Majibu ya H Kigwangalla kwa Bashe na wapambe wake

Majibu ya H Kigwangalla kwa Bashe na wapambe wake

Kuchasoni Kuchawangu

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2012
Posts
623
Reaction score
378
Najua mnaumia sana jinsi tunavyofanikisha kuleta maendeleo kwa wat wa Nzega.Halmashauri zote nchini huwa zina bajeti ya'capacity building' sema huwa hazipati pesa kwa ajili hiyo. Capacity building inasaidia kukuza weledi na uelewa wa watu na nishughuli nyeti sana katika kuleta maendeleo:in fact kwenye mpango wa Taifa wa maendeleo wa miaka mitano, human capacity development (kuendeleza rasliman watu) ni kipaumbele, na mpango huu unatokana nailani ya uchaguzi ya CCM. Sisi katika halmashauri tulipopata pesa kutokana naushuru wa huduma kutoka mgodini tulitumia akili sana kusema tuziweke katika akaunti maalum ya fixed deposit ili izae na itupatie pesa kwa ajili ya semina na ziara kwa waheshimiwa madiwani (ambazo kila mwakahuwa haziji kwenye bajeti). Pesa ya mwanzo iko pale pale. Kuna watu walinipinga sana wakati nikianza harakati za kudai pesa hizi wakiwemo viongozi wa chama na watu wanaotamani nafasi niliyonayo kwa sasa,walisema wanasubiri wajifunze kutoka kwangu aina mpya ya siasa na uongozi, sasa wameona naamini wamejifunza. Nashangaa leo wamekuwa mstari wa mbele kudai wanajua tena kuzipangia matumizi pesa hizi.Kuna watu walipinga ziara ya madiwani na wabunge kwenda Dodoma kufuatilia maswala mbalimbali yanayohusiana na ufuatiliaji wa hizi pesa,leo wanaibuka na kujidai wanajua zaidi matumizi yake.Kuna watu wanaomba hizi pesa wajenge mradi wa CCM (w) hata utaratibu hawaelewi kuwa hilo haliwezekani,hii ni mali ya umma siyo ya CCM. Yote haya yanaibuka leo kwa sababu watu hawaelewi utaratibu na wanaongozwa zaidi na chuki dhidi ya Kigwangalla na mafanikio anayoyapata katika utekelezaji wa majukumu yake.Wana Nzega na watanzania muwakatae hawa na msikubali wawavuruge.
 
Kigwangalla anatakiwa afikishwe mahakamani kwa uhaini wa kujitajirisha kupitia msamaha wa kodi! Kwa nchi za ulaya unaenda jela bila ubishi!! Unaitumia nzega Kama kivuli cha kuficha ufisadi!
 
Jee Kigwangwala kuweka pesa bank badala ya kufanya kazi za maendeleo ni sawa?taratibu za serikali zinaruhusu hivyo?Kumbe kuna wenzenu wa halmashauri zingine hutumia pesa za umma kwa ajili ya manufaa binafsi ya CCM.
 
HK kwenye nchi zilizoendelea angekuwa anashusha mzigo kwenye Ndoo!
 
aloandika hapo ndo huyo anaeitwa dk hamis kigwangwala au msaidizi wake ni mbungee aya bana
 
Hao ndio wabunge wa ccm chini ya uongozi wa katibu wao mkuu aka mzee wa ivory
 
Nilidhani vijana watakapochukua nafasi za uongozi italeta tija kumbe ni uozo tuu sasa haya yanayosemwa ya kigwangala hata kama ni tuhuma tuu lakini ni udhaifu mkubwa kwa vijana wa sasa hiyo dhana sasa naifuta

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Anajaribu sana kujitetea huyu jamaa ili aonekane msafi.

Kama hajajibu zile tuhuma za kodi kwenye gazeti la Tanzania Daima watu hatutamuelewa hata kidogo. HKigwangalla yupo humu ajitokeze ajibu. akijibu huko fb aje na hapa ajibu. Tunahangaika wakati yeye ni member tena verified member. akiacha haya mambo yaendelee basi itakuwa ni kweli iwapo hatatoa maelezo aidha ya kikubali kama muungwana ama kukanusha kwa hoja na ushahidi shadidi.
 
Last edited by a moderator:
Kwa vyovyote hapo hizo fedha zilizowekwa fixed deposit zilikuwa na shughuli maalumu kwa ajili ya halmashauri, najaribu kujiuliza wakati hizo fedha zipo bank (sijui ni miezi 3 au 6 au mwaka), shughuli zilizopangwa zilikuwa zinatekelezwaje maana kwa uzoefu katika halmashauri zetu nyingi fedha huwa ni kikwazo na hata kama budget imepitishwa si kwamba zile hela zipo mikononi bali zinaendelea kukusanywa. Kama halmashauri ilikuwa ina ziada katika akaunti zake kiasi kwamba wakaweka fixed deposit basi hongera zake mheshimiwa huyu otherwise naendelea kujiuliza tu
 
Salaam,

Kigwangala ameleta Maswali mengi bila Majibu;

Nilitegemea mambo aliyosema yangejibu maswali yafuatayo;

1. Utaratibu gani wasioujua hao anaowasema?

2. Pili hiyo interest ya fixed account ni tshs ngapi?

3. Maendeleo aliyoyapeleka Nzega ni yapi?Ambayo yanatokana na nguvu yake ya ziada?

4. Viongozi gani wa chama chake waliopinga 'harakati' za kudai fedha hizo?

5. Kipi kinachofanya aone wenzake wanajifunza zaidi toka kwake na si yeye kujifunza kwa hao wanaoitaka nafasi 'aliyonayo sasa'

6. Kwann aimize watu kuwapuuza wanaohoji baadhi ya mambo na si kuwasisitiza wawajibu kama 'wanaNzega' ndiyo wanajua faida ya maamuzi aliyowahi fanya?

Kuna wakati unapoulizwa kitu,yakupasa ujibu kwa msaada wa elimu yako huku ukiweka pembeni mtazamo wa 'nani kasema' hili kutoa majibu sahihi.

Nikipata majibu ya haya,nitaona jibu limepatikana,otherwise nachukulia "business as Usual"

Naomba kuwasilisha.


Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Hiyo Avarter yako inafanana na Mafilili kunani?
 
Kwa huo uandishi unamfanya msomaji awe na kazi mbili kusoma na ku edit.
 
Huyu ale ubunge wa mwisho mwisho
 
Sijawahi ona mbinge mbae hana hata chembe ya hekima au busara kwenye kichwa chake kama mbunge wa nzega, sikuzote kakalia ugomvi tu akiulizwa hivi yeye huelekeza kwingine na anapenda sana kuongeza maadui kila siku, Grow up man aaa.
 
Sio mfuasi tena wa sera za kuwa SISI VIJANA TUPEWE NAFASI ZA UONGOZI!

Kama vijana wenyewe ndiyo hawa akina Bagaile wanaowaza ni vipi watatumia misamaha ya mabilion ya kodi kujilimbikizia mali basi ni HERI TUWAACHE WAZEE AKINA Malecela waendelee kutuongoza!Kama vijana wenyewe ndiyo hawa akina Bagaile waliokwenda kukopa BOT lkn kurudisha mkopo hadi leo wanapiga chenga ni heri waendelee akina WASIRA kutuongoza!

Ethics za vijana wetu akina Lusinde u p u u z i mtupu!
 
Back
Top Bottom