Maji ya Ndanda yapigwa marufuku mkoani Mtwara

Maji ya Ndanda yapigwa marufuku mkoani Mtwara

mbogyo

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2012
Posts
231
Reaction score
100
kampuni ya ndanda pure spring water ya mkoani mtwara imefungiwa kwa mda usiojulikana. Hii ni kutokana na kubainika kuwa maji yake yaliyopo sokoni hv sasa ni machafu. Akiongea na radio pride ya mjini hapa, afisa afya wa mkoa amesema sampo ya maji hayo imepelekwa dsm mamlaka yachakula na dawa ili yafanyiwe uchunguzi kuona km uchafu huo una athari zpi kwa mlaji na kwamba tayari ameshapeleka barua kwenye kampuni hyo kusimamisha shughuli za kiwanda hcho. Source Amka Na Pride Fm
 
hizi ni fitna za biashara za akina bakhresa,walianza kuyafanyia fitna yasifike dar,haya maji yanapatikana mwisho rufiji tu,ni maji pure na mazuri sana,yakiingia sokoni dar wakina uhai na kilimanjaro kwisha habari yao...
 
kuanzia mtwara,tunduru had songea ndo tunatmia hayo maji na ni cheap. kuhusu uchafu sijui ila yapo poa
 
hizi ni fitna za biashara za akina bakhresa,walianza kuyafanyia fitna yasifike dar,haya maji yanapatikana mwisho rufiji tu,ni maji pure na mazuri sana,yakiingia sokoni dar wakina uhai na kilimanjaro kwisha habari yao...

Wanasema ukiua kwa upanga na wewe utauwa kwa upanga. Hizi fitina walinyiwa kampuni inayotoa Maji Afrika Iringa, na katika kipindi cha wiki moja toka maji Afrika kuwa machafu ndipo wakazi wa Iringa tuliposhuhudia brand mpya ya maji yaitwayo Ndanda. Sina uthibitisho kuwa Ndanda ndio walioifanyia fitina Maji afrika ila uingizwaji kwa wingi wa Ndanda water katika kipindi kifupi tu kunaweza kutufumbua macho.
 
Kwa kweli maji ya ndanda ni matamu na hayana mfano!!

Fitna tuu za wafanyabiashara




kampuni ya ndanda pure spring water ya mkoani mtwara imefungiwa kwa mda usiojulikana. Hii ni kutokana na kubainika kuwa maji yake yaliyopo sokoni hv sasa ni machafu. Akiongea na radio pride ya mjini hapa, afisa afya wa mkoa amesema sampo ya maji hayo imepelekwa dsm mamlaka yachakula na dawa ili yafanyiwe uchunguzi kuona km uchafu huo una athari zpi kwa mlaji na kwamba tayari ameshapeleka barua kwenye kampuni hyo kusimamisha shughuli za kiwanda hcho. Source Amka Na Pride Fm
 
Yale maji ni mazuri ever in tz,alafu yana nembo ya Tbs tangu kiwanda kianze uzalishaji.,ubora huo ulitokea wapi.
Mbali na mengi,nahisi na jamaa wa pride mtwara nao wanahusika ktk fitina kwani ni mmoja wa share holders wa kiwanda kingine cha maji(brand name nimesahau)
 
Mmxxsuuuuuu fitna tu. itabainika tu maana fitina titi la paka halifai kwa mtindi.
 
Fitina tu hizo, hakuna lolote, hakuna maji matamu kama NDANDA!
 
haya ni mapya. Songea ndio maji na yanapendwa sana kwa sasa. Cha msingi ni kututangazia mapema utafiti huo. Kama ni fitna za kibiashara bas inatisha.
 
kuna kipindi mi pia niliacha kuyanywa nilikua nikinywa naskia yana harufu ya vumbi...tangu hapo nakunywaga kama hamna maji mengine
 
Yale maji ni mazuri ever in tz,alafu yana nembo ya Tbs tangu kiwanda kianze uzalishaji.,ubora huo ulitokea wapi.
Mbali na mengi,nahisi na jamaa wa pride mtwara nao wanahusika ktk fitina kwani ni mmoja wa share holders wa kiwanda kingine cha maji(brand name nimesahau)
USISHANGAE kukuta hata huyo bwana afya ametumika kwa ujinga tu.mimi nisipo kunywa NDANDA SPRING WATER silali.nahisi kuna kitu kinaendelea kwani hata kabla ya tangazo la leo tayari kuna baadhi ya baa walikuwa wameshaanza kuuza maji ya kutoka Dar.
 
Nilikwenda Mtwara kufika Nangurukuru
kuuliza Kilimanjaro hakuna ni Ndanda tu

nadhani watu wa kusini acha walilie
maji yao kufungiwa huko.

Nimesikia kuna haya Maji yanaitwa
Dew yanapatikana Katavi eti ya Pinda.
 
hizi ni fitna za biashara za akina bakhresa,walianza kuyafanyia fitna yasifike dar,ni maji pure na mazuri sana,yakiingia sokoni dar wakina uhai na kilimanjaro kwisha habari yao...

Maji gan wewe? Ph 8. Siyo pure water
 
Wanasema ukiua kwa upanga na wewe utauwa kwa upanga. Hizi fitina walinyiwa kampuni inayotoa Maji Afrika Iringa, na katika kipindi cha wiki moja toka maji Afrika kuwa machafu ndipo wakazi wa Iringa tuliposhuhudia brand mpya ya maji yaitwayo Ndanda. Sina uthibitisho kuwa Ndanda ndio walioifanyia fitina Maji afrika ila uingizwaji kwa wingi wa Ndanda water katika kipindi kifupi tu kunaweza kutufumbua macho.

Nimezunguka Tanzania. Maji Mengi yanachumvi. Maji ambayo ni mazuri na ni baridi ni(kwa test yangu mimi binafsi): Ndanda Springs-Mtwara, Kilimanjaro- Kilimanjaro,Rungwe- Mbeya, Ruwenzori- Nilikunywa Mwanza( niliambiwa yanatoka Uganda sina uhakika). Kuna maji fulani yapo Dodoma( nadhani FURAHA).Kosa la Ndanda ni kuwaachia wahuni wachukue.chupa zao hasa pale Stendi ya Basi Lindi, bila jamaa kunitonya ningekunywa tope, yaani wauzaji wadogo wanachukua chupa za maji ya Ndanda wanaweka maji ya Bomba halafu wanauza eti ni Ndanda. Nashangaa wenyewe Ndanda wanakaa kimya badala ya kuwachukulia hatua wanakaa kimya. Ngoja wale ban ndo watakuwa makini kufuatilia bidhaa zao
 
Back
Top Bottom