specialist88
JF-Expert Member
- Aug 31, 2014
- 1,140
- 619
Ndugu zangu,
Wiki iliyopita nilikuwa Mji kasoro bahari, a.k.a Moro town. Nilichokiona mjini pale kimenishangaza sana!
Ujenzi tu wa Moro, ni vituko, nyumba nyingi za Moro mjini (Mfano Nanenane & Kihonda) zimejengwa hovyo hovyo tu, utadhani viwanja havikupimwa. Nyumba zenyewe sasa, utadhani mjengaji alishikiwa bunduki wakati akijenga!
Nyumba hazikamiliki, nyumba zimejengwa hovyo hovyo kama magodauni, unakuta jumba kubwa lakini halina shepu, halijakamilika, vyoo sasa, daaaah! Kiufupi ni hovyo hovyo tu...
Sasa nikawa najiuliza;
1. Hizi nyumba mjengaji ni mmoja?
2. Nani anaidhinisha ramani zao. mpaka waanze kujenga?
3. Kwanini mtu ahangaike kujenga lijumba likuuubwa kama hawezi kulimudu gharama za umaliziaji na asijenge kajumba kadogo kazuri?
4. Hivi wakazi wa Moro, hawaendagi miji mingine kama Moshi, Mwanza, Babati, Dsm, Sumbawanga na kadhalika wakajionea watu wanavyojenga nyumba nzuri?
5. Kama wanaona, kwanini hawatamani?
6. Kama wanatamani, kwanini na wao hawaji kujenga mji wao vizuri?
Naomba kuwasilisha!
Wiki iliyopita nilikuwa Mji kasoro bahari, a.k.a Moro town. Nilichokiona mjini pale kimenishangaza sana!
Ujenzi tu wa Moro, ni vituko, nyumba nyingi za Moro mjini (Mfano Nanenane & Kihonda) zimejengwa hovyo hovyo tu, utadhani viwanja havikupimwa. Nyumba zenyewe sasa, utadhani mjengaji alishikiwa bunduki wakati akijenga!
Nyumba hazikamiliki, nyumba zimejengwa hovyo hovyo kama magodauni, unakuta jumba kubwa lakini halina shepu, halijakamilika, vyoo sasa, daaaah! Kiufupi ni hovyo hovyo tu...
Sasa nikawa najiuliza;
1. Hizi nyumba mjengaji ni mmoja?
2. Nani anaidhinisha ramani zao. mpaka waanze kujenga?
3. Kwanini mtu ahangaike kujenga lijumba likuuubwa kama hawezi kulimudu gharama za umaliziaji na asijenge kajumba kadogo kazuri?
4. Hivi wakazi wa Moro, hawaendagi miji mingine kama Moshi, Mwanza, Babati, Dsm, Sumbawanga na kadhalika wakajionea watu wanavyojenga nyumba nzuri?
5. Kama wanaona, kwanini hawatamani?
6. Kama wanatamani, kwanini na wao hawaji kujenga mji wao vizuri?
Naomba kuwasilisha!