Alwaz
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,115
- 10,822
Nchi imefikia pabaya kuhusiana na mgao wa umeme.Uchumi unaporomoka kwa kasi.Ukijiuliza maswali utashindwa kupata jibu huku ukijua kwamba Tanzania ina vyanzo vingi vya maji.Bado nchi inakumbwa na ukaukaji wa maji kuliko hata nchi zilizo jangwani.
Kwa watu wenye akili hawapaswi kuendelea kulalamika tu na kushutumiana kwa jambo ambalo haliko kwenye uwezo wa watanzania na wala si utaalamu pekee wenye kuweza kutatua mkwamo huu.
Kwa upande wangu napendekeza maji yatolewe sadaka kwa ajili ya mambo ya kiibada.Misikiti na makanisa yapatiwe maji ya bure ili waumini wayatumie kwa shughuli zinazohitaji maji kwenye majengo hayo.
Kwa kuanzia ifanyike tathmini ya idadi ya matumizi ya maji ya kila muumini anayetumia majengo hayo.Baada kupatikana takwmu idara husika zitoe kiwango kulingana na takwimu hizo.Usomaji mita ufanyike kama kawaida na pindi kiwango kikivukwa basi malipo yafanyike kutokana na ziada hiyo.
Kinyume chake maji kwa viwanda kama vya pombe yalipiwe mara 100.Na hata wakitaka kuchimba kisima maji yatakayopatikana yalipiwe sawa na yale yanayotolewa na mamlaka za maji.
Kwa watu wenye akili hawapaswi kuendelea kulalamika tu na kushutumiana kwa jambo ambalo haliko kwenye uwezo wa watanzania na wala si utaalamu pekee wenye kuweza kutatua mkwamo huu.
Kwa upande wangu napendekeza maji yatolewe sadaka kwa ajili ya mambo ya kiibada.Misikiti na makanisa yapatiwe maji ya bure ili waumini wayatumie kwa shughuli zinazohitaji maji kwenye majengo hayo.
Kwa kuanzia ifanyike tathmini ya idadi ya matumizi ya maji ya kila muumini anayetumia majengo hayo.Baada kupatikana takwmu idara husika zitoe kiwango kulingana na takwimu hizo.Usomaji mita ufanyike kama kawaida na pindi kiwango kikivukwa basi malipo yafanyike kutokana na ziada hiyo.
Kinyume chake maji kwa viwanda kama vya pombe yalipiwe mara 100.Na hata wakitaka kuchimba kisima maji yatakayopatikana yalipiwe sawa na yale yanayotolewa na mamlaka za maji.