Miaka mitatu unapata degree kama ukisoma full-time, na siyo part-time evening classes. Na ndiyo maana ameweka usanii hapo kwenye red kutaja miaka mitatu na associate degree. UDSM haikumpa mnyika associate degree.
Kwa ufupi haka kajamaa ni kakilaza haka.
Kwa hili naona 'Kilaza' ni wewe hapo unayepotosha watu humu JF.
Huna ruhusa ya kuzungumza jambo ambalo ama hulifahamu vema ama hujalifanyia utafiti. Kuna watu mbalimbali walio graduate ndani ya miaka mitatu na kupata degree zao kule Open University, Mzumbe na kwingineko ambao walikuwa ni part time students. Ni mwaka jana Nape Nauye alipata degree ya MBA (Mzumbe) na laikuwa ni part time student na alipata ndani ya miaka miwili kama wanafunzi wengine ambao walikuwa full time.
Kama ulikuwa hufahamau ni hivi; mtu anakuwa kwenye program kama part time student anaweza kuchukua kozi load ya kozi zote zinazo takiwa kama full time student pale anapokuwa ana uwezo. Na pale anapokuwa hana uwezo au ana majukumu mazito basi (kuna open option) kuwa anaweza kuchukua kozi chache zaidi (mbili na hata moja akitaka kwa kila semester) ambapo itamchukua muda mrefu zaidi ku graduate. Hivyo wacha kupotosha watu kwa jambo usilolijua. Wachina walisema.... 'No Research No Right to speak'