Umewahi tembelea kiwanda au mgodi? Basi huko kuna maji yanayotumika kupozea mitambo,kusafishia bidhaa n.k. Hayo maji hayana tofauti na maji kutoka kwenye AC. Nikiwa shule ya msingi mzee amewahi leta AC mbovu (SANYO) toka Ofisini kwake kwa utundu wangu nilifungua ili niibe mota. Ukifungua AC kasha lake lile kwenye yale matundu ya wavu utaona kila aina ya uchafu,nzi,vipepeo,memde,vumbi,utando wa buibui n.k. Hiyo feni inayopiga hewa,hewa hiyo hukusanywa,hupulizwa na kisha hugandamizwa ndani ya kasha hilo ndipo hutengeneza hydrogen mbili H2 na Oxygen moja 0 na ndipo tunapata maji (H20). Maji hayo hukutana na vitu hivyo,kutu,vumbi,utando,mende,buibui,vipepeo,virainisho vya mota,mabaki ya msunguano wa vyuma vya mota,grisi,kutu n.k. Hivyo maji hayo ni maji machafu sawa na yale ya mgodi wa dhahabu yenye mecury. Hapa ndipo tofauti yetu sisi na wazungu kufikiri inapokuja kwa muungwana kutumia maji haya.
Jaribio: Kagua pale ambapo maji hayo yameamwagikia kwenye sakafu au marumaru,yaache yakaukie hapo usiyafute,utakacho kibaini njoo ushee hapa na sisi watu wa bara la giza.