KERO Maji Malamba Mawili ni mgao mkali, baadhi ya Wakazi walio kwenye miinuko wana miezi hawapati maji kutokana na kasi ndogo ya maji. DAWASA wafafanua

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,239
4,272
Malamba Mawili maji ni ya mgao yanaweza maliza wiki 2 bila kutoka na yakitoka yanatoka usiku wa manane yakitoka kidogo kidodo, yanachirizika hayana kasi hata kidogo kiasi ambacho baadhi ya watu ambao nyumba zao zimepo kwenye miinuko kidogo maji hayafiki kabisa.

Kuna baadhi ya watu wana miezi hawajawahi kuyaona maji yakitoka kwenye nyumba zao, wanaishi kwa kununua maji yanayouzwa na magari kwa 15000 mpaka 20000 kwa dumu lita 1000.

Napata mashaka huenda hayo magari yakawa yanamilikiwa na baadhi ya watu wa idara ya maji na kusukuma maji kwa kasi ndogo au kutosukuma maji kuyaleta Malamba kwa wiki au wiki 3 au mwezi kabisa wakati mwingine ukawa ni mpamgo mkakati wao wa kuhakikisha magari yao yanapata wateja kila siku.

Wakazi wa Malamba Mawili wanateseka sana na maji, kwa sababu ya gharama wengi hulazimika kutumia maji ya chumvi yalichombwa chini ambayo si salama, kwani mengi huwa yanakuwa yana muingiliano na mifereji ya maji machafu.

DAWASSA tatueni kero ya maji Malamba Mawili, kama mnashindwa kuyasukuma kila siku angalau yawe yanakuja hata baada ya siku 2 na yawe yanakuja kwa kasi kubwa ili hata walio kwenye miinuko wapate, pia muache kuyaleta usiku wa manane.

Natoa wito kwa Waziri wa Maji, Jumaa Aweso awaagize DAWASSA washughulikie changamoto hii kwani mara kadhaa tumeripoti lakini bado kuna kujivutavuta katika kufanya maamuzi, huku sisi tukiendelea kuteseka.

1716366508256.jpeg

Pia soma:
======

DAWASA wakiri kuwepo na tatizo la maji maeneo ya Malamba Mawili kutokana na kuwepo na vilima vikali wasema wanaendelea na jitihada mbalimbali za kufanya maboresho ya huduma za Maji katika eneo hili kwa kufanya mradi wa kuongeza msukumo wa maji kwa kulaza bomba lenye kipenyo cha inchi 8 kwa umbali wa KM 3.5 katika maeneo hayo lengo ni kuboresha huduma.

Zaidi soma: DAWASA yatoa ufafanuzi kuhusu changamoto ya maji Malamba Mawili
 
Tatizo la maji linaikumba jiji nzima, pamoja na mto Ruvu kufurika maji na umeme kutokatika lakini tatizo la maji lipo palepale na mbaya zaidi bili za dawasco hazipungui na inaongezeka. Hatuna sehemu ya kwenda kulalamika kwa sasa nchi ina shida kubwa sana upande wa uongozi.
 
Malamba Mawili maji ni ya mgao yanaweza maliza wiki 2 bila kutoka na yakitoka yanatoka usiku wa manane yakitoka kidogo kidodo, yanachirizika hayana kasi hata kidogo kiasi ambacho baadhi ya watu ambao nyumba zao zimepo kwenye miinuko kidogo maji hayafiki kabisa.
Dumu gani hili la lita 1000??
 
Ukonga banana miezi sasa maji hamna... hata sijui hawa watu Wana shida gani yaan Aweso hajui au siasa hizi mji huu maji shida na hakuna majibu shida ni nini
 
Malamba Mawili maji ni ya mgao yanaweza maliza wiki 2 bila kutoka na yakitoka yanatoka usiku wa manane yakitoka kidogo kidodo, yanachirizika hayana kasi hata kidogo kiasi ambacho baadhi ya watu ambao nyumba zao zimepo kwenye ero ya maji Malamba Mawili, kama mnashindwa kuyasukuma kila siku angalau yawe yanakuja hata baada ya siku 2 na
Chadema wakifanyaga Maandamano ya amani huwa mnatoka? Wacha myoshwe
 
Mimi hapa Malamba mawili sijapata maji bombani kwangu tangu mwaka 2023 mwezi wa pili,
Kiukweli tunateseka sana.

