Majeshi yetu

Majeshi yetu

TPDf...Tanzania peoples defence force liko na tofauti gani na JWTz mkuu?
 
Hebu tupitie kwa ufupi aina ya majeshi yetu na majukumu yake ya kila siku
-JWTZ- hili ndio kama jeshi kuu linalihusika na ulinzi na usalama wa mipaka yetu....naweza kusema ndio jeshi mama na mara chache kuonekana mitaani na linapoonekana mitaani kwenye mavazi yao rasmi ujue hali sio shwari sana... (kuna haja ya kuwa na mjadala kwenye jina)

-JPT/TPDF/TP- Hili ni jeshi la polisi Tanzania, ndio jeshi lililozoeleka zaidi kwa wananchi ndio jeshi linalihusika na kushughulika na maisha ya kawaida ya kila siku ya mwananchi! Kuanzia usalama wa ndani, nyaraka mbalimbali, kesi , hukumu vifungo hata misamaha na madawati ya jinsia na kwa sehemu msaada wa kisheria...! Tungeruhusu mijadala ya wazi hili ndio lilipaswa kuitwa Jeshi la wananchi

-JKT- Jeshi la kujenga Taifa , hili ni jeshi la damu changa madhumuni yake ni kuwafundisha vijana wote wanapomaliza elimu ya kidato cha sita nk uzalendo ukakamavu na stadi anuwai kabla ya kuendelea na elimu ya juu....hapa kuna nguvu kazi kubwa sana inapotea bure nguvu kazi ya kujenga taifa katika nyanja mbalimbali kuanzia kilimo ufundi ufugaji mpaka biashara na sayansi na teknolojia... kile kitengo cha SUMA-JKT kama kungekuwa na uhuru wa majadiliano kingepaswa kipelekwe JKT na wanajeshi waachiwe jukumu lao la msingi

-JLMT- Jeshi la mgambo Tanzania, hili ni jeshi ambalo sio rasmi sana likiwa haitofautiani sana na polisi jamii (kitengo kinachoelekea kufutwa awamu hii)haya ni majeshi ya msingi lakini yasiyopewa kipaumbele sana...haya ndio yanajua kila kitu nyumba kwa nyumba mtu kwa mtu na mtaa kwa mtaa...tungekuwa na mijadala huru hili tungelijadili kitaifa ili iwe ndio msingi rasmi wa majeshi yote na kuwe na program maalum zinazohusika na kutambulika kisheria

-Tuna majeshi mengine kama ya zimamoto nk lakini haya hayawezi kuwa sehemu ya mjadala kwakuwa ni vitengo ndani ya jeshi la polisi

Je katiba yetu inatuambia nini kwenye dhima na utayari wa kuwa na mijadala kama hii?

Nawasilisha....!!!
Hakuna jeshi la zimamoto bali ni kikosi cha zimamoto na uokoaji pia uhamiaji sio jeshi bali ni idara ya uhamiaji!
 
Mmh hapana japo kwa tafsiri ya kiswahili ni mlinda usalama wa Mali na RAIA
Kuna mahala nilipitia kukuta kama sikosei
P-people
O-offences
L-liberty
I-investigation
C-criminal
E -enforcement
Kwa haraka haraka sikuangalia viunganishi, sijui kuna ukweli hapo?
 
Kuna mahala nilipitia kukuta kama sikosei
P-people
O-offences
L-liberty
I-investigation
C-criminal
E -enforcement
Kwa haraka haraka sikuangalia viunganishi, sijui kuna ukweli hapo?
Hakuna mantiki yoyote kwenye hiyo ordha. Police ni neno moja linalotaja taaluma mojawapo kama zilivyo taaluma nyingine kama vile mwalimu, daktar n.k
 
Vipi hawa MP...militiary police kaz zao ni zipi hasa??
 
Hakuna mantiki yoyote kwenye hiyo ordha. Police ni neno moja linalotaja taaluma mojawapo kama zilivyo taaluma nyingine kama vile mwalimu, daktar n.k

Noted (from encyclopidea).
Thanks kasigazi kalungi for your clarification.
Kumbe niliingia chaka na kuuziwa chai.
 
Jmn km nitakuwa nimekosea naomveni mnisahihishe,JWTZ,Polisi,magereza na JKT yote hayo in majeshi ya taifa au serikali lkn kwann JKT wakimaliza mafunzo ajira zao huwa km zinasumbua sumbua hv,ukilingabisha na majeshi mengine?
 
Jmn km nitakuwa nimekosea naomveni mnisahihishe,JWTZ,Polisi,magereza na JKT yote hayo in majeshi ya taifa au serikali lkn kwann JKT wakimaliza mafunzo ajira zao huwa km zinasumbua sumbua hv,ukilingabisha na majeshi mengine?
Sijui kwasasa ikoje ila zamani ilikuwa ukimaliza form six ama chuo ndio unaenda JKT na ukitoka huko ndio unaenda chuo kikuu ama kwenye ajira yako
 
Vipi hawa MP...militiary police kaz zao ni zipi hasa??
Nadhani hiki ndio cheo cha chini kabisa cha askari au mwanajeshi
1472082416570.jpg
 
Nadhani hiki ndio cheo cha chini kabisa cha askari au mwanajeshi View attachment 387158
Hapana MP sio cheo mkuu ni kitengo ndani ya jeshi (MP:Military Police) kazi yao ni kusimamia nidhamu ndani ya jeshi..cheo cha chini ni PRIVATE hivyo MP anaweza kuwa wa cheo chochote kile endapo atakuwa amepata mafunzo ya MP.
 
Kwa hiyo tiss wanaajiri kupitia chipukizi au JKT au mgambo?, nimetoka nje ya mada?, aaaah nilitaka kusema wananchi ndiyo wenye majeshi yote, kwa hiyo imefika wakati tuwe na mkuu mmoja wa majeshi yetu yote, halafu ndiyo kuwe na wakuu wa majeshi mengine, kwa sasa CDF ndiye anaonekana kama joint chief of staff jambo ambalo kwa maoni yangu linashusha heshima ya majeshi mengine
 
Wewe jamaa hujui kitu,,,,,,,majeshi yetu na yaliyopo kwenye katiba, sheria ni jwtz, Jkt, polisi, Magereza, zimamoto,na uhamiaji imeonyeshwa kama idara sio jeshi,,,,,,,, nimekushangaa pia uliposema fire ni idara ndani ya polisi, sio kweli toka 2012 fire iliidhinishwa rasmi kuwa jeshi, chini ya commandment 1 na kuhamishiwa wizara ya mambo ya ndani bz zamani walikua tamisei
 
Back
Top Bottom