Wapi tunaweza kujua hii nyumba ni contemporary mkuu??
Hapo ni umechukua fundi ambae hana utaalamu wa kuweka mapaa ya aina hiyo.Video inajieleza
Kuna rafiki yangu kajenga hii nyumba
Kumbe gypsum boards zipo kitambo sana. I thought zamani hzo tng ndio zilikua zikitambaHapo ni umechukua fundi ambae hana utaalamu wa kuweka mapaa ya aina hiyo.
Wakati nilipokuwa nikijenga nyumba yangu (early 90s) utaalamu wa kutumia gypsum boards ulikuwa bado uko kwa mafundi wachache. Fundi wangu aliniambia anajua kuweka gypsum na alinipa estimate, lakini kumbe wala hakuwa akijua kwani yeye alikuwa fundi wa kuweka 'hardboards'.
Nilipokwenda dukani basi yule mwenye duka akawa anaulizia 'mbona kitu fulani na fulani hakuweka kwenye hesabu?'. Ndipo hapo akaniambia huyu fundi wako hajui kuweka hizi gypsum ataharibu bure. Niliporudi kumuuliza akaniambia ni kweli hajawahi kuweka na alidhani ni sawa na kuweka zile hardboards.
Mafundi wengine hawataki kukiri kwamba kazi aina fulani hawaijui baadae wanaishia kukupa hasara wewe mwenye nyumba.
Zipo kitambo lakini wengi tulikuwa tunaona ni ghali sana na mafundi walikuwaw wachache. Na zamani hazikuwa zinawekwa nakshi nakshiKumbe gypsum boards zipo kitambo sana. I thought zamani hzo tng ndio zilikua zikitamba
Fundi Juma kashafanya yake
Kina adriz atajitetea et alikuwa anawahi kuswaliFundi Juma kashafanya yake 🤣