi nawafahamu kina Sykes hizo porojo hawana muda nazo. Kuwa mstaarabu.
 
Kwani ajui acha wivu wa kike huo yericko mwenyewe umemsikia kutoka kwenye kinywa chake akimwita mwalim mohamed said hayo ndio matatizo yetu watu weusi tuna roho za kwa nn sna
Yericko kamu ita mwalimu lakini hakusema huyo said yupo sahihi. Na si kila mwalimu anajua kiasi cha kutosha. Ndio kampa majibu ili kumweka ktk usahihi.
Mzee said ndio atajisema km ni kwamba hajui au kaamua potosha makusudi.
 
Nicholas humjui Mohamed Said unamsoma humu JF hujawahi kukutana nae,Mimi nafahamiana nae binafsi,Mwezi huu Mtukufu yupo kwenye ibada na ukitaka anapofanyia ibada nitakutajia hayo mambo ya porojo Maalim hana muda nayo.
Lakini pia mimi nawafahamu kina Sykes hizo porojo hawana muda nazo. Kuwa mstaarabu.
Ulichoandika hapa ni porojo zake. Kwa hiyo kaacha mwezi na kuja kuandaa mazingira ya kuingia ktk hoja? Alichoandika kinajisema chenyewe jinsi jamii zenu ilivyo vulnerable kwa umbea, rumors, conspiracy theorems etc.

Tatizo sihitaji njia km unavyotaka. Hoja zake km zinahitaji nijue ndipp nizikubali ipo kazi. Ina maana baada yake muda na hoja hazitowashawishi viazi vijavyo visivyomjua.

Sishangai waumini wenzie mlivyoamua mpiga jack . Na mwisho mmewaaminisha wengine habari potofu. Said+zitto+ponda= lunatism.

Huwa mna akili ndogo sana, Imeingia kwa I'd ingine uanze hutengeneza km mvha Mungu ila hujasahau ingia palepale nilipo Sema. Kamjua Sykes. Km kamjua kutia mfanya na Sykes kuwa mkweli.
 
Yaani watu wakishindwa kujibu hoja za mtu au kuunga mkono huwa busy kutafuta vichochoro
kumbe ujasusi wa kidola kitabu kiko makini..last year kwenye uchaguzi nilivyowaona wale masister pale mikumi wakimpokea rais wetu nikawaza nje ya box,..leo yametimia lile shirika na mkuu wetu wapo kisiasa zaidi..mwaka ule hawakutoa waraka wao kwa waumini ila lipo wazi.,.
 
Hawa wazee , na wale political science pale mlimani wamepewa kick za design km za zitto ili wapotoshe sana watz na mwisho mikoa kati yao ipate mizizi. Siku zao zahesabika. Wasomi vibaraka wanaumbuka kila siku. Na siku moja maharamia wa nchi kavu waliouza waafrika wenzao na baadae kuitwa mashujaa, watapewa majina stahiki.
 
Ulichoandika hapa ni porojo zake. Kwa hiyo kaacha mwezi na kuja kuandaa mazingira ya kuingia ktk hoja? Alichoandika kinajisema chenyewe jinsi jamii zenu ilivyo vulnerable kwa umbea, rumors, conspiracy theorems etc.

Tatizo sihitaji njia km unavyotaka. Hoja zake km zinahitaji nijue ndipp nizikubali ipo kazi. Ina maana baada yake muda na hoja hazitowashawishi viazi vijavyo visivyomjua.

Sishangai waumini wenzie mlivyoamua mpiga jack . Na mwisho mmewaaminisha wengine habari potofu. Said+zitto+ponda= lunatism.

Huwa mna akili ndogo sana, Imeingia kwa I'd ingine uanze hutengeneza km mvha Mungu ila hujasahau ingia palepale nilipo Sema. Kamjua Sykes. Km kamjua kutia mfanya na Sykes kuwa mkweli.
Sishangai, chanzo cha chuki yako hiyo ni Dini yako! Ila jiongeze kidogo wazungu waliokuletea hiyo dini washaishtukia, they are no longer believing in it
 
Back
Top Bottom