Kibaya zaidi kumekuwa na majibu ya kiss asa yasiyokuwa na mwisho kutoka Kwa Meneja na viongozi wa idara ya maji pale Kibamba.

Inashangaza, Malamba mawili tunakosa kabisa maji, lakini Kinyerezi wanapata huduma hiyo Kwa masaa 24.

Mambomba yanapita Malamba mawili kwenda Kinyerezi, lakini hapa maji tunanua ya ndoo mpk 800 tzs
 
Nadhani kuna mitambo dawasco huwa wanaizima ili kupunguza pressure kubwa ya maji ambayo husababisha kupasuka kwa mipira na uvujaji wa maji mkubwa sana.

Shirika la dawasco kama mashirika mengine yaliyopo chini ya serikali yanaendeshwa chini ya watu wasio na uwezo wa kusimamia na pia wasioweza kudeal na changamoto zinazohitaji personal initiative kutatua.

Nilishawahi hoji haya mambo nikapata majibu kadhaa .

1. Inaonekana kuna ufisadi mkubwa ulifanyika katika manunuzi ya mipira kwaajiri ya kuunganisha line mpya za maji. Mipira iliyonunuliwa ni ile milaini ambayo ni rahisi kupinda, kupasuka na kuachia kwenye bomba kubwa endapo pressure ya maji itaongezeka. Ukitaka kujiridhisha kuhusu hili swala nenda hapo nje kwako tazama Bomba zilizowekwa na Dawasco kwenye line yako ya bomba halafu fananisha na ile mipira ya zamani waliyoweka NUWA. Mipira ya zamani ni migumu na haizidiwi nguvu na pressure ya maji, inaitwa "type C" nenda Hardware store ulizia utaiona.

2. Kipindi cha magufuli kulifanyika maboresho makubwa sana ya mifumo ya maji ikiwamo kufungwa kwa pump kubwa na zenye nguvu za maji ili kusaidia pressure ya maji kuwa kubwa na kufikisha maji maeneo ya mbali zaidi.

Kumbuka zamani kila mwenye tanki alilazimika kununua pump ya kupandisha maji kwenye tenki juu na ilikuwa lazima uchimbe karo la kukusanya maji yakijaa pump ianze kuyapandisha kwenye tank ila kipindi cha magufuli hali ilibadilika watu walikuwa hawatumii tena pump sababu ya pressure kubwa ambayo ilipandisha maji kwa kasi kwenye kwenye matenki bila msaada wa pump.

Hizi power station pump kutokana na nguvu yake kubwa zilipelekea hizi line za mabomba cheap kupasuka kila uchao na kulisababishia taifa hasara kutokana na kuvujisha maji 24/7 ambayo husukumwa kwa umeme na ni gharama sana, mafundi kurepair ni zoezi la kila siku sababu mipira hafifu ilikuwa inapasuka kila uchao na kuharibu mazingira kwa kuchimbua barabara na kuweka madimbwi ya maji.

Kinachochangia zaidi mipira kupasuka ni idadi kubwa ya wateja wa Dawasco hawana matenki na huhifadhi maji yao kwenye ndoo chache ndani na pengine majaba mawili. Hivyo demand dongo huku pressure ya kusukuma maji ikiwa kubwa inachangia kupasuka kwa mipira hii dhaifu. Ukilinganisha na masaki ambapo ukiacha tu demand kubwa ya maji kuna easy flow na miundo mbinu yao walitengenezewa zile bomba za type C ambazo hazipasuki kizembe. Muda wote kule watu wanaflush na kutumia maji so inabalance pressure ya maji yanayoflow kwenda kule ushuani.

Ila huku kwa swekeni ni kila watu watakinga maji dakika 30 au masaa mawili wakijaza tu ndoo basi mabomba yanafungwa the pressure ya maji inaanza kujaa na hatimae mipira inaanza kupasuka na kuachia kutoka katika main pipes za maji au kwenye joints maji ya atapakaa kila kona.

So nadhani Dawasco wanazima hizi power stations na kuziwasha kwa muda mdogo ili kubalance pressure na kupunguza gharama na hasara za shirika.

But hii sio suluhu ya kudumu, suluhu ni kumtafuta mshenzi aliyefisadi hela ya mipira hadi wakafunga mipira hafifu na kulipa shirika hasara.

Mipira ibadilishwe yote wafunge ile migumu yaani type C halafu wanainchi waelimishwe umuhimu wa kuwa na matenki kuanzia lita 5000 hadi 20,000 ya kuhifadhi maji na kuwa na direct usage ndani ya nyumba yaani kusiwe na mambo ya kukinga maji kwa kopo au ndoo nje bali chooni, jikoni kuwe na koki na mifumo ya maji mtu atumie direct akihitaji maji ili kuweza kusaidia kubalance pressure ya maji kutoka katika zile power stations.
 
Huduma ya maji Dar nzima imekuwa hovyo kabisa. Yaani inashangaza namna mambo yanavyorudi nyuma haraka baada ya JPM kufariki.
 
Mimi hapa Malamba mawili sijapata maji bombani kwangu tangu mwaka 2023 mwezi wa pili,
Kiukweli tunateseka sana.

Kibaya zaidi kumekuwa na majibu ya kiss asa yasiyokuwa na mwisho kutoka Kwa Meneja na viongozi wa idara ya maji pale Kibamba.

Inashangaza, Malamba mawili tunakosa kabisa maji, lakini Kinyerezi wanapata huduma hiyo Kwa masaa 24.

Mambomba yanapita malamba mawili kwenda Kinyerezi, lakini hapa maji tunau ya ndoo mpk 800 tzs
Pole sana mkuu. Wanasema tatizo ni nini?
 
Kwa case ya Mbezi na dawasa (hawa umbwa waliojimilikisha cheo cha kugawa uhai wa maji wanavyotaka wao) ni tofauti na maeneo mengine ya jiji,Magomeni maji yasipotoka huwa hitilafu ukanda wa Mbezi huwa hujuma.

Mbezi vipo vi-canter 2tons vimesajiliwa kabisa ubavuni vina sticker za dawasa kuviruhushu kuuza maji base yao ipo hapo Daraja la Mto Mbezi I think kipindi fulani palikuwa na office za dawasa,wamiliki wake (wapemba wa Mbezi Msakuzi na wachagha wa Mbezi Makabe) ndiyo remote ya kufungua maji ukanda huo,hao jamaa huchanga kiasi cha pesa per month wanahonga injinias na mameneja wa kanda yenu wasifungue maji ili mnunue kwenye hivyo vigari na ile midumu yao isiyooshwa

Hayo wanayofungua kidogo ambapo hayana pressure ya kupanda kwenye matank yaliyosimamishwa target yao huwa ni kwa ajili ya matajiri waliochimba visima vya chini wapate maji kwa sababu tajiri akikosa maji yeye ana connection kubwa ya kuripot juu akawachoma tofauti na maskini zaidi ya kusubiri mkutano wa chama hana namna nyengine ya kufanya huku akinunulishwa maji,zikikaribia siku za kusoma meter wanafungua mengi usiku kwa masaa mane mgombanie kisha wanafunga asubuhi unakutana nao kwako wakikagua Mita yako kesho yake unatumiwa bill yako iliyoongezeka tofauti na matumizi yako maisha yanaenda
 
Kesho njoo tuandamane kwa amani kupata haki yetu na kudai kodi tunayolipa kila siku
 
Pole sana mkuu. Wanasema tatizo ni nini?
Huwa hakuna tatizo lolote.

Unakuta gate valve handle yupo stuff wa dawasa anatembea nayo kwenye bag mgongoni yaani kitu ilibidi kikae stoo ili iwe rahisi kwa utendaji wa taasisi kinamilikiwa na mtu mmoja,so asipokuwepo au akiwa na nia yake ovu wananchi wanateseka na ndiyo maana inakuwa rahisi hata kwa wafanyabiashara kumuhonga.

Na utawala huu huyo waziri wa maji alikuwa anapiga piga kelele kipindi kile kwa manufaa ya kisiasa siku zaidi ya kuongeza wake na kuwapeleka bungeni kuwaringia wenzake hana kingine.
 
Back
Top Bottom